Kuna nini kati ya Mwigulu na Zitto?

Kuna nini kati ya Mwigulu na Zitto?

masanjasb

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2011
Posts
2,364
Reaction score
869
wasalaam wanaJF?

Nimekuwa mfatiliaji sana wa siasa za hapa nyumbani kwa muda mrefu,ila sijawahi shuhudia mh Mwigulu akimkosea adabu mh. Zitto Kabwe kama anavyofanya kwa katibu mkuu dr. Slaa,hawa watu vyeo vyao viko sawa ndani ya vyama vyao,Zitto kabwe ni naibu katibu mkuu wa CHADEMA na Mwigulu nae ni naibu katibu mkuu wa CCM.

Katika mda tofauti watu hawa wamekuwa wakialikwa kwenye vipindi vya Tv kwa pamoja ila kuna muda mmoja nashindwe kutokea mara nyingi watangazaji husingizi foleni,kuwa mgeni wetu kashindwa kuja sababu ya foleni,mfano,kuna siku star tv waliwaalika naibu katibu mkuu wa CUF Mtatiro,naibu katibu mkuu wa CHADEMA Zitto na naibu katibu mkuu wa CCM Mwigulu ila Zitto Kabwe hakutokea na siku hiyo Mwigulu aliutangazia umma kuwa anao mkanda unaonyesha viongozi wa juu wa CHADEMA wa kupinga mauaji:

Nimekuwa nikiwaangalia hawa watu kwa jicho la 3 muda mrefu sana,Mwigulu kajikita sana kumshambulia Dr. Slaa,vile vile mh. Zitto Kabwe nae kajikita sana kwa waziri mkuu Pinda mpaka ilifikia hatua ya kukusanya sahihi za kutokuwa na imani na waziri mkuu,na sasa kaja na suala la mshahara wake,.

Nikirudi upande wa Mwigulu imefikia hatua mpaka kaajiri vijana ambao wanatumia Id zaidi ya 4 kwa mtu mmoja ili kumdhalilisha Slaa na mara chache Mbowe,kuna mambo mengi sana hayako sawa na ukiyafuatilia utagundua nachoongelea hapa,kwani kuna mambo mengi sana mabaya ambayo Mwigulu kaifanyia CHADEMA mpaka sasa lakini kamwe hutamsikia Zitto kayakemea pia upande wa Zitto kuna vitu vingi sana kaviibua kuhusiana viongozi wa CCM mfano fedha za Uswiz and so on ila hutamsikia Mwigulu kamsema Zitto kwa lolote kama alivyozoea kuwasema Slaa na Mbowe:

Swali la msingi: Watu hawa kuna makubaliano yoyote waliyoyafanya ili kutunziana heshima?

sina nia ya kuwachonganisha Zitto na Mwigulu bali wao ni public figures na matendo yao yanafuatiliwa kwa ukaribu mkubwa na watu mbali mbali nje na ndani ya nchi yetu.

Ombi: Tusijadili maisha yao binafsi bali kazi zao na harakati zao ndani ya vyama vyao.
 
niliisha hisi kitu kama hicho, hapo kuna tatizo, haitatokea mtu mwenye mapenzi ya kweli na hii nchi anaye chukia siasa za uzandiki na za kumwaga damu ambaye hawezi kuwa na chuki za ndani na mwigulu nchemba! mpaka kunabwana mmoja humu ndani aliandika mwigulu angependa kugombea urais lakini wasiwasi wake ni kuto kukubalika na vijana! sasa inakuwaje zitto mwenye mtazamo wa juu asione upuuuzi wa mwigulu. nakuunga mkono, pana tatizo hapo!
 
Anas al liby,mullar omar,mwigulu nchemba,samantha lewithwaite,suleman kova mbona harakati za hawa jamaa zinafanana.
 
chuki ya Mwigulu ni kujua wazi kuwa Dr Slaa alifanya vizuri sana kwenye uchaguzi wa 2010 kuliko ilivyotangazwa , kwa hiyo anajua 2015 kama atakuwepo na juhudi anayofanya ya kujenga na kuhimarisha chama CCM itakuwa haina chake , na kila jitihada anayofanya ya kumvuruga na kuvurugu CHADEMA zinafeli kwani Dr ni shushu mkubwa aliekuwa na dawati lake Ikulu Enzi ya Nyerere, zito ni kama simba asiye na meno na Mwigulu analijua hilo.
 
Siku zote zitto huwananga viongozi wa serikali na sio wa vyama! Anapomnanga mtu huwa analenga direct utendaji wake na athari yake moja kwa moja kwa wananchi! Ukinangana na mwigulu wote mnakuwa hamna malengo zaidi mtadhalilishana tu. Zitto yuko makini
 
zito na mwigulu wote ni wanasiasa wa hoja siyo porojo wewe unataka wakosoane hata kama hakuna sababu we vipi.
 
chuki ya Mwigulu ni kujua wazi kuwa Dr Slaa alifanya vizuri sana kwenye uchaguzi wa 2010 kuliko ilivyotangazwa , kwa hiyo anajua 2015 kama atakuwepo na juhudi anayofanya ya kujenga na kuhimarisha chama CCM itakuwa haina chake , na kila jitihada anayofanya ya kumvuruga na kuvurugu CHADEMA zinafeli kwani Dr ni shushu mkubwa aliekuwa na dawati lake Ikulu Enzi ya Nyerere, zito ni kama simba asiye na meno na Mwigulu analijua hilo.

uongo mwingine mtanyongwa slaa alikuwa wa tatu utasemaje alifanya vizuri.
 
niliisha hisi kitu kama hicho, hapo kuna tatizo, haitatokea mtu mwenye mapenzi ya kweli na hii nchi anaye chukia siasa za uzandiki na za kumwaga damu ambaye hawezi kuwa na chuki za ndani na mwigulu nchemba! mpaka kunabwana mmoja humu ndani aliandika mwigulu angependa kugombea urais lakini wasiwasi wake ni kuto kukubalika na vijana! sasa inakuwaje zitto mwenye mtazamo wa juu asione upuuuzi wa mwigulu. nakuunga mkono, pana tatizo hapo!

Huwezi kujifunza siasa nzuri bila kumwangalia zito z kabwe na pia vijana wa ccm nao siasa zao zina mkono mkubwa wa mh mwigulu, kufikia hatua yakuandika uzi kama huu nimefatilia mda sana siasa za hawa watu, na kwa nini zito awe kimya wakati chama kinaumizwa au viongozi wake wanashambuliwa?
Tatizo lipo and we need to fix it kabla ya 2015
 
Siku haipiti bila ya Chadema kumshambulia Kiongozi na Mbunge wao Zitto Kabwe kama hamumtaki si mumfukuze hiyo kazi ya kumfukuza ni yenu sio ya wana Jf na haiwezi kuwa delegated! Au mnadhani hiyo ni Kazi ya NEC ya CCM? Kama Zitto hawafai mtimueni mnayo mamlaka ya kisheria na kisiasa, Safari hii vaeni ujasiri kwenye Vikao vyenu maana mnapoulizwaga mwnye Madai dhidi ya Zitto kwenye Vikao Rasmi mnapiga Kimya akiomba kujibu madai ya kwenye Mitandao kwenye Vikao Rasmi Mbowe anatumia Mamlaka kumzuia sasa mnataka mambo ya Chama henu yajadiliwe kwenye Mitandao ya kijamii au wewe ni Mamluki wa kuvuruga Vyama kwa mgongo wa kujifanya Mfia chama?
 
Siku haipiti bila ya Chadema kumshambulia Kiongozi na Mbunge wao Zitto Kabwe kama hamumtaki si mumfukuze hiyo kazi ya kumfukuza ni yenu sio ya wana Jf na haiwezi kuwa delegated! Au mnadhani hiyo ni Kazi ya NEC ya CCM? Kama Zitto hawafai mtimueni mnayo mamlaka ya kisheria na kisiasa

Kiongozi lengo sio hilo,zitto ni mwanasiasa mwelevu na pia anajua anachokifanya,shida yangu ni kutaka kujua kwa nini siasa zao zimekuwa nzuri kati yake yeye na mwigulu? why ishindikane kwa slaa na mbowe? think big
 
Zitto ni mwanasiasa mstaarabu mwenye agenda ya ujenzi wa Taifa imara lenye amani, utulivu na umoja...
 
Katibu Mkuu wa magwanda Dr.W.Slaa aka babu, hampati Zitto kwa lolote, Zitto ni kijana, mwerevu, mchapa kazi, msomi, kwa juhudi zake pekee aliinyanyua chadema aka kadima na kuifikisha hapo ilipo.

Zitto hatujamuona wala kumsikia akifanya kazi za unaibu katibu mkuu wa chadema, sio saizi yake, huyo ni zaidi ya Katibu Mkuu na Mwenyekiti wa chadema kwa pamoja.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
 
mpaka sasa hakuna asiyefahamu kuwa mwigulu ni bata anayetaka kuatamia mayai ya kuku huku akitegemea kuangua watoto wa bata.na kuhusu zitto bado natafakari.
 
Umemaliza vizuri kuwa Mwigullu na ZITTO ni pubic figures, unachotaka kufanya ni kuwachonganisha tu, kaanze weekend.
 
Katibu Mkuu wa mgwanda Dr.W.Slaa aka babu, hampati Zitto kwa lolote, Zitto ni kijana, mwereu, mchapa kazi, msomi, kwa juhudi zake pekee aliinyanyua chadema aka kadima na kufikia hapo ilipo.

Zitto hatujamuona wala kumsikia akifanya kazi za unaibu katibu mkuu wa chadema, sio saizi yake, huyo ni zaidi ya Katibu Mkuu na Mwenyekiti wa chadema kwa pamoja.

soma uzi wangu mpk mwisho then rudi tena hapa,maana tunaongelea watu wawili,dr slaa kapita humu kama mfano but our topic ni mwigulu na zitto,tusaidiane kujijenga kifkra ili tutoke hapa tulipo
 
Back
Top Bottom