Kuna mahusiano yasiyo na unafiki?

Kuna mahusiano yasiyo na unafiki?

vyevye

Member
Joined
Mar 5, 2015
Posts
19
Reaction score
7
Habari members wote,

Naomba kuuliza kama kuna mahusiano ya dhati kizazi hiki. Namaanisha upendo wa kweli kwa pande zote. Mtu yupo tayari kumtetea.

Kumlinda na kusimama nafasi ya mpenzie kwa gharama yeyote. Iwe girlfriend/boyfriend, mchumba au mume/mke? Nimekuwa na mashaka kama yapo ni 1 kwa 100. Hii inasabahishwa na nini?

Naomba tujadili
 
Huwez Kuwa na mahusiano bila urafiki na UK Iona mahusiano yamepitia bila urafiki mmmmmh sijui,.......
 
Mkuu mimi naamini mahusiano kama hayo yapo. Ila vilevile ni imani yangu kuwa aina hii ya mahusiano kwa kiasi kikubwa inaendana na tamaduni za jamii husika na kiwango cha maendeleo..yote ya kiuchumi na kifikra.

Ukichukulia jamii zetu za kiafrika na kitanzania kwa uhalisia utaona kuwa tupo kwenye zama ambazo mwanamke anaamini ana kitu cha kuuza na mwanamme anaamini kuna kitu anatakiwa kununua kwa mwanamke..kwa mahusiano kama haya unafiki lazima utawale. Mwanamme anaona ana haki ya kununua hicho kitu mahali pengine iwapo akijisikia maadam pesa ni yake na mwanamke anaamini anayo haki ya kumuuzia mnunuzi zaidi ya mmoja maadamu mzigo ni wake.

kwa wenzetu kama ulaya hali hii kidogo ipo tofauti maana wenzetu wamepiga hatua zaidi katika kufikiria kwao kiasi mwanamke anaona akiingia katika mahusiano kwa ajili ya kupata kitu fulani basi thamani yake anakuwa ameishusha na kuwa sawa na bei ya kitu hicho anachokitarajia kupata.

nikirudi kwetu ni kuwa kuna wanawake wachache wanaoamini katika mahusiano ya kweli, yasiyo na unafiki..na kwa upande mwingine kuna wanaume ambao wanaamini katika hilo. Tatizo ni JE, HUYU MWANAMKE MWENYE KUAMINI KATIKA TRUE LOVE ATAFANIKIWA KUKUTANA NA MWANAMME ANAYEAMINI KATIKA TRUE LOVE? WATATAMBUANA NA KUANZA MAHUSIANO? Thats the million dollar question.
 
Mwanzo wa mahusiano ndiyo, unafiki hakuna. Kwa sababu mapenzi ni mapya na kila mmoja anakuwa na upendo wa kweli. Mkishazoeana unafiki unaongezeka na upendo kupungua.
 
unafiki eeee kabanga em ongea machache
 
Last edited by a moderator:
Hii inasabahishwa na nini?

Naweza kuwa nakosea lakini kwa mtazamo wangu msababishaji ni huu utandawazi!

Utandawazi umekuwa kiungo muhimu sana katika kuchochea na kuendeleza unafiki, udanganyifu, na uzinifu.
 
Ni wachache sana wengi wamebakia kwenye mahusiano yao kwa sababu ya pesa, dini n.k lakini sio kwamba wanapendana toka rohoni.
Unafiki unajionyesha pale wapenzi hasa wanandoa wanaposhindwa kupeana makavu hata kwenye visa vya kawaida kama mavazi, matumizi ya cm, kampan zao, matumizi ya pesa hata lugha ko unakuta mtu anasema anampenda mume/mke lakini hajawai kumfokea ata siku moja (mtu huonyesha who is he/she pale anapokasirika
 
Hii inasababishwa na watu kupungukiwa na madini mwilini aina ya gynesimpsonic
 
Watu siku hizi ni watafutaji juu ya migongo ya wenzao
 
Mapenzi ni unafiki tu kwa kwelii tutafika hivyo hivyo
 
Unachotakiwa kukiweka akilini mwako ni kwamba, dont trust someone that much maana ipo siku akikubadilikia hutaamini na roho yako. Hata kama mnalala kitanda kimoja muone tu ipo siku anaweza geuka ili akigeuka usishangae sana
 
Mkuu mimi naamini mahusiano kama hayo yapo. Ila vilevile ni imani yangu kuwa aina hii ya mahusiano kwa kiasi kikubwa inaendana na tamaduni za jamii husika na kiwango cha maendeleo..yote ya kiuchumi na kifikra.

Ukichukulia jamii zetu za kiafrika na kitanzania kwa uhalisia utaona kuwa tupo kwenye zama ambazo mwanamke anaamini ana kitu cha kuuza na mwanamme anaamini kuna kitu anatakiwa kununua kwa mwanamke..kwa mahusiano kama haya unafiki lazima utawale. Mwanamme anaona ana haki ya kununua hicho kitu mahali pengine iwapo akijisikia maadam pesa ni yake na mwanamke anaamini anayo haki ya kumuuzia mnunuzi zaidi ya mmoja maadamu mzigo ni wake.

kwa wenzetu kama ulaya hali hii kidogo ipo tofauti maana wenzetu wamepiga hatua zaidi katika kufikiria kwao kiasi mwanamke anaona akiingia katika mahusiano kwa ajili ya kupata kitu fulani basi thamani yake anakuwa ameishusha na kuwa sawa na bei ya kitu hicho anachokitarajia kupata.

nikirudi kwetu ni kuwa kuna wanawake wachache wanaoamini katika mahusiano ya kweli, yasiyo na unafiki..na kwa upande mwingine kuna wanaume ambao wanaamini katika hilo. Tatizo ni JE, HUYU MWANAMKE MWENYE KUAMINI KATIKA TRUE LOVE ATAFANIKIWA KUKUTANA NA MWANAMME ANAYEAMINI KATIKA TRUE LOVE? WATATAMBUANA NA KUANZA MAHUSIANO? Thats the million dollar question.

Tatizo liko kwenye hiyo paragraph ya mwisho hiyo,myself simwamini mwanamke yeyote.
 
Tatizo liko kwenye hiyo paragraph ya mwisho hiyo,myself simwamini mwanamke yeyote.

yeah, ni kweli. hata mimi simuamini mwanamke hata mmoja, ila najipa imani kuwa may be kuna siku atapatikana wa ukweli...na hapo nitaimba hossana milele
 
mapenzi kwa kweli yamejaa unafiki mtupu,usimuamin mtu maxima utakuja umia sana..fall in love with yourself my dear u won't b dissapointed,I guarantee!
 
Back
Top Bottom