Polisi wanakodiwa na kuahidiwa kulipwa mamilioni ya pesa za mlipakodi/mwananchi/mlalahoi kwa ajili ya kuua raia wasiokuwa na hatia.
http://www.mwananchi.co.tz/hab...
Kuna mama wajawazito na watoto wadogo wanafariki hospitalini kwa kukosa huduma muhimu kwa kisingizio cha kukosa fedha lakini serikali inatumia pesa nyingi kiasi hiki kwa
ajili ya kuwaua wafuasi wa vyama vya siasa na waandishi wa habari.
Mashambulizi yapolisi dhidi ya CHADEMA na wafuasi wake ni mpango wa kishenzi unaosukwa na Chama Cha Magamba (CCM) na serikali yakeya kikauzu. Na jambo la kusikitisha ni kwamba badala ya kutumia bajeti ya chama hawa umbwa wa mafisadi wanalipwa mamilioni ya pesa za walipakodi kwa ajili ya kufanya kazi wanayotumwa na mafisadi.
http://www.mwananchi.co.tz/uch...
Watoto wa shuleza kata wanaketi chini kwa kukosa madawati, hawafundishwi kwa kukosa waalimu, na hawasomi kwa kukosa vitabu (wanaingia sekondari wakiwa hawajui kusoma wala
kuandika)! Lakini bado serikali hii ya mafisadi inatumia mamilioni ya fedha za
umma kiasi hiki kwa manufaa ya kuwafurahisha mafisadi! Ni lini hasa wananchi
mtaamka na kukataa upumbavu kama huu? Nchi ina matatizo lukuki badala ya
kuyashughulikia CHADEMA kana kwamba hili ndio tatizo kuu linaloisumbua nchi.
Jamani tuacheuchama katika hili na tujadili bila jazba. Inakuwaje serikali inachezea pesa za
umma na kuhatarisha amani ya nchi kama hivi huku tumekaa kimya?
Haya ni mauaji ya kulipwa. Serikali inayokodi watu kwa ajili ya kuua raia wasokuwa na hatia ni serikali ya kigaidi. Na wala tutakuwa hatujajosea kuiita hii seriakali kwamba ni yakwamba ni
serikali ya kigaidi. Inasikitisha kuona kwamba polisi wanakodiwa kwenda kuua
badala ya kwenda kuimarisha amani!
Mikono yaserikali hii ya mafisadi imejaa damu na hiyo damu haitapotea bure. Polisi
wakiitwa kwenda kulinda mikutano ya vyama vya upinzani, wanadai hawana nafasi,
lakini wakiitwa kwenda kuua na kulipwa posho, wako tayari kufanya hivyo! Hapa
pana tofauti gani na serikali ya kikoloni ikiyokuwa imejikita kwenye kuua tu?
Yaani polisi wanatumwa wakaue ili walipwe posho na wao wanashangilia kupokea
posho za damu? Tafakari, chukua hatua!