Kumbukumbu ya mauaji ya Daudi Mwangosi

Kumbukumbu ya mauaji ya Daudi Mwangosi

Leo ni mwaka wa pili toka aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Iringa Daudi Mwangosi auawe pale kijiji cha Nyororo Mufindi wakati akiwa katika kazi yake ya kuandika habari.
Serikali sikivu ya CCM japo imeoneshwa kila aina ya ushahidi imepuuza kuwachukulia hatua stahiki waliofanya ukatili huu.Tumeambiwa waliofanya ukatili huu wamepandishwa vyeo na watawala wetu wasikivu.
Dhihaka nyingi zimefanywa juu ya kifo hiki hata kufikia hatua ya mpiga propaganda Habibu Mchange kusema mauaji yalifanywa na CHADEMA.Anataka tuamini eti watu waliovalia sare za polisi tunaowaona kwenye picha ya mauaji ni CHADEMA na magwanda yao.
Familia yake na ndugu zake, IPC, UTPC na wadau wengine hawawezi kamwe kusahau mauaji ya Daudi Mwangosi kwani yalikua ni mauaji ya kinyama na ukatili wa hali ya juu.
Kuna kila dalili kwamba wauaji wameshajitangaza washindi hapa duniani.R.I.P Mwangosi.
 
Leo ni mwaka wa pili toka aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Iringa Daudi Mwangosi auawe pale kijiji cha Nyororo Mufindi wakati akiwa katika kazi yake ya kuandika habari.
Serikali sikivu ya CCM japo imeoneshwa kila aina ya ushahidi imepuuza kuwachukulia hatua stahiki waliofanya ukatili huu.Tumeambiwa waliofanya ukatili huu wamepandishwa vyeo na watawala wetu wasikivu.
Dhihaka nyingi zimefanywa juu ya kifo hiki hata kufikia hatua ya mpiga propaganda Habibu Mchange kusema mauaji yalifanywa na CHADEMA.Anataka tuamini eti watu waliovalia sare za polisi tunaowaona kwenye picha ya mauaji ni CHADEMA na magwanda yao.
Familia yake na ndugu zake, IPC, UTPC na wadau wengine hawawezi kamwe kusahau mauaji ya Daudi Mwangosi kwani yalikua ni mauaji ya kinyama na ukatili wa hali ya juu.
Kuna kila dalili kwamba wauaji wameshajitangaza washindi hapa duniani.R.I.P Mwangosi.
umesomeka Mkuu, inasikitisha sana!
 
Kamuhanda yeye baada ya mauaji ya Mwangosi said:
Unamaanisha alifanikiwa kuwashawishi wakubwa zake kuwa ameweza kazi nzuri na kustahili kupanda cheo? Huu waweza kuwa ni uchochezi wako .
 
daaah, sijui waliofanikisha mauji hayo wanajiskiaje aisee!? inauma,yaani jamaa ndio ameiacha familia yake kwa unyama mkubwa alofanyiwa tena na watu wenye jukumu la kutulinda!
 
Ni kweli unyama huu uliofanywa na askari hautasahaulika! Ninaamini damu ya Mwangosi itaendelea kuwafuata wauaji wote. Familia ya Mwangosi nawaombea Mungu aendelee kuwapa ujasiri na kuzidi kumuomba yy huku mkiamini ya kwamba ipo siku wauaji watapata hukumu toka kwa Mungu ijapokuwa hukumu ya kibinadamu haijatoka. R.I.P Shujaa Mwangosi.
 
Hivi ile kesi ya yule polisi aliyekuwa akifichwa sura na askari wenzie, kila alipokuwa akipandishwa kizimbani, hivi ile kesi 'iliyeyukia' wapi?

Kwa sababu hatujaona mwendelezo wa ile kesi na mshiriki mwenzake wa mauaji ya Mwangosi, kamanda Kamuhanda, hatukuona akipandishwa kizimbani, na badala yake, tukashuhudia mkuu wake JK, akimpandisha cheo!
Operesheni ya cdm ilisimama
 
Ingekuwa vyema kama hizi nguvu mgezipeleka kwa familia ya marehemu kusomesha watoto wake na kumsaidia mjane kiuchumi.

Hivi Ritz nilisikia hivi karibuni jamaa mmoja anasema hata mauaji ya Mwangosi kuna watu wa chama flani walihusika na magazeti yakasema sana sana hebu naomba unikumbushe mkuu ni nani yule?!
 
Chadema wanahusika na mambo haya-Kada Chadema.

Mkuu nikumbushe kuna jamaa mmoja wa chama hicho alitoa taarifa ndeeefu sana hivi karibuni juu ya uhalifu unaodaiwa kufanywa na chadema hivi ni nani yule?!

Na kama kuna mtu anayo hiyo taarifa abandike humu tuipitia na kuitafakari wakati tunamboleza kifo cha Mwangosi!!
 
mim huwa nawashangaa wakristo na waislamu wanapofunga kuombea chama .....kidumu na kiendelee kutawala vyema madarakan wakat wanadhambi bora hata ya osama,wanaua raia mwema wapandishwe cheo,jk tubu dhambi ya vijana wako japo hatujui kama uliwatuma au laa,ila kumpandisha cheo huyo jamaa ni pongez kwa kazi nzuri ya kummaliza daud mwangosi,
 
Mungu amlaze Mahala pema Marehemu Mwangosi.Wahusika wote wa mauaji ya Mwangosi,waanze kupata mapigo makali na laana hata kama sheria haitawatia hatiani kutokana na mipango ya wauaji kuizidi nguvu haki.
 
Huyu jamaa wa kushoto anayemfyatulia bomu Marehemu sehemu za tumbo, damu hii itamfuata kokote hapa duniani - amini amini nawaambieni, Mwenyezi Mungu hakuagiza tutoane roho kirahisi namna hii. Na walaaniwe wote na vizazi vyao waliokuwa nyumba ya mauaji haya ya kinyama!! Amen.


attachment.php
 
TAFAKARI YANGU KUHUSIANA NA PICHA YA MAUAJI YA MWANGOSI

Nikiwa nalengwa lengwa na machozi nimeiangalia na kuitafakari vizuri sana picha hiyo inayoonesha jinsi Mwangosi alivyotolewa uhai kikatilia sana. Mimi nimeiangalia na kuona kuna askari ambao walikuwa na uchu wa kumpiga na kuangamiza kabisa maisha ya Mwangosi na wale waliokuwa wanajaribu kuzuia wenzao asiendelee kushambuliwa na askari wenye uchu wa kutoa roho za watu. Mfano kuna askaari anayeonekana katikati akiwa ameshikwa kiunoni na Mwangosi huku Mwangosi mwenyewe akiwa ameshika kamera yake, anajaribu kwa kadiri awezavyo kuwazuia wenzake wasiendelee kumshambulia Mwangosi na ndio maana ilibidi Mwangosi ajishike kwake nafikiri wakati akianguka ili kujiokoa. Huyu askari anaonekana ameinua juu kirungu chake kama ishara ya kuwazuia wenzake wasiendelee kufanya unyama waliokuwa wakimfanyia Mwangosi. Kwakweli natamani kulijua jina la askari huyu pamoja na yeye mwenyewe. Alifanya jitihada za pekee lakini alishindwa kutokana na jinsi wauaji walivyokuwa na uchu na hasa huyu wa nyuma yake ambae ndio mlipuaji wa Mwangosi.

Mwingine anayeonekana kutaka kuzuia unyama huu ni huyo aliyeipa mgongo kamera. Huyu anaonekana kumzuia askari aliye kulia kwake ambaye anaonekana kwenda kwa kasi kumshambulia Mwangosi. Kuna huyo pia aliyevaa shati la kiraia akiwa na kofia nyeusi naye anaonekana kutaka kuzuia madhara zaidi.

Sasa askari watoa roho ni hao watatu wa upande wa kushoto au nyuma ya yule askari anayejitahidi kuzuia wenzake na ambaye ndiye ameshikwa kiunoni na marehemu Mwangosi. Hao ndio watoa roho wakuu wakiongozwa na huyo wa kushoto kabisa ambaye wakati huyo wa katikati anajitahidi kuzuia wenzake yeye akapata mwanya wa kufyatua kombora lake na kumtekeketeza kabisa mwanamwema Daud Mwangosi.

Huyo wa katikati ambaye ndiye anayeonekana kuwazuia wenzake huku Mwangosi akiwa amejishika kiunoni mwake anaonekana kama ni mtu aliyeona kuwa, kama ni kipigo alichokipata Mwangosi, basi kilikuwa kimetosha hivyo kuendelea zaidi ya hapo ingekuwa ni madhara makubwa ndio maana anajitahidi kuwazuia wenzake. Lakini kwa bahati mbaya alikuwa amezidiwa na askari waliokuwana uchu wa kumtoa roho Mwangosi.

Mimi binafi nawapongeza sana askari hao niliowaelezea kwa jinsi walivyojitahidi sana kuokoa maisha ya Mwangosi. Laana zote za duniani na mbinguni ziwaendee hao wengine wote waliohakikisha kuwa Mwangosi anafutika katika duniani hii kikatili kabisa, wa kwanza wao akiwa huyo Michael Kamuhanda na huyo mlipuaji wa bomu.

May the almighty God Rest In Peace the Innocent soul of Daud Mwangosi! AMEN!
Ooo


Majina yao yatajwe ili alie ua kwa upanga nae auwawe kwa upanga waislamu huamini hivi
 
Nao hao asikari wasakwe nao wauwawe popote walipo haki itendeke
 
Nao hao asikari wasakwe nao wauwawe popote walipo haki itendeke

Mkuu mie kila nikuangalia hiyo picha ya askari zaidi ya sita wakiwa na mabomu,bastola na virungu wakimshambulia mwandishi wa habari (wanayemfahamu) na kumuua najiuliza hivi kweli hii nchi iko salama? Tuna serikali kweli?


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Leo ni siku ambayo kaka yetu mpendwa Daudi Mwangosi alifariki, Machungu ya kushambuliwa kwa kipigo, kisha kwa bomu na kikosi cha FFU huko mkoani Iringa katika eneo la Nyololo chini ya amri iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Iringa wakati huo RPC Kamuhanda

Tunaweza kujifunza nini juu ya utashi wa viongozi wa dola la Tanzania katika utekelezaji wa sheria mbali mbali? Mimi sijui sana kama kweli tuna nia ya dhati ya kuwatoa wa Tanzania hapa walipo ili wayafikie maisha bora kwa kila mtanzania.

Kwa kuwa nilikuwepo siku ya tukio, nilishuhudia yote na kwa kuwa nilikuwa kiongozi wa chadema wakati huo. Ningeomba niwashirikishe machache juu ya tukio zima. nimeattach document ambayo, nimeiandika mimi mwenyewe kwa kutumia vithibitisho halali vya chama lakini pia vya jeshi la polisi. Mpango wangu ni kuandika kitabu. tutaendelea kuwasiliana pale inapobidi

Justin Mpotwa
kwa kukusaidia jina la huyo askari alie tekeleza unyama huo na kufikishwa kwa pilato anaitwa PASIFIKUS ALISOMEA SHULE MOJA HUKO BUKOBA VIJIJINI SHULE YA SECONDARY KISHOGO
 
kwa kukusaidia jina la huyo askari alie tekeleza unyama huo na kufikishwa kwa pilato anaitwa PASIFIKUS ALISOMEA SHULE MOJA HUKO BUKOBA VIJIJINI SHULE YA SECONDARY KISHOGO
Ahsante mkuu tuhabarishe vile vile yuko wapi sasa hivi!! ili-------------
 
Back
Top Bottom