Asante CCM
JF-Expert Member
- Jun 22, 2023
- 346
- 1,301
Kama lipo jambo la hatari ambalo wenye Mamlaka wanataka kulifanya, basi ni kuanza kumfuatilia Tundu, huku wakimwandikia barua za miito ya mashtaka.
Jamani, Lissu hana cha kupoteza hapa Duniani. Tundu, ni mfanya siasa aliyepitia kiwango cha juu na cha mwisho kwa mwana siasa wa upinzani kuteswa! Namaanisha, kupigwa mabomu ya machozi, kuzuiliwa mahabusu na hata kupigwa risasi, Lissu ameshayapitia yote hayo. Na hata kupigwa ngwala, Lissu alishapigwa za kutosha!
Shime, wenye Mamlaka, mpuuzeni Tundu endapo mnataka kutawala kwa amani.
Mwisho, kutaka ligi na Lissu ni sawa na kuwasha moto nyikani! Na kama lipo jambo Mnyaturu yule hupenda, basi, ni ligi ya kisiasa yenye michezo ya kisheria ndaniye. Kwa tunaomfahamu Mnyampaa yule, katulia na acheni kumchokoza kwa barua za miito. Vinginevyo, atawaumbua tu.
Jamani, Lissu hana cha kupoteza hapa Duniani. Tundu, ni mfanya siasa aliyepitia kiwango cha juu na cha mwisho kwa mwana siasa wa upinzani kuteswa! Namaanisha, kupigwa mabomu ya machozi, kuzuiliwa mahabusu na hata kupigwa risasi, Lissu ameshayapitia yote hayo. Na hata kupigwa ngwala, Lissu alishapigwa za kutosha!
Shime, wenye Mamlaka, mpuuzeni Tundu endapo mnataka kutawala kwa amani.
Mwisho, kutaka ligi na Lissu ni sawa na kuwasha moto nyikani! Na kama lipo jambo Mnyaturu yule hupenda, basi, ni ligi ya kisiasa yenye michezo ya kisheria ndaniye. Kwa tunaomfahamu Mnyampaa yule, katulia na acheni kumchokoza kwa barua za miito. Vinginevyo, atawaumbua tu.