Kuna ulazima gani wa mambo kuwa hivi?

Jeho

JF-Expert Member
Jul 2, 2011
5,053
5,503
Mwalimu wangu wa somo la jiografia alinifundisha ya kuwa dunia inalizunguka jua katika mhimili wake kwa muda wa mwaka mmoja. Pia alisema mwaka mmoja huo waweza kuwa ni siku 365 na 1/4 au siku 366. Lakini katika gregorian callendar inayotumika nchini mwetu ili mwaka uwe mfupi(siku 365 na 1) au mrefu(siku 366) inategemea mwezi wa pili una siku ngapi, kama siku ni 28 ndipo tunapata mwaka mfupi na kama siku ni 29 tunapata mwaka mrefu. Kwa mjibu wa kautafiti kangu kadogo nilikofanya ambako hakakuwa rasimi nimegundua ya kuwa ili tupate mwaka wenye siku 29 katika mwezi wa pili ni lazima miaka mitatu yenye siku 28 katika mwezi wa pili ifuatane mfano mwaka 2008 ulikuwa na siku 29 katika mwezi wa pili 2009,2010 na 2011 hii yote ilikuwa na siku 28 katika mwezi wa pili 2012 utakuwa na siku 29 katika mwezi wa pili 2013, 2014 na 2015 itakuwa na siku 28 katika mwezi wa pili. Sasa huu utaratibu unatokana kweli na mzunguko wa dunia au unatokana na kuwekwa na wanadamu? Kwa anayefahamu anieleweshe juu ya umhimu wa miaka mitatu kuwa ni mifupi(yenye siku 365 na 1/4) ikifuatiwa na mwaka mmoja ambao ni mrefu(wenye siku 366). Handsome wa mama nawasilisha.
 
simple mathematics, approximation nadhani inatumika hapo.
Namba ikiwa 365.25, round off to 365 huu ni mwaka wenye siku 28
afu 365.75 round off to 366 huu uwe mwaka wenye siku 29

sasa kumbuka ile miaka yenye siku 365.25 yoe inakuwa na siku 28, kwa hiyo take 365.25-365=0.25,
hizi robo siku za miaka mitatu hazipotei hewani, lazima wanazi-offset kwenye mwaka wa nne kupata siku nzima moja na mwaka kuwa mrefu.

Kwa hiyo zile robo za miaka mitatu wanazijumlisha kwenye mwaka wa nne kupata siku nzima.

Ila kitu kinachonisumbua mie ni kujua wanacalculate vipi time difference.
Utasikia sasa hivi Utah na tz tunapishana masaa 8, mara wanatangaza tena tunapishana masaa labda 7. It confuses me.
 
nadhani umuhimu wa kwanza wa kufanya hivi ni i kuweza kupanga tarehe na masaa kwa urahisi zaidi. Bila ya hivyo ile robo ingekuwa inakaaje?
 
simple mathematics, approximation nadhani inatumika hapo.
Namba ikiwa 365.25, round off to 365 huu ni mwaka wenye siku 28
afu 365.75 round off to 366 huu uwe mwaka wenye siku 29

sasa kumbuka ile miaka yenye siku 365.25 yoe inakuwa na siku 28, kwa hiyo take 365.25-365=0.25,
hizi robo siku za miaka mitatu hazipotei hewani, lazima wanazi-offset kwenye mwaka wa nne kupata siku nzima moja na mwaka kuwa mrefu.

Kwa hiyo zile robo za miaka mitatu wanazijumlisha kwenye mwaka wa nne kupata siku nzima.

Ila kitu kinachonisumbua mie ni kujua wanacalculate vipi time difference.
Utasikia sasa hivi Utah na tz tunapishana masaa 8, mara wanatangaza tena tunapishana masaa labda 7. It confuses me.

kwa hiyo haitokani na mzunguko wa dunia bali na calculations za kibinadamu, naomba unieleweshe zaidi maana sijakusoma zaidi mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom