Kumkopesha baba mwenye nyumba

Unakopesha milion 20 alafu unaishi nyumba ya kupanga??? Tena unakaa hapo hapo na mwenye nyumba??.
kupanga haimaanishi huna nyumba au huwezi kujenga unaweza kuwa umehamisha biashara /kazi sehemu mbali na kwako mfano umejenga morogoro shughuli zako dar itabidi upange tu
 
kupanga haimaanishi huna nyumba au huwezi kujenga unaweza kuwa umehamisha biashara /kazi sehemu mbali na kwako mfano umejenga morogoro shughuli zako dar itabidi upange tu
Inshu sio kupanga, siamin mwenye nyumba anaweza kupanga mahali ambapo mwenye nyumba atamuomba amkopeshe milion 20??? .

Anyway nmekuelewa mkuu
 
Unakopesha milion 20 alafu unaishi nyumba ya kupanga??? Tena unakaa hapo hapo na mwenye nyumba??.
MKUU MI MWENYEWE NIMESHANGAA
Unamkopesha Mil 20, Bado Umepanga!

Akili ni nywele.
Duniani bado kuna malofa ya akili. Eti 20 m yakumkopesha mtu unayo ilhali unakaa nyumba ya kupanga tena uswahilini maana huko ndiko wapangaji wanakokaa na wenye nyumba. Kama wewe huna laana ya wazazi wako basi utakua bwege wa kutupwa.
Ushauri wangu . Mkopeshe tu kesho na kesho kutwa atakubambikia ndoa ya mkeka na binti yake single mother
Mkuu mwenye nyumba kakuloga huyo. Haiwezekani una uwezo wa kukopesha m20 alafu bado unaishi kwake. Kuna walakini hapo
Na Wahindi wanaoishi National housing wamelogwa na nani? Hizi ni akili za kimaskini, kila mtu ana priorities zake.
 
Watu mnao hukumu.....mnajuaje kama yeye hana nyumba ila tu ameamua tu kupanga.....!!!?

Mtu anaomba ushauri wa jambo lingine anashauriwa jambo lingine
Una nyumba Bunju, mishe zako City center, ukipangisha nyumba yako na wewe kupanga sehemu ambayo ni easy accessible kwenda city center tatizo liko wapi?

Zamani nilikuwa na akili za kijima kama wao nikajenga mjengo sehemu kufika town natumia hadi masaa matatu kwa mkweche wangu, gharama za matumizi ya mafuta au daladala plus bodaboda ziko juu nikaona huu ni upuuzi na nikagunduwa ni kwa nini watu wanaojuwa uchumi vizuri kama Wahindi wanakaa town.

Namshukuru Mungu hesabu zangu zimekubali nina mjengo kilometers 10 tu kwenda City center, sina tena stress za namna ya kufika town na wala sidamki alfajili kama mchawi kisa kuwahi mjini, nimeushinda utumwa huu.
 
Yaan unauwezo wa kumuazima mtu 20m afu upo nyumba ya kupanga... Daah we unahitaj maombi kabsaa
 
Je mlishawahi kufanya hiki kitu? Nataka nimkopeshe baba mwenye nyumba pesa milioni 20, ambapo kila mwezi atarejesha 1000,000 kama riba kwa miezi mitatu.je imeekaaje wenzangu.hofu yangu naona kweny kudai hizo pesa baada ya muda kuisha,je kuna mtu anauzoefu na hii kitu?
Andikishaneni kwa mwanasheria ili akizingua kieleweke
 
Je mlishawahi kufanya hiki kitu? Nataka nimkopeshe baba mwenye nyumba pesa milioni 20, ambapo kila mwezi atarejesha 1000,000 kama riba kwa miezi mitatu.je imeekaaje wenzangu.hofu yangu naona kweny kudai hizo pesa baada ya muda kuisha,je kuna mtu anauzoefu na hii kitu?
Hii kitu kisheria hasa hapa kwetu Tz iko hivi..

Hiyo riba unayomtoza ni illegal...wewe binafsi huna vigezo au vibali toka mamlaka husika vya kukuwezesha kumkopesha huyo landlord kwa riba.

Kumbuka kukopesha kwa riba ni mojawapo ya banking activities ambayo inahitaji compliance toka mamlaka zinazoratibu mambo hayo.

Ukimkopesha hiyo TZS 20,000,000 na riba juu hutoweza kudai riba uliyom-charge anywhere kama landlord ata default kulipa. Sana sana utarejeshewa kiasi kile kile...milioni 20 za kitanzania.

Hivyo kama unaamua kumkopesha hiyo ndiyo hali halisi.
 
Yaan unauwezo wa kumuazima mtu 20m afu upo nyumba ya kupanga... Daah we unahitaj maombi kabsaa
Sasa wewe ukiwaona wanaolipa hiyo millioni 20 kama kodi ya miezi 6 kwenye apartment sijui utapatwa na kichaa kabisa?

For ur information hiyo million ni mshahara wa mtu kwa mwezi, endeleeni kukalili tu kwa kudhani binadamu wote ni sawa.
 
Wakati wengine wanakuponda mi naiona fursa hapo,
Mkopeshe na muandikiane kabisa,
Akija tena mpe tu kama unazo ila muandikishane umwambie kabisa familia yako inafahamu kua umempatia hela.

Kuja kushtuka hiyo nyumba unayokaa ishakua yako umeinunua kwa installments. Akijua kua familia yako inafahamu hatoweza/hatowaza kukudhuru ili kuua deni, maana hata watakaobakia wataliendeleza tu
 
Wakati wengine wanakuponda mi naiona fursa hapo,
Mkopeshe na muandikiane kabisa,
Akija tena mpe tu kama unazo ila muandikishane umwambie kabisa familia yako inafahamu kua umempatia hela.

Kuja kushtuka hiyo nyumba unayokaa ishakua yako umeinunua kwa installments. Akijua kua familia yako inafahamu hatoweza/hatowaza kukudhuru ili kuua deni, maana hata watakaobakia wataliendeleza tu
Kaka umesema kweli nakubaliana nawe
 
Je mlishawahi kufanya hiki kitu? Nataka nimkopeshe baba mwenye nyumba pesa milioni 20, ambapo kila mwezi atarejesha 1000,000 kama riba kwa miezi mitatu.je imeekaaje wenzangu.hofu yangu naona kweny kudai hizo pesa baada ya muda kuisha,je kuna mtu anauzoefu na hii kitu?
Mkuu vipi mlilipana au?
 
Back
Top Bottom