Kuna swali hapa kwa waliooa au kuolewa na kufanya sherehe: Hivi uwa mrudi kuangalia video za shughuli yenu?

Kuna swali hapa kwa waliooa au kuolewa na kufanya sherehe: Hivi uwa mrudi kuangalia video za shughuli yenu?

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
31,139
Reaction score
88,800
Katika heka heka za kupunguza gharama za uendeshaji wa harusi, kuna hii budget ya videography. Hii sekta inaongeza sana gharama na inaweza kufika Mil 2-3 kizembe sana.

Mara nyingi ukienda kwenye harusi utaona TV kadhaa zinaonesha live, macamera man kadhaa, drones na mataa ya picha. Hao ndigo kitengo cha videography ambao output yao ni kukupa picha na video kwenye USB Flash, picha za A3 na A2 kadhaa basi.

Sasa nauliza, Mbali na kupost kwenye social media, je uwa mnarudia kuangalia tena zoezi zima la harusi kuanzia sendoff, kanisani hadi ukumbini? Au kua na mpiga picha mmoja tu local ambae anaweza kulipwa chini ya laki 2 inatosha?
 
Kifungu Cha 3:4 kina sema haitakiwi kusaliti chama Cha kataa ndoa, kabla mwaka mpya hauja Anza.
FB_IMG_17554142251731119.jpg
 
Harusi yako ni tukio lako. Unatakiwa kulipangilia kwa utaratibu wako na sio namna watu wengine wanataka au mazoea.

Ukipanga tukio lako kaa na wataalamu wa Event planning wakupe ushauri mzuri wa namna ya kupangilia matukio hadi shughuli yako miaka 10 ijayo inakuwa very entertaining kuitazama.
 
Katika heka heka za kupunguza gharama za uendeshaji wa harusi, kuna hii budget ya videography. Hii sekta inaongeza sana gharama na inaweza kufika Mil 2-3 kizembe sana.

Mara nyingi ukienda kwenye harusi utaona TV kadhaa zinaonesha live, macamera man kadhaa, drones na mataa ya picha. Hao ndigo kitengo cha videography ambao output yao ni kukupa picha na video kwenye USB Flash, picha za A3 na A2 kadhaa basi.

Sasa nauliza, Mbali na kupost kwenye social media, je uwa mnarudia kuangalia tena zoezi zima la harusi kuanzia sendoff, kanisani hadi ukumbini? Au kua na mpiga picha mmoja tu local ambae anaweza kulipwa chini ya laki 2 inatosha?
Wanaangalia ndiyo. Tena wanawake ndiyo wanapenda kweli kurudia. Nikupe story moja ya kweli. Miaka ya nyuma enzi tunatumia mikanda ya video, kuna dada mmoja alisimamia harusi. Kipindi hicho picha za video kwenye harusi haikuwa common kama ilivyo sasa ila kwenye hiyo harusi walichukuwa video. Fast foward, baada ya miezi kama sita, yule dada akaibiwa vitu vya ndani pamoja na TV na ule mkanda. Mwizi akaenda kuuza kwa baba mmoja na mkewe, si mbali sana na pale alipokuwa anakukaa aliyeibiwa. Kilichotokea? Siku moja wakawa wanaangalia ile video sebuleni na wageni. Kumbe mgeni mmoja alikuwa anamjua yule dada msimamia harusi japo alikuwa hajui kuwa kaibiwa. Siku moja akakutana naye na kumueleza kuwa ameona mkanda alipokuwa anasimamia harusi. Dada machale yakamcheza, wakachukuwa polisi na kukuta vile vitu vilivyoibiwa kwa yule jamaa.
 
Tuangalie za wangapi hizo video labda wao wakiwa wametoka kuoga na ukiwa zamu kwa mwenzake
 
Wanaangalia ndiyo. Tena wanawake ndiyo wanapenda kweli kurudia. Nikupe story moja ya kweli. Miaka ya nyuma enzi tunatumia mikanda ya video, kuna dada mmoja alisimamia harusi. Kipindi hicho picha za video kwenye harusi haikuwa common kama ilivyo sasa ila kwenye hiyo harusi walichukuwa video. Fast foward, baada ya miezi kama sita, yule dada akaibiwa vitu vya ndani pamoja na TV na ule mkanda. Mwizi akaenda kuuza kwa baba mmoja na mkewe, si mbali sana na pale alipokuwa anakukaa aliyeibiwa. Kilichotokea? Siku moja wakawa wanaangalia ile video sebuleni na wageni. Kumbe mgeni mmoja alikuwa anamjua yule dada msimamia harusi japo alikuwa hajui kuwa kaibiwa. Siku moja akakutana naye na kumueleza kuwa ameona mkanda alipokuwa anasimamia harusi. Dada machale yakamcheza, wakachukuwa polisi na kukuta vile vitu vilivyoibiwa kwa yule jamaa.
Wamenunua mali za wizi halafu wanaangalia ukanda wa harusi wa alie ibiwa ngese sana hao🤣🤣
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom