Kumwambia Babako kuwa Unampenda

Kumwambia Babako kuwa Unampenda

MwendaOmo

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2013
Posts
778
Reaction score
727
Kwa nini sisi waafrika huwa tunaona uoga kuwaambia wazazi wetu tunawapenda? KAtika video hii, wanaume wa Kenya waambiwa kuwapigia wazazi wao simu na kuwaambia eti wanawapenda. Hebu tazama.

 
Last edited by a moderator:
kuna kupenda kwa aina nyingi sana sasa hapa inategemea ni kupenda kupi!!!!
 
Hata Mimi na umri huu sijawahi kumwambia "Baba nakupenda" Kuna kipindi aliumwa tukasema ndio basi tena lakini sikuthubutu kusema Baba nakupenda....i just can't..!
 
Sio baba tu... Hata kwa maza kwangu imekaa kushoto hiyo.
 
mie namwambia sana tena sanaa kwani tangu wadogo tunapokwenda shule mpaka sasa tumeshazowea,na hata watoto wangu wananambia i love u mom,nikawaida lakini inategemea mlivyo lelewa nadhani kama mmezowea...... hata rafiki yangu akiniona nam Hug baba au mama anashangaa lakini mimi namshanga yeye hata wazee wake wawembali wakija anaamkia basi....
 
Hata Mimi na umri huu sijawahi kumwambia "Baba nakupenda" Kuna kipindi aliumwa tukasema ndio basi tena lakini sikuthubutu kusema Baba nakupenda....i just can't..!

hahahahahahahaaaa umenichekesha, lakini kweli unaanzaje kumwambia baba nakupenda?????
 
kuna kupenda kwa aina nyingi sana sasa hapa inategemea ni kupenda kupi!!!!

Kupenda ni kwa aina moja tu hakuna aina nyingi,kutokujua kwetu maana ya kupenda kunatupelekea kuuhusisha na mambo ambayo hata hauna mahusiano nao!
 
Hata Mimi na umri huu sijawahi kumwambia "Baba nakupenda" Kuna kipindi aliumwa tukasema ndio basi tena lakini sikuthubutu kusema Baba nakupenda....i just can't..!

Mkuu kwanini?
 
mie namwambia sana tena sanaa kwani tangu wadogo tunapokwenda shule mpaka sasa tumeshazowea,na hata watoto wangu wananambia i love u mom,nikawaida lakini inategemea mlivyo lelewa nadhani kama mmezowea...... hata rafiki yangu akiniona nam Hug baba au mama anashangaa lakini mimi namshanga yeye hata wazee wake wawembali wakija anaamkia basi....

no doupt umesoma st. mary mary, na ni ile type za dad & mum, not otherwise
 
Kwani kunaugumu gani kumwambia mzazi wako kuwa unampenda? Hiyo kwangu ni rahisi kuliko kwa mtu yeyote.
Upendo wa wazazi mbona unaeleweka?
 
Wazee wetu wa zamani sana, wanaosema wanaweza kumwambia I LOVE YOU MY FATHER ni wale watoto wa 20000 kuja na juu na wazazi ni wale walooa kuanzia 2000 kuja na juu, lakini dingi wa miaka 70 hakuelewi
 
no doupt umesoma st. mary mary, na ni ile type za dad & mum, not otherwise
wala sijasoma huko nimalezi nilolewa kwetu tuu. na wanavyo ishi wazazi wangu hata Dad akirudi kazini mom ana pokea mzigo with kiss ndio nilivyoona sasa ilikua shida pale nilipo olewa mume sie watu wa kiss mwanzo alikua akija nyumbani anasema mnapenda sana nyie kwenu mwaah! mwaah! lol
 
Kila napopata chance ya kumwambia jinsi navyompenda baba angu huwa namwambia. Na yeye akipata nafasi huwa ananiambia. Hakuna feeling nzuri nayoisikia kama baba angu akiniambia the way anavyonipenda na jinsi anavyowish nibehave. Yani huwa nazitunza texts zake na nazisoma mara kwa mara, nabaki tu namshukuru Mungu.
Hata kama mmoja wetu leo akitangulia mbele ya haki (God forbis), atakayebaki hatokuwa na regrets coz alimuonesha mwenzie jinsi gani anavyompenda. I can't thank God enough for the life of my father, he is the best thing that ever happened to me.
 
Sidhani kama akina dada wana shida hii sana. Ni lakini kwa wanaume kufanya hivi, ni kazi ngumu sana.
 
Nadhani kutokana na ukaribu na mahusiano waliyonayo wazazi na watoto, Mimi nilizoea tangu mtoto kumwambia mzazi wangu nampenda, wazazi hufurahi wasikiapo neno hilo toka kwa watoto wao nimeshuhudia hilo Mara nyingi.
 
Kiongozi hata sijui, labda malezi...wakati mwingine nahisi neno lipo kike sana...


Yaani basi tu mimi mwenyewe sipendi kumuambia awe yoyote bali nachoweza kufanya ni kumwambia uko makini basi.
 
Back
Top Bottom