akatanyukuile
JF-Expert Member
- Sep 13, 2019
- 314
- 308
Ni matumaini yangu kuwa hamjambo wanajamvi. Ninaomba bila kupoteza muda nijikite kwenye mada tajwa.
Tangu nimepata akili na kujitambua, nimekuwa nikifuatilia masuala ya kitaifa na kimataifa.
Huwa sipitwi na taarifa ya habari yoyote kama nina muda ila sikuwahi kushuhudia Tanzania ikitajwa vibaya katika nyanja za kimataifa ila kwa miaka minne hii yaani kuna wakati ninawaza kulikoni, kiasi ninawaza labda yanayojiri mashariki ya kati kuna siku yatatukuta.
Hata leo nimeona UN imetoa ujumbe kuishutumu Tanzania kukosa demokrasia. Ukiangalia BBC walivoichambua habari hii inatia wasiwasi kwamba kama hakuna hatua za makusudi, itakuja kuleta shida mbeleni.
Nimewaza pia kwa sauti, je Tundu Lissu walimpuuza ila ndiye kakoleza hali hii au?
Ngoja niwaachie wajuzi wa mambo labda ninaweza pata amani ya moyo.
Karibu.
Tangu nimepata akili na kujitambua, nimekuwa nikifuatilia masuala ya kitaifa na kimataifa.
Huwa sipitwi na taarifa ya habari yoyote kama nina muda ila sikuwahi kushuhudia Tanzania ikitajwa vibaya katika nyanja za kimataifa ila kwa miaka minne hii yaani kuna wakati ninawaza kulikoni, kiasi ninawaza labda yanayojiri mashariki ya kati kuna siku yatatukuta.
Hata leo nimeona UN imetoa ujumbe kuishutumu Tanzania kukosa demokrasia. Ukiangalia BBC walivoichambua habari hii inatia wasiwasi kwamba kama hakuna hatua za makusudi, itakuja kuleta shida mbeleni.
Nimewaza pia kwa sauti, je Tundu Lissu walimpuuza ila ndiye kakoleza hali hii au?
Ngoja niwaachie wajuzi wa mambo labda ninaweza pata amani ya moyo.
Karibu.