Kumiliki simu ya TECNO kuna raha zake bwana!

Kumiliki simu ya TECNO kuna raha zake bwana!

- Mara una type message characters zinajiongeza zenyewe!

- Unaongea mtu, ukikata simu haikati mpaka ung'oe betrii!

- Unafungua screen, inagoma kufunguka hadi uzime uwashe!

- Unasave namba ya mtu, siku unakuta mara imepotea.

- Muziki wake utadhani una suboufer!

- Mafundi wake na spare zake vimejaa kedekede kila kona!

- Zinatuunganisha haswa, kila unayekutana nae anayo!

Hongera TECNO.
Na kweli tecno connecting people hahaha
 
Kuna jamaa yangu mmoja nilimkopesha pesa sasa akashindwa kulipa akasema anipe smartphone yake ya itel kufidia deni, niliikataa japo muda huo nilikuwa natumia kitochi maana simu yangu kubwa ilitumbukia baharini. Itel sijui ni nini kile, ila cha msingi mawasiliano tu tusiseme mengi maana life linapindukaga unakosa hata hiyo itel.
Itel ni simu ya kutumia ukiwa ndani ya chandarua na sio mtaani
 
Nilikiwa mtumiaji mzuri wa samsung ila chaji ikanifanya nizichukie, nilihamia tecno c9 mwaka wa pili sasa pamoja na kuziponda kwenu ila sijawahi kujuta wala sijaexpiriance any of your prblems, kwangu tecno iko poa sn ila tunadharaulika sn,
 
Watumiaji wa i phone wanajiona washafika mbinguni
[emoji3][emoji3]

Mm nna OPPO langu, life linaenda.
be.like.bro-20181016-0002.jpeg
 
Back
Top Bottom