wisdom mapambano
Senior Member
- Jul 17, 2018
- 140
- 192
Heri,
(1) Nabii Isaya katika kitabu cha Isa.4:2, alisema ipo majira ambapo kutakuwepo na chipukizi zuri. Hapa Nabii Isaya alikuwa na maana kuwa kilichokuwepo huko nyuma ni chipukizi la mabaya. Moja ya chipukizi la mabaya ambalo ndilo kubwa kuliko yote ni lile la Nafsi ya mvamizi ambalo limeandikwa katika Ufunuo 12:1-9, hasa Ishara ya kwanza mbinguni (Ufu.12:1), ambaye ndiye sababisho la Ishara ya pili (nyoka) na Ishara ya tatu (vita) mbinguni.
CHANZO CHA MEMA NA MAZURI, yaani CHANZO HALISI, aliisikia Sauti ya sifa ndani ya moyo wake (Zaburi 98), akataka iwe halisi ili apate wa kumpa Ibada, yaani kusudi lake la tangu CHANZO. Ili itokee, aliumba Moyo wa Mwanzo na kuweka ndani yake Heshima na utajiri (kushoto) na siku nyingi (kulia), kama tusomavyo haya katika Mithali 3:16.
Katika moyo huu wa mwanzo, CHANZO HALISI mwenyewe, hakuingia ndani yake, bali aliweka nguvu za uumbaji, ili Moyo wa Mwanzo ndiye atekeleze uumbaji.Hapo ndipo chipukizi la mabaya lilipotokea kwa mara ya kwanza, kwa maana ya nafsi ya uvamizi, kama tunavyosoma katika Ufunuo 12:1. Nafsi ya Uvamizi aliteka kila file ambalo lilikuwa ndani ya moyo wa mwanzo. Wakati Moyo wa Mwanzo anaendelea kujiuliza maswali, kulitokea tena Ishara ya pili mbinguni. Ile HILA ya Ishara ya kwanza kugeuza kila file lililokutwa ndani ya Moyo wa Mwanzo, ilisababisha nyoka achipuke (Ufu.12:2-4). Kilele cha Ishara ya kwanza mbinguni ni hila. Aidha, kilele cha Ishara ya pili ni hila vilevile!
Kitu ambacho napenda wewe msomaji wa ufahamu huu uelewe ni kwamba chipukizi la mabaya hutokea bila mbegu iliyopandwa na bila kiini chochote! Hivyo, chipukizi la mabaya ni kitu kibaya kwa kuwa ni kitu kinachotokea tu kuleta uharibifu bila kusimama popote. Kwa hiyo Nabii Isaya alivyoandika katika Isa.4:2, kuwa ipo majira ambayo litakuwepo chipukizi la mazuri, alikuwa ameona kuwa iko majira ambapo uumbaji utavuka geti hili lililochipuza mabaya.
Kuanzia pale hapakuwahi tena kuwepo na mazuri. Kila kilichoumbwa kikawa mikononi mwa nafsi ya mvamizi ambaye ni chipukizi la mabaya. Nani angetuvusha hapo, na angefikia wapi? Ni lazima awe aliyeumba Moyo wa Mwanzo na apate pa kufikia ndipo kwa uweza wake tuvuke kituo hicho cha chipukizi la mabaya.
(2) Katika Warumi 8:23, imewekwa vizuri kuwa sisi sote tulikuwa ni malimbuko ya Roho na nafsi, matokeo yake ikawa ni kuugua tu. Nafsi kwa kuwa haionekani nayo pia ni Roho. Kwa kuwa Nafsi ya mvamizi ni roho, uumbaji unaoonekana kwa macho, ukawa hauna nguvu kama ule wa rohoni. Ndiyo maana badala ya Mbingu na Nchi, kukatokea dunia na ulimwengu ambavyo havionekani. Katika Mwanzo 1:1, ili kusudiwa Mbingu (Moyo) na Nchi (Uzao Halisi), lakini kilichotokea kikawa ni dunia na ulimwengu!
Nafsi ya uvamizi baada ya kuteka Moyo wa Mwanzo, ambaye ndani yake alikuwa na mafaili ya kila aliyekusudiwa, aligeuza moyo ukawa mwili (Rum.8:4-7). Maana yake ni kwamba, badala ya Moyo wa Mwanzo kuwa upendo (I Korintho 13:13c),aliugeuza kuwa adui wa Aliyeumba, yaani mwili. Kwa hiyo kila kilichoumbwa kikawa ni adui wa CHANZO HALISI na kila aliyeumbwa akawa ni adui na Aliyemuumba!
Hapa kulikuwepo na mtihani mkubwa mno kuwa ni nani ambaye atasababisha tuwe Moyo tena kama ilivyokuwa imekusudiwa (Mbingu); na ni nani atasababisha tuwe nchi kama ilivyokuwa imekusudiwa (Uzao Halisi wa CHANZO ilikuwa ni lazima awe Mwenyewe). Hapa ilikuwa CHANZO HALISI Mwenyewe na apate pa kufikia juu ya nchi palipokusudiwa. ambapo ndipo mahali
Ebu soma vizuri Mwa.2:7, utagundua kuwa hata Adamu wa kwanza alikuwa Nafsi Hai, siyo Moyo! Ina maana kuwa mmiliki wa mtu aliyekabidhiwa Bustani ya Edeni alikuwa ni nafsi ya mvamizi! Hapa tuseme kweli, hakuna ambaye angeturejesha kuwa Moyo tena kama ilivyokusudiwa na kuwa Uzao Halisi wa CHANZO Mwenyewe, kama siyo CHANZO HALISI aliyekuwepo kabla ya Moyo wa mwanzo.
Katika Rum.8:23, imeandikwa kuwa kila mmoja limbuko lake ni hapo kwenye roho na nafsi. Hivi tungetokaje hapo kama CHANZO HALISI asingekuja mwenyewe na kama asingepata pa kufikia ambapo ni sahihi na halisi?
(3) Katika Mwanzo 1:2-3, kuna jambo kubwa. Wakati uumbaji unaanza katika mstari wa tatu (3), tayari giza, ukiwa na utupu alikuwa ametulia katika mstari wa pili (2). Maana yake ni kwamba bado, Jeshi la giza, ukiwa na utupu lilikuwa lina madai ya kutangulia kila kilichoumbwa. Ndiyo maana katika Kutoka 20:21, Mungu aliongea na Musa kutoka gizani! Hata kama Mungu angekuwa nuruni, kwa hali hii tunayoisoma katika Mwanzo 1:2, ile sauti ilikuwa lazima ipite gizani!
Katika II Korintho 4:6, kitabu kinasema, nuru ilitoka gizani! Kwa maana hiyo ni kwamba, kwa kuwa uumbaji wote ulifanyika wakati giza, ukiwa na utupu yupo; ina maana kwamba waliotumwa wote (Ufu.21:9) walikuwa hawawezi kufuta jeshi la giza, ukiwa na utupu. Swali linabaki ni lile lile, nani angetuvusha ng'ambo ya hilo giza, ukiwa na utupu, ili tupokee utajirisho kutoka kwa CHANZO HALISI? Jibu ni kwamba ilikuwa ni lazima awe CHANZO HALISI na apate pa kufikia juu ya Nchi.
(4) Katika Rumi 7:15:21, kuna tabia ya asili tunayoikuta hapo. Unapenda kufanya mema lakini unashindwa. Yale mabaya usiyoyapenda, ndiyo unayoyatenda. Hiyo ndiyo tabia ya asili ambayo kila mtu na kila mwanadamu (hata kama ni mtakatifu) alijikuta anayo. Tumeona kuwa uumbaji wote, ulimilikiwa na nafsi ya mvamizi au mteka nyara wa Moyo wa Mwanzo. Huyo mteka nyara ndiye mtu; mwanadamu; roho; nafsi; mauti; chipukizi la mabaya; kifo; uharibifu; dhambi; uasi; uovu; na kadhalika. Vyote vibaya vilianzia kwake na hiyo ndiyo asili iliyoleta kitu kinachoitwa mila na desturi. Kila mmoja alijikuta ni lazima arithi aliyoyakuta. Na kwa kuwa nafsi ya uvamizi, yaani mteka nyara ndiye mabaya yote, kila mmoja alijikuta anarithi hayo mabaya yote:
* Kerubi alirithi hayo;
* Adamu wa kwanza alirithi hayo;
* Nuhu alirithi hayo;
* Ibrahimu alirithi hayo;
* Musa alirithi hayo;
* Eliya Mtishbi alirithi hayo;
* Yesu (kwa kuwa hata yeye licha ya kuwa Mwana wa Mungu) alikuwa ni Nabii (Yoh.6:11-13) na Mtume (Yoh.17:5), ilibidi arithi hayo;
* Adamu wa pili naye pia alirithi hayo.
* Miaka 1000 ndiye alikataa kwa Barabara ya kumpisha CHANZO HALISI (aliyekuwepo kabla ya mabaya yote). Pamoja na Miaka 1000 kumpisha CHANZO HALISI, huyu CHANZO HALISI hakuja moja kwa moja, alileta kwanza jina jipya (Ufu.3:12; I Kor.15:24-28).
Hilo jina jipya likaja na upendeleo wa kutisha (Isa.60:10), tukavuka: Bonde la uvuli wa mauti (Ufu.11 hadi 22); mto usiovukika (Eze.47:5); ulimwengu wa roho (Efe.2:5-8); korongo la giza (II Kor.4:6); tukaingia Bustani Mpya (II Pet.3:13); na Shamba jipya (Isa.65:24-25).
Baada ya mitihani yote kwisha ndipo sasa CHANZO HALISI kaja kuvutusha mahali Moyo wa Mwanzo alipokwamia.
Swali linarudi pale pale tena, kwamba nani angetuvusha hapo alipokwamia Moyo wa Mwanzo na mauti ya kila aina ikaanzia hapo, bila CHANZO HALISI Mwenyewe? Na kama CHANZO HALISI asingepata pa kufikia juu ya Nchi ingekuwaje?
(5) Katika Zaburi 51:5, Daudi Pamoja na kuwa kipenzi cha Mungu na mwenye Moyo wa kuyafanya mapenzi ya MUNGU yote (Mdo.13:22), alikutana na geti la kuumbiwa katika uovu hatiyani. na kuchukuliwa mimba
Hii ni kusema kwamba, kwa kuwa Moyo wa Mwanzo ndio uliopewa agizo la uumbaji na ukatekwa nyara, hakuna aliyekuwa salama katika hili la kuumbiwa hatiyani. Kila aliyeumbwa aliumbiwa hatiyani, kwa sababu ya Mwa.1:2 na Ufunuo 12:1-9. Ndiyo maana waliotumwa wote wakajikuta wameishia njiani kwa mujibu wa Dan.7:21 na Ufu.13:5-7.
Swali linarudi tena; nani angetutoa katika kituo cha kuumbiwa hatiyani na kuzaliwa katika uovu, kama CHANZO HALISI asingekuja yeye Mwenyewe na akapata pa kufikia ambapo ni sahihi?
(6) Katika I Kor.15:51, Mtume Paulo aliandika kuwa hatutalala sote bali sote tutabadilika. Katika kitabu cha Muhubiri chote, imeandikwa kuwa hakuna jipya, ikiwa ikiwa na maana kwamba mauti ndiyo imesababisha jipya lisiwepo. Katika Hosea 13:14, hata hivyo, iliandikwa kuwa majira itakuja ambayo tutakombolewa kutoka kwenye nguvu za kaburi na mauti. Kwa jinsi tulivyoona kuwa mauti na kaburi vilianzia kwenye lile chipukizi la mabaya; hakuna ambaye angetukomboa na nguvu ya kaburi zaidi ya CHANZO HALISI. Hivyo, ilikuwa ni lazima aje juu ya Nchi na apate mahali pa kutua.
(7) Katika Ufu.1:8, tuna Alfa na Omega yaani Mwanzo na Mwisho. Huu ndio Moyo wa Mwanzo na kila mmoja aliumbiwa hapo kwenye Moyo wa Mwanzo,ambapo kuna mahali pa kuanzia na kuishia. ili kutoka kwenye level ya Moyo wa Mwanzo, ni lazima uhamie ng'ambo Mwanzo.1:1 Ufunuo:12:1, ambapo ndipo kuna Mlima wa CHANZO HALISI au palipokusudiwa.Kwa ufupi, ilihitajika Kituo cha kumpokea CHANZO HALISI ambaye ni upendo uliopitiliza, yaani upendo usiobagua yeyote ndipo tufike palipokusudiwa. Kwa ufupi, Kituo cha Baba Halisi kilihitajika ili kumpokea CHANZO HALISI juu ya Nchi atupeleke ng'ambo ya Mwanzo 1:1 na Ufunuo 12:1 ndipo asambae kote kuhudumia kila mmoja aliyekubali kusamehewa bure (Isaya 43:25).
Nini nafasi ya Mwana wa Azali?