Kuna nini Kati ya wanaharakati na January Makamba?

Kuna nini Kati ya wanaharakati na January Makamba?

Countrywide

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2015
Posts
21,484
Reaction score
34,223
Na declare interest, Mimi binafsi namkubali Sana January, Sana Sana.

Ila naanza kupata mashaka kuwa pengine Kuna namba, nguvu kubwa inatumika. Ni kiongozi mzuri, ila mbona Kama nguvu inakuwa nyingi sana.

Amekuwa waziri kwa muda mrefu, ana mazuri yake sawa.

Nimeshangazwa hata yule dada wa US nae anampigia chapuo na sio Mara ya kwanza, kwa nini anapigiwa Sana promo?

Hapa hakuna walakini? Yote kwa yote namkubali Sana na natamani siku moja aje kuwa namba 1, Ila hizi promo afanye namna aepukane nazo.
 
January ni mpigaji na anaongoza kishikaji, akiukwaa wengi watapewa mapande kama enzi za JK, wizi utarudi na uwajibikaji utaondoka kwa sababu itakuwa serikali ya washikaji.

Kingine nilichojifunza ameweka pesa nyingi sana kuutaka Urais 2025, hajajifunza kwa EL, yoyote ambaye anaonekana mroho wa madaraka ni wa kuogopwa kama ukoma.
 
Hakuna kiongozi mbovu kama January, yule mpenda ashua za kizungu hajui lolote kuhusu masuala ya uongozi na siasa zaidi ya kumezeshwa vitu DM. Na siku zote anajinasibu katika uswahiba wa baba yake na kiongozi mkubwa wa awamu ya nne.Hawa ni ndege warukao kwa pamoja. Sijui unanielewa?
 
January ni mpigaji na anaongoza kishikaji, akiukwaa wengi watapewa mapande kama enzi za JK, wizi utarudi na uwajibikaji utaondoka kwa sababu itakuwa serikali ya washikaji.

Kingine nilichojifunza ameweka pesa nyingi sana kuutaka Urais 2025, hajajifunza kwa EL, yoyote ambaye anaonekana mroho wa madaraka ni wa kuogopwa kama ukoma.
Napata mashaka Sana kuona zile promo
 
Makamba namwona kama ni Lowasa ajaye, kwa promo anazopigiwa sidhani kama Kuna kiongozi atataka kufanya naye kazi.

Maana anawapambe Sana mitandaoni lakini ukija kwenye uhalisia hakuna lolote zaidi ya ujanja wa kucheza na maneno.

Sema kuna uzi mwembamba Sana unaomtenganisha Mwanaharakati na Makamba.
 
Hakuna kiongozi mbovu kama January, yule mpenda ashua za kizungu hajui lolote kuhusu masuala ya uongozi na siasa zaidi ya kumezeshwa vitu DM. Na siku zote anajinasibu katika uswahiba wa baba yake na kiongozi mkubwa wa awamu ya nne.Hawa ni ndege warukao kwa pamoja. Sijui unanielewa?
Ongeza sauti haujaeleweka, hahahaha
 
January hapendi uadui kama mwendazake, hivyo nchi inahitaji watu wasiopenda visasi.
Najua haumjui january vizuri tafuta CV yake enzi za JK alikuwa mbabe na mwenye kiburi kama bashite enzi za jiwe
NB: yeye kipindi cha Jk alikuwa waziri au naibu waziri wa habari na mawasiliano kama sikosei ndo walipandisha vifurushi vya data wananchi tulilalamika wee tukala za uso, tukaenda kipindi cha uchaguzi 2015 hapo ndo niliona rangi yake uchaguzi ukafanyika mda wamatokea alikiwa kuwa anasema maneno mabaya moja ya kauli zake "CCM haiwezi kutolewa mdalakini kwa njia ya makalatasi " mwisho wakunuu baada ya mda mchache matokeo ya zanzibar yakafutwa chini ya Jecha matokeo yalikuwa yanaonesha seffu anaenda kushinda
Ni mmoja wa vijana wa Jk wapo kwa ajili ya familia zao na matumbo yao
 
Back
Top Bottom