Kuna askari wazuri wachache katika hii dunia kama askari huyu hakuna mfano wake.

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,320
33,125
KUNA ASKARI WAZURI WACHACHE KATIKA HII DUNIA.jpg

Helena Raia wa Marekani

Kuna mtu alienda kumshitaki kituo cha polisi kua ameiba katika super market

Askari polisi alipo kwenda kumkamata alienda nae mpaka katika sehemu ya tukio baada ya kufika Polisi alimuuliza dada helena umeiba nini?

Helena"nime iba yai 1 mwanangu alikua na njaa sana"

Yule Askari akalipa hela na kumuongezea mayai mengine na vyakula.
Dada helena alimwambia Polisi kwanini unafanya hivi ?

Polisi alimjibu kua wakati mwengine utu ni bora zaidi kuliko kazi
Helena alitokwa na machozi sana

Mashaa Allah huruma ndio muhimu katika jamii
 
Kuna askar mmoja alikua hapo ubungo traffic tulimpa jina la chochote maana hajawah kuomba zaid ya buku hata uwe na makosa kumi,,,anakuambia nipe hata jero usepe,,lakin leo ni marehem aisee umenikumbusha yule jamaa aisee....
Haha Hahaaa

Huyu kwake Fedha ilikuwa bora zaidi kuliko Adhabu/Kuandikiwa.
 
Upendo huu ukaoneshwe kule Kibiti
Tofautisha kuna jambazi na mwizi ni vitu 2 tofauti. Mwizi ni binadamu mwenye njaa anaiba kwa sababu fulani anaiba kwa sababu ana njaa na jambazi anauwa na kunyang'anya kwa nguvu. Jambazi anatumia silaha na uibaji wa nguvu ukitaka usitake. Tofauti na mwizi anakuibia wewe haujuwi sasa kati ya jambazi na Mwizi,Jambazi ni binadamu mbaya sana kuliko Mwizi.
 
Zamani nikiwa mdogo nilikuwa napenda sana siku moja ni askari ila mzee wangu alikuwa anakataa sana nikimuuliza kwanini? Anasema mwanangu ukiwa askari huwezi kutenda haki utake usitake utadhulumu tu haki ya mtu iwe kwa lazima au bahati mbaya hivi sasa nayaona
 
Us ni pagumu sana mkuu.Ni wachache sana wenye huruma.
Ni bora hata uarabun
Uarabuni ninakokuja mimi au kwingine? Huko si ndo wanawasukumia maghorofani Dada zetu au nimekosea..... Si ndo huko wanakochinjana hadharani au.........
 
Tofautisha kuna jambazi na mwizi ni vitu 2 tofauti. Mwizi ni binadamu mwenye njaa anaiba kwa sababu fulani anaiba kwa sababu ana njaa na jambazi anauwa na kunyang'anya kwa nguvu. Jambazi anatumia silaha na uibaji wa nguvu ukitaka usitake. Tofauti na mwizi anakuibia wewe haujuwi sasa kati ya jambazi na Mwizi,Jambazi ni binadamu mbaya sana kuliko Mwizi.
Hata mimi sikumaanisha kuwapenda majambazi mkuu, nilimaanisha kuwapenda raia. Uhusiano kati ya polisi ni raia ukiwa wa kirafiki, jambazi atakosa pa kujificha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom