Mifuko yote ya hifadhi ya jamii haiko vizuri. Naweza nisiseme moja kwa ufisadi, lakini kuna mambo mengi yanayoashiria hivyo. Wanasema hata shirika moja likijaa watoto wa wakubwa ni sawa tu ili mradi wana sifa. Lakini kuna siku watanzania watakuja kuelewa ukweli wa mambo.....mifuko hii inaendeshwa kisiasa sana. Badala ya kuwa mali ya wanachama (ambao ndio wanaochangia), imefanywa kuwa mali ya serikali na viongozi wa serikali ndio wenye maamuzi makubwa kuliko wanachama. Hizi pensheni zinaonekana kama hisani kwa wanachama na si stahili yao.