Kuna mambo ya ajabu sana CHADEMA

Leo wamekuja na Chadema Digitali ya ada ya sh. 2500/- kila mwanachama na wanakadiria kupata milioni 5,000,000/= kwa mwaka sasa kama walikuwa wanapata bilioni 3,600.000,000/= na ushee na ilikuwa analogi sembuse hii milioni 5 ya digitali ndiyo itajenga ofisi? na ikumbukwe kuwa kile kilikuwa kipindi cha Jakaya watu walikuwa na manoti mfukoni, poleni sana makamanda kwa imani kubwa mlioweka kwa Chadema ni sawa na huku kanisani kama waumini wangejuwa namna tunavyotumia michango yao ya sadaka wange acha kuleta sadaka. Kwani kunawaumini wengine wanaamini bado kuwa sisi wachungaji tunapeleka pesa kwa Mungu.
Sijaelewa unataka kusemaje, sadaka zimepungua? SGR mmeshindwa kujenga? au madege hayanunuliki tena kisa Chadema? Wacha wanaotaka kutoa watoe, na tunajenga ofisi nchi nzima kwa nguvu zetu
 
Leo hii mwenyekiti wa maisha wa chama kilichowai kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania ameanza kuzunguka nchi nzima eti kuimiza ujenzi wa ofisi za chama katika wilaya, makata na matawi, wakati ofisi ya makao makuu wanakaa katika kaofisi ka kupanga ka aibu pale Ufipa.
Mambo ya ajabu sana.

Kwa faida ya wasio fahamu, wakati chama kikiwa chama kikuu cha upinzani Tanzania, Chadema ilikuwa inapokea rukuzu ya milioni 300 na ushee hivi, hivyo kwa mwaka chama kilikuwa kinapata kama bilioni 3,600,000,000/-, Cha ajabu sasa chama kilikuwa akilipi hata katibu yeyote wa ngazi yeyote zaidi ya katibu mkuu. Kwa jimbo lililokuwa na mwakilishi yaani mbunge ndiyo kulikuwa na ofisi ambayo mbunge ndiyo alikuwa anaingia mkataba na mwenyenyumba, ofisi za matawi na kata ambazo hazikuwa na uwakiishi ni wanachama wenyewe walikuwa wanajichangisha na hawakuwai kupata msaada wowote kutoka katika fedha ya ruzuku. Viongozi wengi waliandika barua makao makuu hili kuomba fedha kwa ajiri ya pango wakisema tulianzisha sasa kodi imeisha tunaomba msaada, hawakupata. Tena kodi nyingi zilikuwa elfu 20,000 na 30,000 kwa mwezi lakini chama kilichomoa. Walipokuja makandamanda waandamizi walisema mwanachadema anatakiwa kukibeba chama moyoni mwake. Wakati huo tulikuwa tunaita jasho na damu la makamanda kuhakikisha chama kinasonga mbele bila aibu.

Pamoja na kuwa chama kilikuwa kinauziwa fifaa vya uenezi kama bendera na vifaa vingine unaweza jiuliza ruzuku ilikuwa inafanya kazi gani? ila sisi makamanda tulikuwa tunajua tunafanya jasho na damu.

Kwa msio fahamu mnaweza msielewe chama kilikuwaje katika jamii? chama kilipokelewa kwa mikono na mikuu yote, utashangaa kusikia wakati ule bei ya kadi ya mwanachama ilikuwa sh.1500/- tu, lakini wanachama wapya maitaji yalikuwa makubwa mno hadi kadi ilikuwa inauzwa sh. 3000/- hapa inamaana chama kilipendwa na kukubalika kwa 100%.(wakati wa Dr. Slaa)

Mikutano ya Operasheni Sangara na M4C ilishangaza wanachama wachache waliobaatika kujua kuwa chama kilikuwa kinakopeshwa pesa za mikutano hiyo. Yaani hapa inamaana chama na ruzuku ni watu wawili tofauti. Kama kinafanya mikutano kilipe pesa zote iliwemo magari, petrol, posho na vingine. Ilikuwa ajabu sana. Kama kuna kamanda anabisha aje kanisani nipo.

Leo wamekuja na Chadema Digitali ya ada ya sh. 2500/- kila mwanachama na wanakadiria kupata milioni 5,000,000/= kwa mwaka sasa kama walikuwa wanapata bilioni 3,600.000,000/= na ushee na ilikuwa analogi sembuse hii milioni 5 ya digitali ndiyo itajenga ofisi? na ikumbukwe kuwa kile kilikuwa kipindi cha Jakaya watu walikuwa na manoti mfukoni, poleni sana makamanda kwa imani kubwa mlioweka kwa Chadema ni sawa na huku kanisani kama waumini wangejuwa namna tunavyotumia michango yao ya sadaka wange acha kuleta sadaka. Kwani kunawaumini wengine wanaamini bado kuwa sisi wachungaji tunapeleka pesa kwa Mungu.

Mtoto wa mchungaji.
Hizo tarakimu zako zinatisha. Hivi unajua shilingi bilioni 3,600,000,000 ni Sawa na shilingi 3,600,000,000,000,000,000. Usikurupuke, rejea tena kwenye mpakato wako utuletee tarakimu sahihi.
 
ha ha ha - aisee ni kweli nimeanini kumbe kufiwa ni kubaya eee, jamaa wanaweweseka hatari - mara wamgeukie maza, mara wamgeukie Mbowe - ni kama madish yameyumba vile - signal hamna.
Kurukaruka kwa maharage ndio kuiva kwake
 
Achana na CHADEMA, CHADEMA iko bize kujenga ofisi mioyoni mwa watu, Mwendazake aliichukulia poa Chadema akidai ataiua alipoona imeshindikana akaishia kupindua meza na yeye kufikwa na hilo chambo lake,tusipangiane cha kufanya kwani labda nikuulize kwani ile project ya manunuzi ya madiwani na wabunge imeishia wapi??? la pili hivi kwanini Bashiru alitolewa pale Ikulu na kupekwa bungeni. Ukumbuke pia kuwa mbio za mwenge zina bajeti yake lakini kwa nini wafanyabiashara na wafanyakazi wanachangishwa kwa nguvu???usirushe mawe huku unajua nyumba yako ni ya vioo akili za mataga hovyo kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom