Kuna ushahidi wowote wa faith healing

Kuna ushahidi wowote wa faith healing

Maybe you can help Me. I had a strong faith before, lkn baada ya kuomba na kuombewa sana na tatizo langu halijaisha yaani saivi nikiona, kusikia au kuambiwa habari hizi za maombi ya uponyaji najikuta nimevurugwa kabisa najiuliza wanaoamini na kupokea wanaamini vipi mbona Mimi sipokei hiyo miujiza. Hebu sema chochte mkuu
Kwanza nishukuru kwamba umeamini naweza kukusaidia!Hata hivyo I can only lead you into believing that you can receive your healing from the Lord Jesus Christ,anayeponya ni Kristo.

Katika kitabu cha Isaya 53:5 ile sehemu ya mwisho ya msitari kuna maneno haya,"Na kwa kwa kupigwa kwake sisi tumepona." Brother, maneno haya yanatuhakikishia kwamba the redemption work of Jesus Christ at Calvary brought a new whole dimension in our lives,including healing!But this healing can only be granted if you believe that indeed Jesus Christ heals.If you don't believe or if you doubt, you can't receive your healing.Siwezi kusema wewe una matatizo gani,but asses your faith,inaelekea tatizo lipo hapo.Faith of the person being healed is the most important factor.Tunaona hii sehemu nyingi katika Biblia.Katika kitabu cha Matayo 8:13,Bwana Yesu anamwambia Akida mmoja ambaye mtumishi wake alikuwa mgonjwa,"na iwe kwako kama ulivyo amini,mtumishi wake akapona saa ile ile." You see faith has a strong connection to your healing.

And how do you believe that Jesus heals,through hearing the word of God(Rumi 10:17:Basi imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la Kristo).

You see,huwezi kupokea uponyaji kama huamini kwamba yeye anayekupa uponyaji anaponya.Kama ukipona bila kuamini kwamba Kristo anaponya,aliyekuponya hatakuwa Kristo Yesu,itakuwa ni nguvu nyingine.

I hope through these few words, I have managed to convince you that indeed you can be healed through faith in our Lord Jesus Christ.May the Lord bless you brother.
 
Imani yako ndio itakayokuponya, Kinyume na hapo usitegemee miujiza.
Mleta mada mjinga Fulani hivi hajui hata biashara ni imani unafungua duka unakaa kusubiri mteja usiemjua aje kununua biadhaa yako.Huna imani huwezi fungua duka
 
Now days wachumgaji wengi wamekuwa wakitumia maombi kwa njia amabazo c sahihi,wengi ni kwa ajili ya kukipatia kipato..

But all in all...Faith healing is real na inafanya kazi sana,namshukuru MUNGU kwa kunifunilia hilo na kinipa huo use so.
 
Nilikuwa shafanyiwa matibabu na sikuona unafuu zaidi ya kuongeza tatizo LA maumivu kurudi hospital dr akanipa za kupunguza maumivu nakuniambia maumivu hayaishi na hali ya hewa ikibadilika tu maumivu, so siku hyo nilivornda church sikutegemea aisee maumivu yote yaliisha
Kwahiyo siku ulipokuja kuumwa ugonjwa mwengine, je uliacha kwenda hospitali tena na kuendelea na maombi?? Kama uliendelea kwenda hospital baada ya hapo.. why??
 
Hahaha mi nadhani ukiisha kuwa na imani hupaswi kuombewa, tayari unayo imani, unaamini kwanini uombewe?! Kwanini usijiimbee mwenyewe ukapona?!
Kama huna imani ndiyo unaombewa na hao wanaotoza pesa kuombea watu. Mbona Yesu aliwaombea wenye uhitaji bure na hakuna sehemu inasema alijipatia kipato kwa kuwaponya wagonjwa?!
Halafu kama Yesu ni Mungu na Mungu ni Yesu, kwanini msimuombe na Mungu baba pia?!
Spiritual healer hawana vyeti na hawakusomea kuwa spiritual healer, hivyo hawakulipia ada na hawana sababu kutoza pesa ku heal mtu.
Ulichobarikiwa bure kwanini ukitozee pesa?!
Wanawake wanaouza maungo yao tunawaita majina kama malaya na vyangudoa.
Spiritual healer unapotoza pesa kuponya ukiitwa tapeli ni sawa kabisa.
Wito wangu Kama wenye imani ndio hupona, wajiombee wenyewe kwa imani zao waachane na matapeli.
 
niliumwa macho miaka 12 ikiyopita. nikaenda kwa wataalamu wakanipa miwani. nikatumia kama mwenzi hivi nikasema sitaki kuvaa miwani. nikamwomba Mungu kwa bidii aniponye nikaachana na miwani hadi sasa ni historia na hakuna tatizo lolote la macho.

niliwahi kuwa na uvimbe unaanza kidogokidogo, ukawa mkubwa kidogo. sikuwa na pesa ya hospital nikamwomba Mungu kwa bidii aniondolee ukaondoka na ukuaji wake ukakoma.

kuna mtu alitolewa kizazi na akamwomba Mungu ampe mtoto. alienda kuzalishwa na daktari huyohuyo aliyemtoa kizazi. daktari akabaki anataharuki imekuwaje. (hii nilielezwa na mtu wa karibu na mtu huyo).

nimewahi kushiriki na mdau wangu mmoja kumuombea dada aliyekuwa haongei (bubu) na hatembei. Baada ya kuondoka akiwa amepoteza fahamu alipozinduka mzazi wake kwa furaha akapiga simu huku akimshukuru Mungu kuwa mtoto wake anatembea na kuongea.

nadhani hapa sio suala la huyu anaponya au haponyi. fact ni kwamba Mungu anaweza kuponya hata kufufua. ila kama watumishi wake wengine ni wasanii hilo halizuii uwezo wake....
 
Dini ziko nyingi na karibia zote zina uponyaji wa maombi,ila kwenye ukristo imekuwa ni huduma kabisa ambayo wakati mwengine mwenye kuhitaji anapaswa kulipia na hata wale wasio na imani kwa Yesu pia hukaribishwa kwenye huduma hiyo.
 
Dini ziko nyingi na karibia zote zina uponyaji wa maombi,ila kwenye ukristo imekuwa ni huduma kabisa ambayo wakati mwengine mwenye kuhitaji anapaswa kulipia na hata wale wasio na imani kwa Yesu pia hukaribishwa kwenye huduma hiyo.
Mkuu utapeli aina hiyo ulikuwepo hata enzi za Mt. Paulo. Ninavyoona mimi kwasisi wabantu,ni rahisi sana kumwamin mganga wa kienyeji kuliko biblia. Nakubaliana na wewe manabii na mitume wanaishi maisha ya kutanua sana kwa sadaka na zaka za wapendwa katika bwana na hawataki uhoji matumizi.
 
Katika mitume na manabii yuko mmoja wa zamani sana. Kabla hawajatokea akina upako,efatha,gwajima n.k nilifiwa na mdogo wangu pale siwahaji. Baba alifadhaika sana kwasababu wote walokole na tulimwomba sana Mungu bw mdogo akatuaga akiwa mdogo sana. Akaja kesho yake akatuambia yule dogo hakuzaliwa hospitali. Yaani mama zliposhikwa uchungu wakodi taxi kwenda kibena hosp njombe iko nje ya mji. Ikashindikana wakachepuka pembeni ajifungue. Akamwambia mama anawakumbuka wa mama watatu waliomsaidia .Akatuambia wawiki kati yao walikuwa wachawi na ameishi miaka mingi kwa neema ya Mungu. Mama alipoulizwa alifiki kila kitu.

Bahati nzuri au bahati mbaya mtu wa Mungu huyu alitabiri 2015 siasa za Tanzania kabla ya uchaguzi.Yeye hapayuki payuki.Kwa jinsi ninavyomwamini mi naangalia movie inavyoendelea.

Msaada toka Mungu sio magonjwa tu,ni pamoja na mazingira tuliyomo n.k.

Karibuni kwa Yesu
 
Kwahiyo siku ulipokuja kuumwa ugonjwa mwengine, je uliacha kwenda hospitali tena na kuendelea na maombi?? Kama uliendelea kwenda hospital baada ya hapo.. why??
Sasa hapo uumwe usinywe dawa siku kosa maarifa ndo mana Mungu akatuumbia maarifa tuyatawale mazingira kwa kutupa akili. Mi maombi hufanya kila siku ninapoamka kwa pumzi
 
Sasa hapo uumwe usinywe dawa siku kosa maarifa ndo mana Mungu akatuumbia maarifa tuyatawale mazingira kwa kutupa akili. Mi maombi hufanya kila siku ninapoamka kwa pumzi
Okay, hapo kwenye maarifa nimepapenda..

Lakini hauoni kwamba utafutaji wa maarifa unaathiriwa na kuishi kwa kutegemea imani kwa sana/ kuna mambo yakihojiwa basi mtu anaehoji anaonekana ametenda kosa kubwa sana, na ukiangalia kuna uhalali wa kuhoji....
 
Nimeona niongeze shuhuda nyingine kuwasaidia imani watu wengine. Kuna watu wanadhani tunatania au hatuko seri
ous.


Wakati tunalala nyumbani mara kadhaa wife alikuwa anaona kivuli kwenye kona chenye umbile na ukubwa wa sura ya mtu. Si wote walokole. Basi hakuniambia ila alimwomba Mungu aifunue ile sura. Kwani nilikuwa naumwa sana na uchovu unazidi kila siku. Basi yule mtu alipokuja Kumbe alikuwa ni mama yangu mzazi. Yaani waligongama macho kila mtu akimtambua mwenzake wakati huo mimi nimelala. Hata hivyo asubui hakuweza kuniambia mama yangu mchawi. Angeanzia wapi illa nilishangaa mama akija maana tulikuwa hatukai wote,alikuwa anapenda kumchukua binti yangu wa kwanza miak 10 anaenda bafuni kuoga nae. Mke wangu alipomuuliza binti yangu akasema wamavua nguo zote wanaoga na hii ni mchana kabisa.Nilikuja kujua kama mama ni Witch toka kwa mch wa mbali na hapo ninapokaaa. Akaniambia mama alianza kunichukia nilipogoma uchawi. Ili nichukua muda mrefu sana kuvuta kumbukumbu. Moja mama alijaribu mimi nilale nae akaja chumban amevaa koti refu ndani chupi nyeupe,nilikuwa nimeenda kumtembekea kwake Moshi aliachana na mzee. Au kwa usahihi yeye alimpa talaka mzee. Eti hhafla mle chumbani wakati amesogelea kabisa kitandani akajidai koti limemponyoka kwa mbele akabaki uchi,na chupo yske nyeupe. Kilichonishangaza alionekana kufuatilia reaction zaidi akiniangalia sana usoni. Pili wakati niko Iringa nimeend kumtembelea ghafla akaniambia niwafuate vijana fulani nikaongee nao. Wale vijana waliniambia kwa habari ya mademu nidihangaike,wanaweza kunipa dawa nikamwingilia demu yeyote usiku na kumaliza haja zangu zote mi nilikataa nikaona issue yeyote inayohusu kuingia kwenye nyumba usiku ni uchawi. Wakarudisha ripoti kwa mama aliyekuwa anasubiti nje kwamba nimekataa.

Kwa hiyo huyo mch. Alinipa live mama ni mchawi. Sasa ikawa haiwrzrkani kumkwepa danabu lazima aje kusalimia.

Hii stori ni ndefu kwa kifupi tulikazana kwenye maombi,siku moja wife alimwona mam kwenye ndoto anamuaga anaenda safari. Akamfuata kule anakokaa majohe akamwambia live mbona nimeota uniaga. Akamjibu ni kweli alikuja kumwaga sababu atakufa muda sio mrefu. Hata hivyo ilipia miezi 2 na nusu hivi,ghafla akaanguka akitokea bafuni. Alipokuwa znapelekwa Muhimbili akasema wanahangaika nini kwani yeye ameshakufa ila roho haijatoka. Alimaliza maisha yake psle muhimbili ila cha kushangaza wakati bado mzima tukimwambia atubu akasema ameshachelewa nafasi hiyo haipo tena. Mi naendelea vizuri kwa wale wote shaka na Yesu nadhani hii habari itawatia moyo. Ni baadhi ya vituko vingi ambayo tumekutana navyo kupambana ibilisi. Wenye kudhaki sisi hatujapewa mamlaka eti kumpigania Mungu. Atakutana na wewe utajua leo nimekutana ns Muumba. Uponyaji upo,ila michsnganyo ni kweli imezidi.
 
Okay, hapo kwenye maarifa nimepapenda..

Lakini hauoni kwamba utafutaji wa maarifa unaathiriwa na kuishi kwa kutegemea imani kwa sana/ kuna mambo yakihojiwa basi mtu anaehoji anaonekana ametenda kosa kubwa sana, na ukiangalia kuna uhalali wa kuhoji....
Kuna kutafta maarifa ya kidunia na technology lakini maandiko yasema technology yangu Mungu ni kuu sana imeshinda yote. Mie mwenyewe niliumwa na vipimo vya binadamu havikuonyesha kitu nakilichokuwa chanisumbua ni extra thing ya kiroho so mkuu hii dunia yetu ni zaidi ya mambo ya akili za kibinadamu kabisa.
 
Yesu anaponya (kwa Mungu hakuna linaloshindikana) Mungu hutumia watu katika uponyaji huo (ila sio wa upako)
 
Hakuna kitu complex kama swala la imani..lakini nikwambie kitu MUNGU YUPO..afu dini ya kweli ipo ndani yako namaanisha matendo yako..tenda mema na uishi maisha yako kwa upendo ukiamini mungu yupo ...miracles will happen to you every day and you won't even notice. ...kingine wanaojiita walokole "sio wote" ila wengi wao hawaelewi nini wanafanyana
 
Mimi binafsi nimekuwa nikijiombea mara nyingi pindi ninapo ugua, huwa napona kabisa, hata watuwengine nikiwaombea nmeshuhudia wakipona mbele yangu , namshukuru Mungu katika hili.
 
Back
Top Bottom