Kuna tatizo, mungu anaanza kukosea sasa

Kuna tatizo, mungu anaanza kukosea sasa

Alisha sema watatokea manabii batili
Hii ni dalili ya kiama
 
Ukipata muda angalia chanel inaitwa WRM kwenye startimes .....utaona jinsi watu wanavyopigwa na mtume/nabii
 
Mitume na manabii wanaoibuka kila leo hawana tofauti na wale wa kale, tofauti tu ni kwamba zama zimebadilika science na technology jinsi inavyokua imetufunza mambo mengi sana kiasi inakuwa vigumu kuwaamini
 
Sio bure wewe mtoa post unalaana,tena umelogwa naona

Hata hao watakao kukuunga mkono kwa Matapishi yako hao watakuwa wamelaaniwa.
 
Mungu hajawahi kukosea na hawezi kukosea na hii sifa hana kabisa! Wanao loses ni sisi binadamu wenyewe huwezi kwa zama hizi kumuita mtu nabii kama una akili timamu! Hawa wanaojiita haya majina ya Nabii hawanatofauti na hawa wanaojiita maraisi wakati hawaongozi hata mtaa. Hivyo nao ni wasanii katika hiyo tasnia yao ya maigizo kwenye dini!
 
Kuna kitu kikubwa naona mungu anafanya makosa kwa sasa, nikisoma maandiko mbalimbali nagundua kuwa Mungu alikuwa anawaleta mitume na manabii kwa awamu.

Si hivyo tu, alikuwa anawaleta kwa uchache tena kwa maeneo maalumu hususani yale korofi. Pia alikuwa anawaleta kwa dalili na hoja zilizo wazi, pia ikitokea zama moja kuwa na manabii au mitume wawili au zaidi kwa wakati mmoja basi walikuwa wanaheshimiana sana.

KOSA, ni hawa manabii aliowaleta leo sijui kwanini amewabadilisha hivi;

1. Wanahubiri zaidi kutafuta na kumiliki mali kuliko ufalme wa Mbinguni.

2. Anawaleta wengi kwa pamoja halafu wengi wanashukia mijini, mfano Dar es salaam pekee si ajabu kukuta manabii au mitume mpaka 10.

3.Mitume na manabii anaowaleta kipindi hiki hawapendani yaani ukiwasikiliza kimtindo utajua wanapondana tu.

4. Huduma za maombi kwa hawa manabii wa sasa ni za kulipia.

5. Wengi ni matajiri wakubwa sana sio kama enzi zile za kina Ayubu, Yusufu Abraham/Ibrahim n.k.

Yako mengi wakuu..
Una uhakika gan kam yeye ndo kawaleta hao?
 
Mamitume na manabii ya zama hizi ni mashetani na yametumwa na ibilisi kwa ajili ya utimilifu wa nyakati na maandiko
 
Wewe jamma una Laana! Yani ulefikia hatua ya kumkosoa Muumba wa Mbingu kama hauna la kusema si ukae kimya kwani lazma uwanzishe Uzi

Hapo Dar hakuna Mtume wala Nabii hao wote ni Waongo matapeli wa mjini siku moja aliojiwa mtu mmoja anaedai kuwa yeye ni Mtume na kituo cha TBC akiwa kavaa suti na Cheni Shingoni sasa kweli Mtume / Nabii anaweza kuvaa Cheni shingoni?
Bila shaka hawa ndio walinganizi wanao waita watu kuingia Motoni ?

Hawa Wanaojiita Mitume/Manabii ni watu waovu sana kuliko hata walevi wa Kilabuni...!
well said mkuu...umeniwakilisha vyema
 
The bible has so many ambiguous, contradictory and complex situations, such that if you really want to challenge it, utaishia pabaya, that's why I'd rather remain to be a moderate christian, than being conservative and radical.
 
Watakupinga hapa na kukukejeri ila nimekuelewa.
 
Mtoa Mada ana akili sana unatakiwa utulie uweze kumuelewa Angalia hizi sentesi.
kuna kitu kikubwa naona mungu anafanya makosa kwa sasa

nikisoma maandikombalimbali nagundua kuwa Mungu alikuwa anawaleta mitume na manabii kwa
awamu

Mtoa mada anazungumzia pande mbili tofauti mungu ambaye anakosea na Mungu ambaye aliwaleta
manabii enzi hizo.

Mzee wa kurekebisha saf sanaa jwel w n great thinker
 
Kuna kitu kikubwa naona mungu anafanya makosa kwa sasa, nikisoma maandiko mbalimbali nagundua kuwa Mungu alikuwa anawaleta mitume na manabii kwa awamu.

Si hivyo tu, alikuwa anawaleta kwa uchache tena kwa maeneo maalumu hususani yale korofi. Pia alikuwa anawaleta kwa dalili na hoja zilizo wazi, pia ikitokea zama moja kuwa na manabii au mitume wawili au zaidi kwa wakati mmoja basi walikuwa wanaheshimiana sana.

KOSA, ni hawa manabii aliowaleta leo sijui kwanini amewabadilisha hivi;

1. Wanahubiri zaidi kutafuta na kumiliki mali kuliko ufalme wa Mbinguni.

2. Anawaleta wengi kwa pamoja halafu wengi wanashukia mijini, mfano Dar es salaam pekee si ajabu kukuta manabii au mitume mpaka 10.

3.Mitume na manabii anaowaleta kipindi hiki hawapendani yaani ukiwasikiliza kimtindo utajua wanapondana tu.

4. Huduma za maombi kwa hawa manabii wa sasa ni za kulipia.

5. Wengi ni matajiri wakubwa sana sio kama enzi zile za kina Ayubu, Yusufu Abraham/Ibrahim n.k.

Yako mengi wakuu..
Unataka kutuambia Hawa wote tunaowasikia matapeli?
 
Wajinga hawaishi, hao wahubiri wamechangamkia fursa....hakuna nabii kipindi hichi, manabii enzi hizo walilingania dini walipigwa na kufanyiwa dhihaka za kila aina na wengine waliuwa sasa hawa wahuni tuu
 
Hakika ni mungu wako tu ndio hukosea kwa kuleta mitume na manabii, Mungu wangu alishafunga mjadala wa mitume na manabii.
Namjua mtume wa mwisho na wa kwanza. Na tangu amekufa mtume wa mwisho sijasikia wala kuina tena kiumbe kina jinadi kua yeye ni mtume.

Ushauri wangu kwako mtoa mada jaribu kufanya utafiti inawezekana huko uliko sio sehemu sahihi ndio maana unakutana na uzushi kama huo.
 
kuna watu ni wapumba.. asee,, hivi unawezaje kumkosoa Mungu na una hakika hao mitume na manabii uchwara wametumwa na Mungu ??
 
Back
Top Bottom