Wana jf,
Ni ukweli usiopingika kwamba tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu, tumeshuhudia ukimya mkubwa katika kambi ya Ukawa kwenye kitengo cha uhamasishaji na matangazo.
Tofauti na wenzetu wa ccm ambao wameweka matangazo na amshaamsha kila pembe kama tv, radio, magazeti mitandaoni na kila sehemu ambapo wanahisi ujumbe utawafikia watu wengi kwa muda mfupi(haswa vijana).
Kinachonishangaza zaidi ni ukimya na kupooza huku ambako kumeingia hadi hapa ukumbini.
Sioni tena zile pilika tulizozizoea za akina Molemo na Tumaini Makene.
Swali langu kwenu viongozi wa ukawa, Mnafikiri bidhaa itanunulika vizuri bila matangazo?? Nb. Pamoja na uzuri wa bidhaa za Samsung, wanongoza pia kwa kuzitangaza. Chukueni hatua haraka!!
amen hakika unajua ila watanzania walipofikia hata bila ya matangazo mengi mambo yataenf sawa
Last edited by a moderator: