Kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha Abdul Sykes makala za Aisha ''Daisy" Sykes Buruku katika gazeti la Raia Mwema la Jumatano

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,916
30,259
KUMBUKUMBU YA MIAKA 50 YA KIFO CHA ABDUL SYKES MAKALA ZA AISHA ''DAISY" SYKES BURUKU KATIKA GAZETI LA RAIA MWEMA LA JUMATANO

Kuanzia toleo la kesho tarehe 10 Oktoba Aisha ''Daisy'' Sykes Buruku anaeleza yale aliyoshuhudia nyumbani kwao wakati baba yake anaijenga TANU kuwa chama imara cha ukombozi wa Tanganyika:

''...ilikuwa katika kipindi hiki cha mimi kuanza kupata akili katika kukua kwangu ndipo nilipokutana na wanawake wazalendo waliokuwa wanaochipukia katika uongozi wa Tanganyika, wanawake kama Bi. Lucy Lameck kutoka Moshi, Mary Ibrahim na akina mama wa Kiislam kama Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Hawa bint Maftah, hawa kutoka Dar es Salaam, wote hawa kwangu mimi walikuwa bibi zangu.

Kitu cha kufurahisha ni kuwa hawa akina mama wa Kiislam wote walivutwa katika siasa na Bibi Chiku bint Kisusa, maarufu akijulikana kama Mama Sakina. Alikuwa Mama Sakina ndiye aliyewapa hawa wanawake wa Kiislam niliowataja hapo juu utambulisho na wakaja kuwa watu maarufu.

Baba yeye ndiye alikuwa kiongozi wa mikakati hii yote kwa sababu bila yeye kuwatia hima kwa kutumia ushawishi wake ingekuwa vigumu kuweza kuwatia hawa wanawake katika kuwahamasisha wanawake wenzao wa Kiislam na wao watoke majumbani kuja mstari wa mbele katika mikutano wakiimba na kutoa vibwagizo vya kuunga mkono TANU na kudai uhuru.

Hili jambo lilikuwa jipya, jambo ambalo katika utamaduni wetu kwa wakati ule halikutarajiwa na ni kinyume katika utamaduni wetu kwa wanawake wa Kiislam kulifanya katika siku zile.

Nimesikia mazungumzo mengi wakati baba na wenzake walipokuwa wakijadili majina na shughuli ambazo hawa akina mama walikuwa wahusishwe ili kuleta mvuto wa kisiasa katika mikutano yao ya TANU.

Nakumbuka vizuri sana jinsi baba alivyokuwa karibu sana na Mwalimu Sakina na ndugu yake Mwalimu Fatna (wote hawa watoto wa Mama Sakina), na jinsi alivyowaleta ndugu hawa karibu na Mama Maria na hawa wakamjulisha Mama Maria Nyerere kwa mama yao na mashoga zake Bi Hawa Maftaha, Bibi Titi Mohamed na Bi Tatu binti Mzee...''


Kulia ni Bi. Tatu bint Mzee, Bi, Titi Mohamed, na wa kwanza kushhoto ni Bi. Chiku Said Kisusa wakiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere Uwanja wa Ndege safari ya kwanza UNO 1955
 
Ulimwengu unapaswa kufahamishwa juu ya historia hii adhwimu iliyofichwa kwa malengo na faida ya kikundi kidogo.
Ukweli utawaumbua hakika.
Ipo siku,
Shukrani kwa makala
 
Asante kwa historia nzuri iliyofichwa. Ila unatupa mashaka wengine kwa udini. Neno wanawake wa Kiislam umelirudia mara nyingi sasa sijui nia yako ni nini! Majina yao yatosha tu maana yanawatambulisha uislamu wao, hakuna walei wenye majina hayo.
 
Asante kwa historia nzuri iliyofichwa. Ila unatupa mashaka wengine kwa udini. Neno wanawake wa Kiislam umelirudia mara nyingi sasa sijui nia yako ni nini! Majina yao yatosha tu maana yanawatambulisha uislamu wao, hakuna walei wenye majina hayo.
Chachu,
Hiyo makala kaandika Aisha Daisy Sykes Buruku.
Huo msisitizo hata mie nimeuona.
 
Huyu bwana na Makwahia wa kuhenga huwa sisomagi makala zaidi kwani lazima ziingize udini hata kwa kificho
 
Mzee wa kula, kunywa, kupumua, kunya, kukojoa, kujamba SYKES. No SYKES, no life. Mind numbing obsession with everything SYKES-related.
 
Mzee wa kula, kunywa, kupumua, kunya, kukojoa, kujamba SYKES. No SYKES, no life. Mind numbing obsession with everything SYKES-related.
Ndjabu...
Ondoa tu hayo matusi hayana maana lakini yote uliyoandika ni muhimu.
Obsession honestly...

Hakika kisa cha akina Sykes ni kisa mimi kimenikamata sana.

Achilia ule udugu lakini siku niliposoma kitabu, ''Modern Tanzanians,''
kitabu alichohariri John Iliffe na kusoma, ''The Townsman: The Life of
Kleist Sykes,'' sura iliyoandikwa na mjukuu wa Kleist Sykes, Aisha
''Daisy'' Sykes Buruku
historia hii ilikamata fikra zangu (Modern
Tanzanians
, (ed), East African Publishing House, Nairobi, 1973).

Nakumbuka kama vile jana nnilikuwa katika Maktaba ya Taifa, Arusha
ndipo nilipokikuta kitabu hiki.

Utafiti wangu wa kutaka kujua mengi ulianza siku ile.
Nikawauliza hawa ndugu zangu juu ya kitabu cha Iliffe.

Wakanifahamisha kuwa babu yao, Kleist Sykes kabla ya kufariki mwaka
wa 1949 alikuwa amenadika ''kitabu,'' ambacho alimwachia mwanae Abdul
Sykes
.

Kwa hakika hakikuwa kitabu bali mswada wa kitabu.

Mwanae Abdu Sykes, Daisy alipoingia Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki
mwaka wa 1967 kusoma Elimu na Historia ndipo alipokutana na John Iliffe
na huyu mwalimu wake baada ya kufahamu historia ya akina Sykes na yeye
kama mimi akakumbwa na hii ''obsession,'' akataka kujua mengi vipi walifika
Tanganyika kutoka Afrika ya Kusini.

Hapo ndipo Daisy akawa anachukua nyaraka zilizokuwa katika familia na
kumuonyesha Iliffe pamoja na mswada wa kitabu alichoandika babu yake..

Kutokana na nyaraka hizi Iliffe akaandika paper hii: '‘The Role of the African
Association in the formation and Realisation of Territorial Conciousness in
Tanzania.’ Mimeo, Universityof East Africa Social Sciences Conference,'' 1968.
'
Iliffe kapatwa na homa ya ''obsession,'' ya akina Sykes anataka kujua mengi
zaidi Daisy akipewa ''assignment,'' anakwenda kwa baba yake anauliza anapewa
maelezo na ushahidi wa nyaraka.

Iliffe kila akielezwa hili ndani linazuka jingine akataka kujua ilikuwaje Abdul Sykes
akawa General Secretary wa Dar es Salaam Dockworkers Union mwaka wa 1948.

Iliffe akapewa maelezo na nyaraka akaandika paper hii:‘A History of Dockworkers
of Dar es Salaam’ TNR, Dar es Salaam, 71, 1970.

Iliffe kama mimi miaka mingi baadae akawa Sykes, Sykes na Sykes.

Sijui kwa nini Iliffe hakuandika historia ya TANU kwa ukamilifu wake wala hakuwa
na shauku ya kukutana na Abdul Sykes, baba wa mwanafunzi wake hodari Aisha
''Daisy,' Sykes
ambae kamsaidia sana kuijua historia ya African Association na TANU.

Mohamed Said na yeye kwa kumsoma Iliffe gonjwa la Sykes likamkumba.

Mimi nikaamua kufanya kile Iliffe hakufanya nacho ni kuandika maisha ya Abdul Sykes
lakini nikaamua pia kuweka mguu wangu pale unyayo wa Iliffe ulipokanyaga.

Hapa ndipo ilipoaanza safari yangu iliyonifikisha hadi Imhambane kijiji kinachoitwa Kwa
Likunyi alipotoka Sykes Mbuwane kuelekea Laurenco Marquis akiwa ameongozana na
Chief Mohosh na Wazulu wengine kupanda manowari ya Wajerumani kuja Pangani kuanza
vita na Abushiri bin Salim mwishoni mwa miaka ya 1880.

Huyu Chief Mohosh ndiye akaja kujulikana kama Affande Plantan Tanganyika akiwa mkuu
wa Germany Constabulary.

Prof. Emmanuel Achiempong wa Harvard na yeye gonjwa la Sykes likamkumba akaniandikia
mwaka wa 2008 kuniomba anijumuishe katika mradi wa Dictionary of African Biography (DAB)
anataka niandike mchango wa Kleist Sykes katika historia ya Afrika.

Mradi huu ulijumisha waandishi na watafiti takriban 500 kutoka kila pembe ya dunia.
Oxford University Press, New York wamechapa volumes sita ya kazi hii.

Bwana Ndjabu,
Yako mengi lakini kwa leo tuuishie hapa sitaki kuwachosha wasomaji.
 
Asante kwa historia nzuri iliyofichwa. Ila unatupa mashaka wengine kwa udini. Neno wanawake wa Kiislam umelirudia mara nyingi sasa sijui nia yako ni nini! Majina yao yatosha tu maana yanawatambulisha uislamu wao, hakuna walei wenye majina hayo.

Mkuu:
Kwa ufahamu wa kawaida, sidhani kama kuna uhusiano mkubwa sana kati ya jina na imani ya mtu pamoja na kuzoeleka kushabihiana kati ya hivyo vitu viwili.
 
Ulimwengu unapaswa kufahamishwa juu ya historia hii adhwimu iliyofichwa kwa malengo na faida ya kikundi kidogo.
Ukweli utawaumbua hakika.
Ipo siku,
Shukrani kwa makala
Ukweli upi sasa kwamba wais.lam ndio mmeikomboa Tanganyika? Haya basi ni kweli nyie ndio majembe tumekubali, haya umepata nini sasa?
 
Huyu bwana na Makwahia wa kuhenga huwa sisomagi makala zaidi kwani lazima ziingize udini hata kwa kificho
Muda wote anaonaga wao wanabaguliwa sijui wanaonewa, sijui anatakaje huyu
 
Shark,
Nadhani mwandishi anaweka msisitizo kwa kuwa katika nyakati
zile mwanamke wa Kiislam ilikuwa tabu kujionyesha hadharani.
Na jambo hilo limewekewa msisitizo na ni ukweli kabisa. Ukienda Zanzibar utaelewa kwa nini kaweka msisitizo.
 
Back
Top Bottom