Kuna ubaya gani kufuatilia nyendo za mpenzi wako?

MTENDAHAKI

JF-Expert Member
Mar 3, 2011
4,013
1,443

attachment.php

Ni wiki nyingine tulivu kabisa tunakutana kupitia safu hii nikiamini umzima na unaendelea nyema na maandalizi ya sikukuu za Christmas na Mwaka Mpya.

Mimi namshukuru Mungu kwa kila jambo ambalo amekuwa akinitendea katika kila siku ya maisha yangu na nimuombe tu anijaalie niwe miongoni mwa wale watakaouona mwaka 2015 wakiwa wazima.
attachment.php

Mpenzi msomaji wangu, kilio cha wengi walio kwenye uhusiano ni kusalitiwa na wapenzi wao waliotokea kuwaamini sana. Wapo ambao si tu kwamba wanahisi bali wanawafumania kila kukicha waume/wake zao licha ya imani waliyokuwa nayo kuwa hawawezi kusalitiwa.

Imefika wakati baadhi yetu hatutaki hata kufuatilia nyendo za wenza wetu tukijua kwamba kufanya hivyo ni kujitafutia presha za bure. Labda mimi naweza kuwa na uelewa tofauti katika hili la kufuatilia nyendo za wapenzi wetu. Ninachojua mimi ni kwamba, ili uwe na amani moyoni mwako juu ya mwenza wako lazima uthibitishe kama kweli anakupenda na ametulia.

Utafanya hivyo kwa kufuatilia nyendo zake bila yeye kujua na katika kufuatilia kwako ndipo utajua kama kweli umempata mwenza sahihi ama laa. Wapo ambao husimamia kwenye ule msemo kwamba, ukimchunguza sana bata humli! Jamani ule ni msemo tu, tunajua kila mmoja ana mapungufu yake ila ni vyema ukayajua ya wako ili ujue namna sahihi ya kuishi naye.

Nalazimika kusema haya kwa kuwa, kasi ya wapenzi kusalitiana imekuwa ikishika kasi kila siku kiasi cha baadhi kuhisi bila kusaliti hawasikii raha. Yaani wanapatilizwa kila kitu na wenza wao lakini bado wanatoka nje.

Unakuta mwanaume ana mke mzuri anayejua mapenzi na kila kitu lakini bado mwanaume huyo haridhiki. Pia wapo wanawake ambao wamebahatika kuwapata wanaume ‘handsome', wanaojua mapenzi na kujali pia lakini bado tamaa za usaliti wanakuwa nazo. Ukiuliza kipi kigeni wanachofuata huko nje, jibu hakuna.

Watu wa sampuli hii ni vyema kuwabaini kuliko kubaki na ile imani kwamba, anakupenda na hawezi kukusaliti. Una ushahidi gani kama kweli anakupenda na hakusaliti huko anakopita?
Hivi leo ukiambiwa utaje sababu inayokufanya uamini kuwa mwenza wako hachepuki utatoa sababu gani? Hakika huwezi kuwa nayo, sanasana utaishia kusema unamuamini kwa kuwa hujawahi kumfumania wala kuona dalili za kuzungukwa.

Kizuri ni kwamba, ukifuatilia sana utagundua wengi wetu hutuna imani ya asilimia 100 ya kutosalitiwa. Wengi wetu licha ya wenza wetu kuonyesha wametulia, bado hatuwaamini kupitiliza. Hii yote ni kwa sababu akiamua kukusaliti anaweza kufanya hivyo na wewe usijue lolote.

Nilishawahi kufanya uchunguzi huko nyuma kwa kuzungumza na baadhi ya watu kuhusu hili suala la kusalitiwa. Wengi walikiri kujua kwamba wanasalitiwa lakini wenyewe wanadai ni mambo ambayo wakiyafuatilia hawawezi kudumu kwenye ndoa zao.

Ni kweli niliobahatika kuongea nao kwenye hili ni wachache sana lakini maelezo yao yamenifanya niwe na uhakika wa hiki ninachokiandika leo.

Kipi kifanyike?
Kutokana na maelezo yangu hapo juu utakubaliana na mimi kwamba hakuna anayeweza kusimama mbele za watu na kuthibitisha kuwa hasalitiwi. Kikubwa ni wewe na mimi kuwaamini wapenzi wetu.
Lakini pia hakuna ubaya kama utafuatilia na kujua kama kweli uliye naye ametulia na hachepuki. Usibaki kuamini kibubusa kwamba husalitiwi, wakati mwingine fuatilia nyendo zake bila yeye kujua.

Najua kweli ukifanya hivyo unaweza kugundua madudu mengi kwa huyo uliyenaye na ukajikuta unachanganyikiwa lakini ni bora utakuwa umejua yaliyojificha ili uchague mwenyewe kusuka au kunyoa.
Heri ujue kisha kama huwezi kumuacha, uzungumze naye, abadilike kuliko umuache aendelee kufanya ufuska wake gizani kisha wewe ubaki na imani kwamba ametulia na hawezi kukusaliti.

Lakini kama moyo wako unagoma kumfuatilia mpenzi wako na moyo wenyewe unakuhakikishia kwamba mwenza wako katulia, basi baki na imani yako hiyo.Lakini kwa ulimwengu wa sasa kama utakuwa umejihakikishia kwa asilimia 100 kwamba una mpenzi ambaye hajawahi kukusaliti na wala hafikirii, jiweke kwenye kundi la watu waliobahatika na Mungu awabariki sana.

Source:http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/kuna-ubaya-gani-kufuatilia-nyendo-za-mpenzi-wako
 

Attachments

  • love.jpg
    love.jpg
    48 KB · Views: 2,161
  • spy.jpg
    spy.jpg
    26.2 KB · Views: 2,084
Ukimfatilia sana utapata BP isiyo kua ya lazima chamsingi mweleze vp unataka muishi hiyo ndio muhimu tabia ya mtu kuibadili tabu sana...........
sio suala la kuibadili, kama hawezi bora uanze upyaa, au kama vipi umvumilie lakini unamjua vyema
 
Inauma sana kuwa na MTU ambaye hakuamini....Why kufuatiliana? We muamini in the name of love. ...hayo ya gizani IPO Siku yatakuja mwangani...halafu itakuwa aibu yake sio yako....

Huwezi kumchunga binadamu kwa kumfuatilia hivyo....just love n trust him/ her....

Trust yako inatosha kuwa mfuatiliaji....amini MTU hawezi kumcheat MTU anayemwamini......ila ukimuhisihisi ndo aweza kufanya kweli.....si humuamini? Bora afanye kweli yaishe......
 
kwa nini mawazo yako uyapeleke kwenye usaliti?? ni heri uzungumze naye pasi kuweka akilini anakusaliti .. maana ukishaweka dhana ya usaliti utahangaika kutafuta usaliti kwa lazima pasi hata kuwepo
cha msingi usijiumize moyo kwa kutafuta magonjwa ya moyo
 
Inauma sana kuwa na MTU ambaye hakuamini....Why kufuatiliana? We muamini in the name of love. ...hayo ya gizani IPO Siku yatakuja mwangani...halafu itakuwa aibu yake sio yako....

Huwezi kumchunga binadamu kwa kumfuatilia hivyo....just love n trust him/ her....

Trust yako inatosha kuwa mfuatiliaji....amini MTU hawezi kumcheat MTU anayemwamini......ila ukimuhisihisi ndo aweza kufanya kweli.....si humuamini? Bora afanye kweli yaishe......
Na akikuletea ngoma
 
Dawa ya MTU kukuhisia mabaya usiyofanya,unampa likizo ya kujiona yeye msafi fanya yako na wala hatokuwa na cha kuhoji kupata attention
 
Back
Top Bottom