Kuna Tatizo gani benki ya CRDB?

Upo Kama mimi
 
Mimi nimeamua kuachana na posi yao siwezi Kuwa mtumwa wao yaani unafanya muamala karibu 400 kwa mwezi unachoambulia ni cha hivyo kabisa.
 
Mkuu mbona Kuna bank nzuri zenye international exposure Kama AbSa bank ila watu mnang'ang'ania hizo saccos maana sion Kama Zina hadhi ya kuitwa bank.
 
sio hapa tu sasa hivi Mikopo CRDB hawatoi kama ilivyokuwa mwanzo na kwa Wafanyabiashara na wajasiliamali ndio kabisa.
CRDB kuna matatizo ya kifedha ni miezi karibu 5 sasa-inakwenda kufilisika hii Bank.

Mkui hamia Bank nyingine.
Benki nyingi zitafilisika kwani kwa sasa wote wanapigania kudhibiti akaunti za TRA zaidi ambao pesa zoa hazikopesheki kwa wateja wengine.Angalau hizi akaunti za TRA zinawafikisha mahesabu ya kubaki na kiwango cha uhai kwa mujibu wa BOT.
 
Tulikubaliana kuwa huduma za kibenki bila longolongo nenda ABSA BANK mkopo ndani ya masaa 24 kwa riba ya 15%,hakuna haja ya kuhamisha mshahara kwani pesa yako ya mkopo utaingiziwa kwenye account unayopitishia mshahara kwenye benki yako.

Hao CDRB wana liquidity issue ila hawataki kuwa wawazi and bad enough wateja wakienda kuchukua settlement letter wanamuwekea amount sawa na inayoonekana kwenye payslip hii kitu haikubaliki popote ila kwa kuwa mmeaminishwa kuwa benki ni CRDB na NMB basi kaeni kwa kutulia dawa iwaingie vizuri.
 
CRDB now imekuwa ya ajabu mno ingawa naitumia.mkuu kwenye mikopo mwalimu commercial bank wapo vizur ingawa wanakukata kwanza then ndo wanakupa.ila kwenye top up wapo vizuri sana.mi nilipofanya top up,siku nilipopitisha kwa HR nikawatumia.baada ya saa 5 mzigo ukaingia ndani ya cku moja.yaani nilifurahi hadi nikasahau machungu ya kukatwa.
 
Hili tatizo lipo CRDB tangu mwaka Jana August, kuna baadhi ya matawi yalikuwa hayakopeshi kabisa, naona limeanza kwa kasi tena.

Walitoa pesa nyingi sana kwa kampeni za CCM
 
Hawa absa wananunua mikopo toka mabenki mengine?
 
Mbuzi anakula urefu wa kamba yake, usifinye sana mkono. We unakopa milioni ishirini unaona tabu kumpa mtu laki mbili?

Ukiona ugumu ndo utaishia kuzungushwa hivi. Toa kitu upate kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…