Kuna Tatizo gani benki ya CRDB?

Kuna Tatizo gani benki ya CRDB?

Kufuatilia mkopo wapo, nadhani unajua anapata commision kwa kila mkopo unao kamilika.. so anakuona mtu muhimu sana.

Hutakiwi kumpa hata cent 5.

Siyo kila taasisi inampa loan officer commission. Tena nyingi ni target driven,loan officer usipofikisha kwa muda flani kazi huna. Na wengi wanaotoa kitu kidogo ni wafanyabiashara na lengo ni kutengeneza mazingira mazuri baada ya mkopo(marejesho). Loan officer akiamua kufuata sheria kabisa za marejesho,unaweza kuichukia Taasisi. Ila mfanyakazi haina haja ya kubembeleza sana kwani Taasisi nyingi zinawatafuta
 
Kufuatilia mkopo wapo, nadhani unajua anapata commision kwa kila mkopo unao kamilika.. so anakuona mtu muhimu sana.

Hutakiwi kumpa hata cent 5.
Utakuwa ulizaliwa miaka ya 1960s mpaka 1970s... kwa msamiati unaoutumia.

Wa siku hizi wangisema, hutakiwi kumpa hata mia! / jero / buku...
 
CRDB kupata mkopo baada ya mwezi 1 hata kama umejaza na kurudisha form.
Huwa wanadanganya mfumo lakini si kweli wanatoa kwa mafungu.
CRDB imeondoka na Kimei
 
Benki ya kifala sana hii kwa sasa, wapo na huduma yao ya e-banking wanahimiza watu kujiunga ila bado wako zama za mawe hawa jamaa. Wiki jana nilitoka nje ya nchi kidogo nikataka kutuma chochote kwa familia hii "system"yao inagoma haitoi password, kutafta msaada kwao zaidi ya wiki mbili hakuna solution wafanyakazi hawajielewi mpaka mameneja wao kwenye hiki kitengo cha e-banking, non-proffessional kabisa sijui wanawaokota wapi. Well, safari bado ni ndefu.

Kweli kabisa.
Juzi nime download app yao.
Nikaweka taarifa zote.
Mwisho ikagoma .

Makato sim banking ni makubwa sana.
 
Kuna rafiki yangu alijaza fomu ya kuomba mkopo ilichukua wiki 3 ndio akapata. Nikamuuliza loan officer akaniambia wana shida kwenye system yao. Nikamuuliza tena nikianzisha mchakato inachukua muda gani kupata,akaniambia hana uhakika maana makao makuu ndio wanazingua.
Baada ya kama wiki moja tena nikamuuliza,akaniambia ni bora nicheki kwingine maana kwao kwa sasa system haieleweki. Anasema wamewaandikia barua makao makuu ili wawaelekeze mfuko utakaa sawa lini,makao makuu wamepiga kimya hawajibu.
 
Siku zote hakikisha loan officer una namba yake.
Na uhakikishe hiii kitu unampiga mara kwa mara
FB_IMG_1613022110348.jpg
 
Tulikubaliana kuwa huduma za kibenki bila longolongo nenda ABSA BANK mkopo ndani ya masaa 24 kwa riba ya 15%,hakuna haja ya kuhamisha mshahara kwani pesa yako ya mkopo utaingiziwa kwenye account unayopitishia mshahara kwenye benki yako.
Hao CDRB wana liquidity issue ila hawataki kuwa wawazi and bad enough wateja wakienda kuchukua settlement letter wanamuwekea amount sawa na inayoonekana kwenye payslip hii kitu haikubaliki popote ila kwa kuwa mmeaminishwa kuwa benki ni CRDB na NMB basi kaeni kwa kutulia dawa iwaingie vizuri.
Hao ABSA utaratibu wao wa mikopo ukoje mkuu?
 
Back
Top Bottom