Kumbukumbu ya mauaji ya Daudi Mwangosi

Kumbukumbu ya mauaji ya Daudi Mwangosi

Leo ni mwaka wa pili toka aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Iringa Daudi Mwangosi auawe pale kijiji cha Nyororo Mufindi wakati akiwa katika kazi yake ya kuandika habari.
Serikali sikivu ya CCM japo imeoneshwa kila aina ya ushahidi imepuuza kuwachukulia hatua stahiki waliofanya ukatili huu.Tumeambiwa waliofanya ukatili huu wamepandishwa vyeo na watawala wetu wasikivu.
Dhihaka nyingi zimefanywa juu ya kifo hiki hata kufikia hatua ya mpiga propaganda Habibu Mchange kusema mauaji yalifanywa na CHADEMA.Anataka tuamini eti watu waliovalia sare za polisi tunaowaona kwenye picha ya mauaji ni CHADEMA na magwanda yao.
Familia yake na ndugu zake, IPC, UTPC na wadau wengine hawawezi kamwe kusahau mauaji ya Daudi Mwangosi kwani yalikua ni mauaji ya kinyama na ukatili wa hali ya juu.
Kuna kila dalili kwamba wauaji wameshajitangaza washindi hapa duniani.R.I.P Mwangosi.
mwenye taarifa za wauaji ni huyu hapa!! tumtafute!!

image.tiff
 
Kuna mwendawazimu anayetuhumiwa kupanga mauji ya Dr. Slaa ameibuka na kusema CHADEMA ndio waliomuua Daud Mwangosi kule Iringa. Hivyo kwa mujibu wa wendawazimu wake hao wanaoonekana pichani wakiutoa uhai wa Mwangosi kama vile wanaua nyoka, ni CHADEMA. Kamuhanda yeye baada ya mauaji ya Mwangosi, alipandishwa cheo!
Wanasema picha imetengezwa na watalamu wa chadema na sio ya ukweli.
 
Kuna mwendawazimu anayetuhumiwa kupanga mauji ya Dr. Slaa ameibuka na kusema CHADEMA ndio waliomuua Daud Mwangosi kule Iringa. Hivyo kwa mujibu wa wendawazimu wake hao wanaoonekana pichani wakiutoa uhai wa Mwangosi kama vile wanaua nyoka, ni CHADEMA. Kamuhanda yeye baada ya mauaji ya Mwangosi, alipandishwa cheo!

yule kijana kuanzia aliposema CDM imemtumia askari wa kukodi ili kumuua Mwangosi nilimdharau kabisa Mchange,nilimuona hana tofauti sana na yule mdudu anayesukuma m.a.v.i
 
Mnamo mwezi Agosti na September 2012 Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kilifanya ziara ya ujenzi wa Chama (M4C) huko Mkoani Morogoro na Mkoani Iringa. Tarehe 02/09/2012 kulikuwa na ufunguzi wa Ofisi ya Chama katika Kijiji cha Nyololo. Polisi walizuia ufunguzi wa ofisi hiyo kinyume na taratibu na sheria kwa kisingizio cha kuendelea kwa zoezi la sensa ya watu na Makazi ambayo Kimsingi zoezi hilo lilikuwa limeisha na taasis na vyama vingine vya siasa vilikuwa vinaendelea na shughuli zao kama kawaida. Mathalani Chama cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa kinaendelea na kampeni huko Zanzibar.

CHADEMA tulisema agizo lile la kusitisha ufunguzi wa ofisi yetu halikuwa halali kwa sababu agizo la awali ilikuwa ni kusitishwa kwa mikutano ya hadhara peke yake na si mikutano ya ndani. Ufunguzi wa Ofisi yetu haikuwa mkutano wa hadhara. Polisi walijipanga kutumia nguvu kupita kiasi ambapo majira ya asubuhi waliwatangazia wananchi wasitoke nje wala kushiriki katika shughuli hiyo. Mchana ulipofika Viongozi na Wanachama wetu wakiongozwa na Mh. Benson Kigaila walifika eneo hilo la ofisi ambapo Polisi kwa upande wao wakiongozwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa Michael Kamhanda waliamua kutumia nguvu kuvunja shughuli hiyo na hatimaye askari wapatao saba wakiwa na silaha za moto walimzingira na kumlipua Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel Ten ndugu Daud Mwangosi kwa bomu na kumwaga utumbo palepale. Kwa kweli ilikuwa ni miongoni mwa matukio mabaya sana, na la kinyama kuwahi kutokea katika nchi yetu

Ndugu Wananchi Wenzangu leo ni takribani miaka miwili sasa imepita tangu kutokea kwa tukio hilo; hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na serikali kwa wahusika, Kamanda Kamhanda bado yuko mtaani kana kwamba hakufanya chochote tena alipandishwa na cheo kabisa baada ya tukio lile. Askari aliyefunguliwa kesi ambaye hatumfahamu na hatawahi kuonekana na wananchi hatujui hata kesi yake hiyo imeishia wapi tayari yameshafunika kombe mwanaharamu apite kama walivyosema Wahenga wetu.

Sisi kama Chama kupitia Kamati Kuu yetu tuliitaka serikali kupitia Rais kuunda tume ya kijaji kuchunguza matukio haya ambayo tumekuwa tukifanyiwa na polisi ambapo wanachama na mashabiki wetu wanauawa bila hatia lakini serikali imeziba masikio na isitoshe mauaji yameendelea. Mtakumbuka kule Soweto Arusha ambapo polisi hao hao walitupa bomu kwenye mkutano wetu wa hadhara na kuua watu wengine wanne. Morogoro walimuua Ally Zona, Igunga akafa Mbwana Masoud, Arumeru alichinjwa ndugu Mbwambo na watuhumiwa wakakamatwa lakini tunaambiwa walitoroka wakiwa mikononi mwa Polisi tena wenye bunduki za SMG. Napenda kurudia tena kuitaka serikali iunde tume ya kimahakama ili Taifa lijue ukweli na uhakika wa nani hasa anahusika na mauaji haya ya watu wetu.

Ndugu Wananchi wenzangu wakati umefika wa sisi kupaza sauti zetu kwa nguvu kuungana na vilio vya damu za ndugu zetu hawa na mateso ambayo makundi mbalimbali yanapata bila hatia katika jamii yetu. Tunao ndugu zetu Albino wanakufa na hakuna anayechukua hatua, wengine wanateswa na kudhalilishwa wakiwa mikononi mwa vyombo vya usalama na sheria kisa tu eti hawakubaliani na Serikali. Hivi karibuni tumesikia wanavyofanyiwa Masheikh 19 walioko mahabusu, wanadhalilishwa sana kisaikolojia. Kuna vijana wetu walibakizwa kesi za ugaidi nao waliteswa na kuharibiwa sehemu za siri na jeshi la polisi. Imefika wakati sasa tuunganishe nguvu zetu kupambana na ukatili huu.

Napenda kuchukua fursa hii kutoa salam zangu za rambirambi kwa familia ya marehem Mwangosi na kwa wanahabari wote. Nawatia moyo wanahabari kuwa majasiri hususan wakati huu tunapoelekea katika chaguzi mbalimbali katika nchi yetu. Mwalimu Nyerere alisema ukishakula nyama ya mtu hutaacha hivyo tunatarajia kabisa Polisi na Watawala wataendeleza mauaji haya hasa watakapoona dalili za wao kunyang’anywa dola lakini tusiogope tutashinda.

Dr.Wilbrod Slaa
Katibu Mkuu 02/09/2014
 
TAFAKARI YANGU KUHUSIANA NA PICHA YA MAUAJI YA MWANGOSI

Nikiwa nalengwa lengwa na machozi nimeiangalia na kuitafakari vizuri sana picha hiyo inayoonesha jinsi Mwangosi alivyotolewa uhai kikatilia sana. Mimi nimeiangalia na kuona kuna askari ambao walikuwa na uchu wa kumpiga na kuangamiza kabisa maisha ya Mwangosi na wale waliokuwa wanajaribu kuzuia wenzao asiendelee kushambuliwa na askari wenye uchu wa kutoa roho za watu. Mfano kuna askaari anayeonekana katikati akiwa ameshikwa kiunoni na Mwangosi huku Mwangosi mwenyewe akiwa ameshika kamera yake, anajaribu kwa kadiri awezavyo kuwazuia wenzake wasiendelee kumshambulia Mwangosi na ndio maana ilibidi Mwangosi ajishike kwake nafikiri wakati akianguka ili kujiokoa. Huyu askari anaonekana ameinua juu kirungu chake kama ishara ya kuwazuia wenzake wasiendelee kufanya unyama waliokuwa wakimfanyia Mwangosi. Kwakweli natamani kulijua jina la askari huyu pamoja na yeye mwenyewe. Alifanya jitihada za pekee lakini alishindwa kutokana na jinsi wauaji walivyokuwa na uchu na hasa huyu wa nyuma yake ambae ndio mlipuaji wa Mwangosi.

Mwingine anayeonekana kutaka kuzuia unyama huu ni huyo aliyeipa mgongo kamera. Huyu anaonekana kumzuia askari aliye kulia kwake ambaye anaonekana kwenda kwa kasi kumshambulia Mwangosi. Kuna huyo pia aliyevaa shati la kiraia akiwa na kofia nyeusi naye anaonekana kutaka kuzuia madhara zaidi.

Sasa askari watoa roho ni hao watatu wa upande wa kushoto au nyuma ya yule askari anayejitahidi kuzuia wenzake na ambaye ndiye ameshikwa kiunoni na marehemu Mwangosi. Hao ndio watoa roho wakuu wakiongozwa na huyo wa kushoto kabisa ambaye wakati huyo wa katikati anajitahidi kuzuia wenzake yeye akapata mwanya wa kufyatua kombora lake na kumtekeketeza kabisa mwanamwema Daud Mwangosi.

Huyo wa katikati ambaye ndiye anayeonekana kuwazuia wenzake huku Mwangosi akiwa amejishika kiunoni mwake anaonekana kama ni mtu aliyeona kuwa, kama ni kipigo alichokipata Mwangosi, basi kilikuwa kimetosha hivyo kuendelea zaidi ya hapo ingekuwa ni madhara makubwa ndio maana anajitahidi kuwazuia wenzake. Lakini kwa bahati mbaya alikuwa amezidiwa na askari waliokuwana uchu wa kumtoa roho Mwangosi.

Mimi binafi nawapongeza sana askari hao niliowaelezea kwa jinsi walivyojitahidi sana kuokoa maisha ya Mwangosi. Laana zote za duniani na mbinguni ziwaendee hao wengine wote waliohakikisha kuwa Mwangosi anafutika katika duniani hii kikatili kabisa, wa kwanza wao akiwa huyo Michael Kamuhanda na huyo mlipuaji wa bomu.

May the almighty God Rest In Peace the Innocent soul of Daud Mwangosi! AMEN!
Picha hii ina define uwezo wa askari wa kitanzania.Hii ni aibu kubwa!.Hapa tunaweza kujiuliza kama wamepewa elimu kuhusu haki za binadamu?,je wana ile human intellegence?,je wanaheshimu mwandishi wa habari?,maswahili ni mengi mno.Na wewe jiulize
 
Wanasema picha imetengezwa na watalamu wa chadema na sio ya ukweli.
Ni uendawazimu tu unawasumbua. Sasa kama ni hivyo kwanini wamemfungulia mashitaka huyo askari anayeonekana kumlipua Mwangosi? Kisheria tunamchukulia huyo askari kuwa ni mkosaji wa mwisho kwani alikuwa anatekeleza amri ya mkubwa wake Kamuhanda na ukienda juu zaidi baadaye inapanda mpaka kwa IGP na kisha kwa rais kama mkosaji mkuu kwani ndiye mwenye serikali na amiri jeshi mkuu. Katika nchi za wenzetu wanaojali haki za binadamu rais akiwa madarakani au akitoka anashitakiwa kwa kuamrisha, kufumbia macho au kuamuru mauaji ya raia asiyekuwa na hatia. Huku kwetu hata rais akiua mkewe au mwanae hashitakiwi. Ingekuwa ni huko kwa wenzetu tukio lile lilikuwa linamuondoa au kujiuzulu waziri wa mambo ya ndani, IGP na RPC madarakani na kisha kushitakiwa. Huku kwetu polisi wanaua raia halafu rais anasema ni "It is very unfortunate nitahakikisha halitokei tena"(kumbuka mauaji ya Arusha kwenye maandamano ya CHADEMA) halafu wiki inayofuata askari wanaua tena anakaa kimya na hachukui hatua zozote
 
RIP Shujaa mwangosi,nafikiri kuna sms ilikuwa imepenyezwa kwa baadhi ya askari kwasababu wengine hawakuwa wanataka aendelee kupigwa huku baadhi yao wakiwa wamedhamiria kuuwa
 
Hivi Ritz nilisikia hivi karibuni jamaa mmoja anasema hata mauaji ya Mwangosi kuna watu wa chama flani walihusika na magazeti yakasema sana sana hebu naomba unikumbushe mkuu ni nani yule?!
Mkuu mie navyofahamu Chadema walitengeneza CD ya mauaji ya Mwangosi na kumpa John Heche kuzunguka nayo Ulaya kuwaonyesha wazungu na kujipatia pesa lakini hakuna fungu lolote liloenda kwa mjane.

Cc: chama
 
Last edited by a moderator:
Hivi marehemu Mwangosi R.IP alikuwa ni kada wa Chadema.
 
Ingekuwa vyema kama hizi nguvu mgezipeleka kwa familia ya marehemu kusomesha watoto wake na kumsaidia mjane kiuchumi.
Ni jambo la ajabu na madharau pale uhai wa mtu anayetimiza wajibu wake wa kuitumikia taifa unapokatishwa bila sababu halafu ww unaongea maneno kama hayo.
 
Hivi marehemu Mwangosi R.IP alikuwa ni kada wa Chadema.
Ww unazungumzia mambo ya kada wa chama watu wanachoangalia ni ugeukwaji wa haki za binadamu bila kujali ametoka chama gani.
Au haki ya binadamu inatolewa na kuangalia kichama. Haki za binadamu haiangali chama, dini, kabila, rangi wala hali ya mtu.
 
daaah, sijui waliofanikisha mauji hayo wanajiskiaje aisee!? inauma,yaani jamaa ndio ameiacha familia yake kwa unyama mkubwa alofanyiwa tena na watu wenye jukumu la kutulinda!

WENZIO WAMEPANDISHWA VYEO , wewe UNASEMA WANAJISIKIAJE ?
 
Mkuu mie navyofahamu Chadema walitengeneza CD ya mauaji ya Mwangosi na kumpa John Heche kuzunguka nayo Ulaya kuwaonyesha wazungu na kujipatia pesa lakini hakuna fungu lolote liloenda kwa mjane.

Cc: chama
Kwaiyo wewe ndo ulisafiri na John Heche hadi ulaya?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mie navyofahamu Chadema walitengeneza CD ya mauaji ya Mwangosi na kumpa John Heche kuzunguka nayo Ulaya kuwaonyesha wazungu na kujipatia pesa lakini hakuna fungu lolote liloenda kwa mjane.

Cc: chama

weka ushahidi kuhusiana na cdm kujipatia pesa kwa kutumia picha za mauaji ya mwangosi .
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom