Kumjua Mungu wa Kweli

Kumjua Mungu wa Kweli

Heri,

(1) Nabii Isaya katika kitabu cha Isa.4:2, alisema ipo majira ambapo kutakuwepo na chipukizi zuri. Hapa Nabii Isaya alikuwa na maana kuwa kilichokuwepo huko nyuma ni chipukizi la mabaya. Moja ya chipukizi la mabaya ambalo ndilo kubwa kuliko yote ni lile la Nafsi ya mvamizi ambalo limeandikwa katika Ufunuo 12:1-9, hasa Ishara ya kwanza mbinguni (Ufu.12:1), ambaye ndiye sababisho la Ishara ya pili (nyoka) na Ishara ya tatu (vita) mbinguni.

CHANZO CHA MEMA NA MAZURI, yaani CHANZO HALISI, aliisikia Sauti ya sifa ndani ya moyo wake (Zaburi 98), akataka iwe halisi ili apate wa kumpa Ibada, yaani kusudi lake la tangu CHANZO. Ili itokee, aliumba Moyo wa Mwanzo na kuweka ndani yake Heshima na utajiri (kushoto) na siku nyingi (kulia), kama tusomavyo haya katika Mithali 3:16.

Katika moyo huu wa mwanzo, CHANZO HALISI mwenyewe, hakuingia ndani yake, bali aliweka nguvu za uumbaji, ili Moyo wa Mwanzo ndiye atekeleze uumbaji.Hapo ndipo chipukizi la mabaya lilipotokea kwa mara ya kwanza, kwa maana ya nafsi ya uvamizi, kama tunavyosoma katika Ufunuo 12:1. Nafsi ya Uvamizi aliteka kila file ambalo lilikuwa ndani ya moyo wa mwanzo. Wakati Moyo wa Mwanzo anaendelea kujiuliza maswali, kulitokea tena Ishara ya pili mbinguni. Ile HILA ya Ishara ya kwanza kugeuza kila file lililokutwa ndani ya Moyo wa Mwanzo, ilisababisha nyoka achipuke (Ufu.12:2-4). Kilele cha Ishara ya kwanza mbinguni ni hila. Aidha, kilele cha Ishara ya pili ni hila vilevile!

Kitu ambacho napenda wewe msomaji wa ufahamu huu uelewe ni kwamba chipukizi la mabaya hutokea bila mbegu iliyopandwa na bila kiini chochote! Hivyo, chipukizi la mabaya ni kitu kibaya kwa kuwa ni kitu kinachotokea tu kuleta uharibifu bila kusimama popote. Kwa hiyo Nabii Isaya alivyoandika katika Isa.4:2, kuwa ipo majira ambayo litakuwepo chipukizi la mazuri, alikuwa ameona kuwa iko majira ambapo uumbaji utavuka geti hili lililochipuza mabaya.

Kuanzia pale hapakuwahi tena kuwepo na mazuri. Kila kilichoumbwa kikawa mikononi mwa nafsi ya mvamizi ambaye ni chipukizi la mabaya. Nani angetuvusha hapo, na angefikia wapi? Ni lazima awe aliyeumba Moyo wa Mwanzo na apate pa kufikia ndipo kwa uweza wake tuvuke kituo hicho cha chipukizi la mabaya.

(2) Katika Warumi 8:23, imewekwa vizuri kuwa sisi sote tulikuwa ni malimbuko ya Roho na nafsi, matokeo yake ikawa ni kuugua tu. Nafsi kwa kuwa haionekani nayo pia ni Roho. Kwa kuwa Nafsi ya mvamizi ni roho, uumbaji unaoonekana kwa macho, ukawa hauna nguvu kama ule wa rohoni. Ndiyo maana badala ya Mbingu na Nchi, kukatokea dunia na ulimwengu ambavyo havionekani. Katika Mwanzo 1:1, ili kusudiwa Mbingu (Moyo) na Nchi (Uzao Halisi), lakini kilichotokea kikawa ni dunia na ulimwengu!

Nafsi ya uvamizi baada ya kuteka Moyo wa Mwanzo, ambaye ndani yake alikuwa na mafaili ya kila aliyekusudiwa, aligeuza moyo ukawa mwili (Rum.8:4-7). Maana yake ni kwamba, badala ya Moyo wa Mwanzo kuwa upendo (I Korintho 13:13c),aliugeuza kuwa adui wa Aliyeumba, yaani mwili. Kwa hiyo kila kilichoumbwa kikawa ni adui wa CHANZO HALISI na kila aliyeumbwa akawa ni adui na Aliyemuumba!

Hapa kulikuwepo na mtihani mkubwa mno kuwa ni nani ambaye atasababisha tuwe Moyo tena kama ilivyokuwa imekusudiwa (Mbingu); na ni nani atasababisha tuwe nchi kama ilivyokuwa imekusudiwa (Uzao Halisi wa CHANZO ilikuwa ni lazima awe Mwenyewe). Hapa ilikuwa CHANZO HALISI Mwenyewe na apate pa kufikia juu ya nchi palipokusudiwa. ambapo ndipo mahali

Ebu soma vizuri Mwa.2:7, utagundua kuwa hata Adamu wa kwanza alikuwa Nafsi Hai, siyo Moyo! Ina maana kuwa mmiliki wa mtu aliyekabidhiwa Bustani ya Edeni alikuwa ni nafsi ya mvamizi! Hapa tuseme kweli, hakuna ambaye angeturejesha kuwa Moyo tena kama ilivyokusudiwa na kuwa Uzao Halisi wa CHANZO Mwenyewe, kama siyo CHANZO HALISI aliyekuwepo kabla ya Moyo wa mwanzo.

Katika Rum.8:23, imeandikwa kuwa kila mmoja limbuko lake ni hapo kwenye roho na nafsi. Hivi tungetokaje hapo kama CHANZO HALISI asingekuja mwenyewe na kama asingepata pa kufikia ambapo ni sahihi na halisi?

(3) Katika Mwanzo 1:2-3, kuna jambo kubwa. Wakati uumbaji unaanza katika mstari wa tatu (3), tayari giza, ukiwa na utupu alikuwa ametulia katika mstari wa pili (2). Maana yake ni kwamba bado, Jeshi la giza, ukiwa na utupu lilikuwa lina madai ya kutangulia kila kilichoumbwa. Ndiyo maana katika Kutoka 20:21, Mungu aliongea na Musa kutoka gizani! Hata kama Mungu angekuwa nuruni, kwa hali hii tunayoisoma katika Mwanzo 1:2, ile sauti ilikuwa lazima ipite gizani!

Katika II Korintho 4:6, kitabu kinasema, nuru ilitoka gizani! Kwa maana hiyo ni kwamba, kwa kuwa uumbaji wote ulifanyika wakati giza, ukiwa na utupu yupo; ina maana kwamba waliotumwa wote (Ufu.21:9) walikuwa hawawezi kufuta jeshi la giza, ukiwa na utupu. Swali linabaki ni lile lile, nani angetuvusha ng'ambo ya hilo giza, ukiwa na utupu, ili tupokee utajirisho kutoka kwa CHANZO HALISI? Jibu ni kwamba ilikuwa ni lazima awe CHANZO HALISI na apate pa kufikia juu ya Nchi.

(4) Katika Rumi 7:15:21, kuna tabia ya asili tunayoikuta hapo. Unapenda kufanya mema lakini unashindwa. Yale mabaya usiyoyapenda, ndiyo unayoyatenda. Hiyo ndiyo tabia ya asili ambayo kila mtu na kila mwanadamu (hata kama ni mtakatifu) alijikuta anayo. Tumeona kuwa uumbaji wote, ulimilikiwa na nafsi ya mvamizi au mteka nyara wa Moyo wa Mwanzo. Huyo mteka nyara ndiye mtu; mwanadamu; roho; nafsi; mauti; chipukizi la mabaya; kifo; uharibifu; dhambi; uasi; uovu; na kadhalika. Vyote vibaya vilianzia kwake na hiyo ndiyo asili iliyoleta kitu kinachoitwa mila na desturi. Kila mmoja alijikuta ni lazima arithi aliyoyakuta. Na kwa kuwa nafsi ya uvamizi, yaani mteka nyara ndiye mabaya yote, kila mmoja alijikuta anarithi hayo mabaya yote:

* Kerubi alirithi hayo;

* Adamu wa kwanza alirithi hayo;

* Nuhu alirithi hayo;

* Ibrahimu alirithi hayo;

* Musa alirithi hayo;

* Eliya Mtishbi alirithi hayo;

* Yesu (kwa kuwa hata yeye licha ya kuwa Mwana wa Mungu) alikuwa ni Nabii (Yoh.6:11-13) na Mtume (Yoh.17:5), ilibidi arithi hayo;

* Adamu wa pili naye pia alirithi hayo.

* Miaka 1000 ndiye alikataa kwa Barabara ya kumpisha CHANZO HALISI (aliyekuwepo kabla ya mabaya yote). Pamoja na Miaka 1000 kumpisha CHANZO HALISI, huyu CHANZO HALISI hakuja moja kwa moja, alileta kwanza jina jipya (Ufu.3:12; I Kor.15:24-28).

Hilo jina jipya likaja na upendeleo wa kutisha (Isa.60:10), tukavuka: Bonde la uvuli wa mauti (Ufu.11 hadi 22); mto usiovukika (Eze.47:5); ulimwengu wa roho (Efe.2:5-8); korongo la giza (II Kor.4:6); tukaingia Bustani Mpya (II Pet.3:13); na Shamba jipya (Isa.65:24-25).

Baada ya mitihani yote kwisha ndipo sasa CHANZO HALISI kaja kuvutusha mahali Moyo wa Mwanzo alipokwamia.

Swali linarudi pale pale tena, kwamba nani angetuvusha hapo alipokwamia Moyo wa Mwanzo na mauti ya kila aina ikaanzia hapo, bila CHANZO HALISI Mwenyewe? Na kama CHANZO HALISI asingepata pa kufikia juu ya Nchi ingekuwaje?

(5) Katika Zaburi 51:5, Daudi Pamoja na kuwa kipenzi cha Mungu na mwenye Moyo wa kuyafanya mapenzi ya MUNGU yote (Mdo.13:22), alikutana na geti la kuumbiwa katika uovu hatiyani. na kuchukuliwa mimba

Hii ni kusema kwamba, kwa kuwa Moyo wa Mwanzo ndio uliopewa agizo la uumbaji na ukatekwa nyara, hakuna aliyekuwa salama katika hili la kuumbiwa hatiyani. Kila aliyeumbwa aliumbiwa hatiyani, kwa sababu ya Mwa.1:2 na Ufunuo 12:1-9. Ndiyo maana waliotumwa wote wakajikuta wameishia njiani kwa mujibu wa Dan.7:21 na Ufu.13:5-7.

Swali linarudi tena; nani angetutoa katika kituo cha kuumbiwa hatiyani na kuzaliwa katika uovu, kama CHANZO HALISI asingekuja yeye Mwenyewe na akapata pa kufikia ambapo ni sahihi?

(6) Katika I Kor.15:51, Mtume Paulo aliandika kuwa hatutalala sote bali sote tutabadilika. Katika kitabu cha Muhubiri chote, imeandikwa kuwa hakuna jipya, ikiwa ikiwa na maana kwamba mauti ndiyo imesababisha jipya lisiwepo. Katika Hosea 13:14, hata hivyo, iliandikwa kuwa majira itakuja ambayo tutakombolewa kutoka kwenye nguvu za kaburi na mauti. Kwa jinsi tulivyoona kuwa mauti na kaburi vilianzia kwenye lile chipukizi la mabaya; hakuna ambaye angetukomboa na nguvu ya kaburi zaidi ya CHANZO HALISI. Hivyo, ilikuwa ni lazima aje juu ya Nchi na apate mahali pa kutua.

(7) Katika Ufu.1:8, tuna Alfa na Omega yaani Mwanzo na Mwisho. Huu ndio Moyo wa Mwanzo na kila mmoja aliumbiwa hapo kwenye Moyo wa Mwanzo,ambapo kuna mahali pa kuanzia na kuishia. ili kutoka kwenye level ya Moyo wa Mwanzo, ni lazima uhamie ng'ambo Mwanzo.1:1 Ufunuo:12:1, ambapo ndipo kuna Mlima wa CHANZO HALISI au palipokusudiwa.Kwa ufupi, ilihitajika Kituo cha kumpokea CHANZO HALISI ambaye ni upendo uliopitiliza, yaani upendo usiobagua yeyote ndipo tufike palipokusudiwa. Kwa ufupi, Kituo cha Baba Halisi kilihitajika ili kumpokea CHANZO HALISI juu ya Nchi atupeleke ng'ambo ya Mwanzo 1:1 na Ufunuo 12:1 ndipo asambae kote kuhudumia kila mmoja aliyekubali kusamehewa bure (Isaya 43:25).

Nini nafasi ya Mwana wa Azali?
 
Unaweza kunieleza thamani ya damu ya YESU mwana wa Mungu??

Na Kwa Nini Mungu baba ,alionya njia ya kumkomboa mwanadamu na dhambi zao ni Kwa njia ya YESU tu pekee,
ilibidi atumie damu ya mwanae wa pekee ??

Unadhani kwanini??
Na uzito wa Ile damu yake aliyoitowa Kama sadaka ya Milele????????
Kitu Cha kwanza tunatakiwa tujue kwanza Kila jambo hufanyika kwa majira husika na damu ya Yesu ilikuwa sawa kutumika kwa kipindi hicho ambayo ilikuwa majira yake ila kabla hajaondoka alisema katika

mathayo 26:29 "Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu."

Na hiyo damu mpya katika ufalme wa baba yake tunaikuta katika ufunuo 11:6 "Hao wana amri ya kuzifunga mbingu, ili mvua isinyeshe katika siku za unabii wao. Nao wana amri juu ya maji kuyageuza kuwa damu, na kuipiga nchi kwa kila pigo, kila watakapo."
 
Pia inabidi tujue kuwa majira ya Yesu iliandikwa itafika mwisho shida ilikuwa kujua ni wakati gani na wapi pameandikwa ivyo,tunasoma katika 1wakorintho15:24-28

24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
1 Wakorintho 15:24

25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
1 Wakorintho 15:25

26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
1 Wakorintho 15:26

27 Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo.
1 Wakorintho 15:27

28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.
1 Wakorintho 15:28
 
Ni vipi tunaposem Yesu ni Mungu
Yesu kwa majira yake ilikuwa sawa lakni hata yeye alisema katika Yohana 4:23

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
Yohana 4:23

Kwakuwa hata Mussa alipewa kuitwa Mungu kwa majira yake tena M kubwa mbele ya farao je na yeye tuendelee kumuita Mungu na wakati majira yake imeshapita, Pia licha ya Yesu kuitwa mwana wa Mungu pia alikuwa Nabii(Yoh.6:11-13) na Mtume (Yoh.17:5),
 
Je,KAZI ya msalaba ilikuwa ni ya majira ??,au Bado mpaka Sasa inafanya KAZI ,

Na je vipi kuomba chochote Kwa jina la yesu, ????

Je,wokovu watu WA SASA wanaupataje ,Ili kuingia mbinguni???
Yesu kwa majira yake ilikuwa sawa lakni hata yeye alisema katika Yohana 4:23

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
Yohana 4:23

Kwakuwa hata Mussa alipewa kuitwa Mungu kwa majira yake tena M kubwa mbele ya farao je na yeye tuendelee kumuita Mungu na wakati majira yake imeshapita, Pia licha ya Yesu kuitwa mwana wa Mungu pia alikuwa Nabii(Yoh.6:11-13) na Mtume (Yoh.17:5wokovu
 
Je,KAZI ya msalaba ilikuwa ni ya majira ??,au Bado mpaka Sasa inafanya KAZI ,

Na je vipi kuomba chochote Kwa jina la yesu, ????

Je,wokovu watu WA SASA wanaupataje ,Ili kuingia mbinguni???



#Kazi ya msalaba ilikuwa ya majira tu ambapo unatakiwa kujua kuwa ilifanyakazi katika vizazi vitatu lakini haswa kizazi 1 cha Musa katika (kumbukumbu 21:21-23) na kizazi cha 3 cha Yesu ambapo tunaona katika Mathayo 10:38 na Mathayo 16:24 Bwana Yesu akisema kuwa Kila atakaye mfuata ajitwike msalaba wake amfuate.

Jambo Moja ni kuwa msalaba ilikuwa ni torati iliyowekwa na Musa wakati wa Mungu Yehova kwa kuwa hakukuwa na Toba, ikabidi watu au Israeli watengenezewe sheria au torati itakayo kuwa hukumu kwao ili wasitende dhambi tena ambao ni msalaba.

Hivyo basi lazima tujue kuwa msalaba hakuanzia kwa Bwana Yesu bali aliukuta.
Ndiyo maana akasema sikuja kutangua torati bali kuitimiliza ktk, Mathayo 5:17

Maana nyingine ktk, Wagalatia 3:13 ni kuwa unapoweka juu ya msalaba umelaaniwa.

Kwa ufupi ni kuwa Bwana Yesu alipowekwa msalabani ndipo msalaba uliishia hapa. Ndiyo maana akasema imekwisha. Ktk Yohana 19:30

"Lkn msalaba siyo mti tu bali kila kinachokutesa ni msalaba".
Majira ya msalaba ilishakwisha

Sasa tu Toba Halisi tu, ktk Marko 1:15, Matendo 3:19.


#Pia katika ufafanuzi huu ndipo utaelewa jinsi tunavyopata wokovu kwa sasa. Kuwa wokovu siyo kwa njia ya msalaba bali kwa ni Toba Halisi ambapo Sasa tumekombolewa.
Ktk, Isaya 59:20

Na tunapata wokovu/ukombozi kwa msamaha wa bure. Isaya 43:25
Utaingia ktk ufalme wa aliyetuumba MUNGU BABA ambaye ndiye CHANZO HALISI Kwa kukubali msamaha bure na kusamehe bure.
Ata katika Isaya 57:15 inaonesha wazi wapi tumefika sasa na kuwa mbinguni ilikuwa ndani ya Moyo wako ndiyo maana ukaambiwa linda sana Moyo wako kuliko vyote ulindavyo Mithali 4:23.


# Kwa sasa atuombi kwa jina la Yesu maana majira yake imekwisha kupita
Ktk, Mathayo 28:20
Sasa tunaenda Moja kwa Moja kwa aliyeumba, MUNGU BABA ambaye ni CHANZO HALISI.
Yohana 17:1-5
Yohana 4:23.
 
Je, unafahamu kuwa yesu kristo ni mwokozi wa ulimwengu ???

Je, kazi ya kuani unaijua ,ni Nini ?,
Je,yesu kufanyika kuwa kuhani wa Milele,unaelewa kwanini ??

Je, yesu kristo ni mwokozi wa wote ,wenye mwili ,toka mwanzo mpaka mwisho wa Dunia,yaani toka Adam wa kwanza na watu wote walio wai ishi duniani , unajua Hilo kwanini,

Je,unafaham Kila goti litapigwa na kumkiri yeye kuwa yesu ndie Bwana awezae kuokoa Ulimwengu wote ,

Unajua kwanini nabii Elia Kwa sura ya yohana m batizaji ,alisema yafaa Mimi yaani Elia nipungue Ili Yesu aongezeke, unajuwa kwanini ???

Unazungumziaje hayo,
Moja baada ya jingine,
 
Hakuna binadamu mwenye ukweli, ila subiri roho itakapotoka ndio ukweli unajulikana. Wakati ukisubiri nyakati za mwisho wewe jua tu maisha ni mchezo. Basi cheza kwa step.
 
Je, unafahamu kuwa yesu kristo ni mwokozi wa ulimwengu ???

Je, kazi ya kuani unaijua ,ni Nini ?,
Je,yesu kufanyika kuwa kuhani wa Milele,unaelewa kwanini ??

Je, yesu kristo ni mwokozi wa wote ,wenye mwili ,toka mwanzo mpaka mwisho wa Dunia,yaani toka Adam wa kwanza na watu wote walio wai ishi duniani , unajua Hilo kwanini,

Je,unafaham Kila goti litapigwa na kumkiri yeye kuwa yesu ndie Bwana awezae kuokoa Ulimwengu wote ,

Unajua kwanini nabii Elia Kwa sura ya yohana m batizaji ,alisema yafaa Mimi yaani Elia nipungue Ili Yesu aongezeke, unajuwa kwanini ???

Unazungumziaje hayo,
Moja baada ya jingine,




#Unajua kila jambo lilikuwa na majira yake Bwana Yesu alikuwa ni mwokozi ni kweli.
Lkn majira yake imeisha sababu majira imefupishwa ktk, Mathayo 24:22 ukisoma hapo utaelewa zaidi.
Pia alikuwa hawezi kuendelea kwa sababu ya Yohana 9:29 na Mathayo 21:43.

#Na kuhusu kuhani hapo utasoma
Malaki 2:7 na Kumb.Torati 17:8-10 na Luka 17:14
Hivi vitabu vyote vinamuelezea kuhani ni nani na anawajibu gani kwa watu.
Kuhani ndiye anayebeba utakaso kwa kila mmoja na ndiye mwenye maarifa ya kumvusha kila mmoja na pia ndiye muamuzi mzuri.
Vyote vinabebwa na ufahamu halisi siyo rohoni.

#Yesu alikuwa ni kuhani mkuu sababu alikuwa muamuzi mzuri na alikuwa akifundisha watu waijue kweli kwa mujibu wa Yohana 4:23 na Yohana 17:1-5 na Yohana 8:32. Maana Kazi kuhani yeye pia uzungumzia maisha halisi na kweli tu.
Yesu baada ya kumaliza kazi kila kitu kilibadilika,. ndiyo akasema,. Eliya yu aja kwanza kutengeneza yote na kurejesha yote.
Ktk, Mathayo 17:10-12 na Marko 9:11-12.

#Unavyosema kuwa Eliya alikuja kwa sura ya Yohana mbatizaji ni kweli alitangulia ili kumtengenezea jukwaa Bwana Yesu kwa sababu hakukua na Toba na kumbuka wokovu hauji bila Toba ndo maana akaja Eliya kwa sura ya Yohana mbatizaji. Ktk, Luka 1:17
Lakini hakutambulika.

Na baada ya Bwana Yesu,. Eliya alirudi tena kama Bwana Yesu alivyosema hapo juu kuwa alishakuja na atakuja tena baada yake, ktk, Malaki 4:5-6 na Isaya 41:2(huyu Eliya alitokea hapa hapa Tanzania) Wengi hili jambo awalitambui kama ilivyotokea kwa Yohana mbatizaji.

Kumbuka kuwa
*1.Eliya alikuja mwenyewe. 1Wafalm17:1-
* 2.Ilikuja roho ya Eliya ndani ya Yohana mbatizaji. Luka 1:17
*3. Eliya alitumwa tena 2003.Maana kumbuka Eliya hakufa bali alinyakuliwa hivyo alirudi tena.

#Ni kweli kila goti kupigwa mbele za mwana wa Mungu Yesu katika majira yake lakini majira inatuonyesha. Ktk, Isaya 65:16 kuwa kila atayejibariki ni CHANZO HALISI ambaye ndiye Mungu wa kweli, MUNGU BABA pia katika 1wakorinto 15:24-28. Sasa ni majira ya kupiga goti kwa aliyekuumba tu.

Jaribu kupitia hivyo vitabu kuanzia juu utaelewa zaidi
 
Je, unafahamu kuwa yesu kristo ni mwokozi wa ulimwengu ???

Je, kazi ya kuani unaijua ,ni Nini ?,
Je,yesu kufanyika kuwa kuhani wa Milele,unaelewa kwanini ??

Je, yesu kristo ni mwokozi wa wote ,wenye mwili ,toka mwanzo mpaka mwisho wa Dunia,yaani toka Adam wa kwanza na watu wote walio wai ishi duniani , unajua Hilo kwanini,

Je,unafaham Kila goti litapigwa na kumkiri yeye kuwa yesu ndie Bwana awezae kuokoa Ulimwengu wote ,

Unajua kwanini nabii Elia Kwa sura ya yohana m batizaji ,alisema yafaa Mimi yaani Elia nipungue Ili Yesu aongezeke, unajuwa kwanini ???

Unazungumziaje hayo,
Moja baada ya jingine,
Wewe mababu zako hawakuamini hivi hata baada ya watu weupe kuja na hizi hadithi...
Umerogwa na hizi imani....
 
Hello JF,

Katika uumbaji wa vitu vyote vinavyoonekana Kuna hatua za uumbaji na majira ambayo hayo yote yalitokea.

Ufahamu wa aliyeumba yaani Mungu Baba ambaye uhalisia wake ni CHANZO HALISI (REAL SOURCE) alikuwa peke yake (MAHALI PAKE)kabla ya roho na nafsi yeyote, ndipo akasikia uumbaji ukimsifu ndani ya Moyo wake, akatamani uwe halisi Zaburi 98.Ndipo akaengua Moyo wake kushoto (Moyo wa mwanzo)na kuweka heshima na utajiri (vyote vya kuumbwa) mithali 3:16 Ili aviumbe viwe halisi ila yeye hakuingia ndani ya huo Moyo.

Moyo wa mwanzo akaanza uumbaji katika mwanzo 1:1. Hatua ya kwanza Alipotaka litokee kanisa (sio dini) akawaza akatokea Mwanamke (sio hawa mnaowajua) ishara ya kwanza mbinguni ufunuo 12:1. Huyu mwanamke ndie aliyeteka uumbaji ukafanyika chini yake ila sio kwa kusudi la CHANZO HALISI, freemason na wayahudi ndo wanamwita Sophia ila ni roho chipukizi iliyotokea baada ya Moyo wa mwanzo kushindwa kutekeleza alichokuwa amepewa.

Hatua ya pili Alipotaka zitokee sifa akatokea nyoka(hila) Ufunuo 12:3

Hatua ya tatu Alipotaka kuwepo amani ya Kila kitu ikatokea vita. Ufunuo 12:7

Hivyo mafaili yote ya viumbe vyote yaliwekwa katika huo Moyo wa mwanzo rejea Yeremia 1:5 na warumi 8:29 Ili viumbwe kwa uhalisia (muonekano) ila baada ya kutekwa na mwanamke ndio uumbaji ukawa unafanyika kwa amri na matakwa ya huyo ufunuo 12:1 (mwanamke). Ndo maana mchawi au mganga alikuwa anaweza kuona nyota yako na vitu ulivyokusudiwa kuwa navyo kabla hujazaliwa nakuviiba sababu wao ndiyo walikumiliki na kuwa katika yao. Isaya 26:13-18

Ilikuwa ni ngumu kuyajua haya pasipo kupata ufahamu ulio juu ya thiolojia ambapo ni kumjua Aliyeumba.
Ili utoke kwa huyo mmiliki Mhubiri 7:26.

Mungu wa freemason ambaye Dunia na ulimwengua unamuabudu kwa kujua au kutokujua unamkuta katika mistari ifuatayo 2korintho 4:4, yeremia 44:17-18, ufunuo 12:1, matendo 19:27 aliyepotosha fikra za wengi wasimjue aliyeumba.

Majira ya kanisa (sio dini) mwezi unasiku 28 ivyo mwaka unasiku 336 ila Dunia iliongeza siku ya 29,30 na 31, mwaka ukawa na siku 365 kukawa na ongezeko la mwezi mmoja.Ndo kalenda ya Gregory inayotumika Hadi Leo.Ndo maana katika mashirika na taasisi kubwa watu hulipwa mshahara wa mwezi wa 13 inapofika December.

Kanisa (sio dini) siku zake ziko kama ifuatavyo:-

Jumatano- Nuru Moja Halisi
Alhamisi- Akili Moja Halisi
Ijumaa- Thamani Moja Halisi
J/mosi- Majira Moja Halisi
J/pili- Moyo mmoja Halisi
J/tatu- Hatma Moja Halisi
J/nne- Kustareheshwa na CHANZO HALISI

Iliuyajue haya lazma upate ufahamu ambao upo juu ya thiolojia, elimu ya Dunia na ulimwengu.Haya yote ninayokwambia ni kwa sababu tupo katika ufalme mwengine kabisa ambao ni waaliyeumba.Ufalme hauji kwa kuchunguzwa 1petro 1:10, Kila aliyechunguza hakuwa na majibu sahihi kuanzia nabii paka mtume ndio maana na kumjua Mungu wa Kweli ni ufahamu mithali 9:10.

 
Hello JF,

Katika uumbaji wa vitu vyote vinavyoonekana Kuna hatua za uumbaji na majira ambayo hayo yote yalitokea.

Ufahamu wa aliyeumba yaani Mungu Baba ambaye uhalisia wake ni CHANZO HALISI (REAL SOURCE) alikuwa peke yake (MAHALI PAKE)kabla ya roho na nafsi yeyote, ndipo akasikia uumbaji ukimsifu ndani ya Moyo wake, akatamani uwe halisi Zaburi 98.Ndipo akaengua Moyo wake kushoto (Moyo wa mwanzo)na kuweka heshima na utajiri (vyote vya kuumbwa) mithali 3:16 Ili aviumbe viwe halisi ila yeye hakuingia ndani ya huo Moyo.

Moyo wa mwanzo akaanza uumbaji katika mwanzo 1:1. Hatua ya kwanza Alipotaka litokee kanisa (sio dini) akawaza akatokea Mwanamke (sio hawa mnaowajua) ishara ya kwanza mbinguni ufunuo 12:1. Huyu mwanamke ndie aliyeteka uumbaji ukafanyika chini yake ila sio kwa kusudi la CHANZO HALISI, freemason na wayahudi ndo wanamwita Sophia ila ni roho chipukizi iliyotokea baada ya Moyo wa mwanzo kushindwa kutekeleza alichokuwa amepewa.

Hatua ya pili Alipotaka zitokee sifa akatokea nyoka(hila) Ufunuo 12:3

Hatua ya tatu Alipotaka kuwepo amani ya Kila kitu ikatokea vita. Ufunuo 12:7

Hivyo mafaili yote ya viumbe vyote yaliwekwa katika huo Moyo wa mwanzo rejea Yeremia 1:5 na warumi 8:29 Ili viumbwe kwa uhalisia (muonekano) ila baada ya kutekwa na mwanamke ndio uumbaji ukawa unafanyika kwa amri na matakwa ya huyo ufunuo 12:1 (mwanamke). Ndo maana mchawi au mganga alikuwa anaweza kuona nyota yako na vitu ulivyokusudiwa kuwa navyo kabla hujazaliwa nakuviiba sababu wao ndiyo walikumiliki na kuwa katika yao. Isaya 26:13-18

Ilikuwa ni ngumu kuyajua haya pasipo kupata ufahamu ulio juu ya thiolojia ambapo ni kumjua Aliyeumba.
Ili utoke kwa huyo mmiliki Mhubiri 7:26.

Mungu wa freemason ambaye Dunia na ulimwengua unamuabudu kwa kujua au kutokujua unamkuta katika mistari ifuatayo 2korintho 4:4, yeremia 44:17-18, ufunuo 12:1, matendo 19:27 aliyepotosha fikra za wengi wasimjue aliyeumba.

Majira ya kanisa (sio dini) mwezi unasiku 28 ivyo mwaka unasiku 336 ila Dunia iliongeza siku ya 29,30 na 31, mwaka ukawa na siku 365 kukawa na ongezeko la mwezi mmoja.Ndo kalenda ya Gregory inayotumika Hadi Leo.Ndo maana katika mashirika na taasisi kubwa watu hulipwa mshahara wa mwezi wa 13 inapofika December.

Kanisa (sio dini) siku zake ziko kama ifuatavyo:-

Jumatano- Nuru Moja Halisi
Alhamisi- Akili Moja Halisi
Ijumaa- Thamani Moja Halisi
J/mosi- Majira Moja Halisi
J/pili- Moyo mmoja Halisi
J/tatu- Hatma Moja Halisi
J/nne- Kustareheshwa na CHANZO HALISI

Iliuyajue haya lazma upate ufahamu ambao upo juu ya thiolojia, elimu ya Dunia na ulimwengu.Haya yote ninayokwambia ni kwa sababu tupo katika ufalme mwengine kabisa ambao ni waaliyeumba.Ufalme hauji kwa kuchunguzwa 1petro 1:10, Kila aliyechunguza hakuwa na majibu sahihi kuanzia nabii paka mtume ndio maana na kumjua Mungu wa Kweli ni ufahamu mithali 9:10.
 
2 Wathesalonike 2:10-12 (KJV) na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.
 
Mtoa mada anachanganya kati ya Roho na Moyo. Moyo ni organ ya mwili na Roho ni Uhai. Moyo ni organi ya mwili kazi yake kugawa damu na hewa, wakati Roho ni uwezo wa kuwepo au kuishi.

Pili mtoa maada anamueleza Mungu kwa kutumia akili, ambayo haiwezi kumjua Mungu. Kwani akili inatambua kwa kutumia vipimo vya Muda na nafasi (dimension of time and Space) akili inatambua maumbo na mabadiliko wakati Mungu hana mwanzo wala mwisho, hana umbo yuko wakati wote, kwa maana hiyo ni sawa na kusema yuko kila mahali wakati wote (Infinty state of consciosness). Mungu anajulikana na binadamu kiroho kwani Roho ya binadamu ikiondoa unafsi pia iko na infinity consciosness ambao ndio inaitwa hali ya Kweli. Ili umjue Mungu ni lazima upate spiritual initiation (Ubatizo wa Kiroho) Uzaliwe mara ya pili.

Yesu alibatiza kwa Roho na alifundisha wafuasi kumuabudu Mungu Kwa njia ya Roho na katika hali halisi ya Mungu (Kweli) ambaye pia ni Roho. Yesu hakufundisha Imani kwa Mungu, bali wafuasi wake wawe na Imani nae ya kuwa anamafundisho ambayo wakimpa nafasi ya kuwafundisha, watapata kujua njia ya uzima wa milele, na watamjua Mungu na hawatakufa tena. Bahati mbaya tunazani kutokufa tena kwamba huu mwili nyama ndio utakaa milele hapana, alimaanisha Roho. Yesu aliwatambulisha wafuasi wake kwenye ulimwengu wa Kiroho au Spiritual awareness. Au kujitambua kiroho ambako kunaletezea kumjua Mungu ambaye ni Roho.

Kuamini kuhusu Mungu haifanyi kuwa unamjua Mungu au ndio inahalalisha kuwa umeishi kwa mapenzi ya Mungu. Mapenzi ya Mungu ni Umjue na uwe pamoja nae Rohoni (Mbinguni) To be One with God or to attain Oneness state of consciousness.
 
Mungu wa Israel tuwaachie Waisrael, Mungu wa Waarabu twaachie Waarabu, sisi Waafrika turudi kwenye asili yetu,kwani Mungu wa kweli anapatikana kwenye asili yetu.
 
Back
Top Bottom