Hapana watu wengi wamechukizwa sana
Khaa!! wewe vipi bana? mie nazungumzia mtaani kwetu siyo huko kwenu :crazy:Jamaa muongo sana, yaani huku mtaani watu wengi ni kama wako kwenye msiba, na wengi wamekata tamaa kabisa ya kupiga kura tena, maishani mwao!! Wanasema bila kupatikana tume huru ya uchaguzi, bora pasiwe na uchaguzi tu, iwe kama china wawe wanapokezana tu wao kuliko kusumbua watu.
Unaujua msemo wa "KULA CHADEMA KULALA CCM" hiyo ndio siasa welcome 2 the real worldNimeshangaa sana,
Zaidi ya nusu ya vijana wa bodaboda waliokuwa wakipeperusha bendera ya CDM huku wakirandaranda mitaani leo wanafanya hivyohivyo huku wakiwa na bendera ya ccm.
Kina dada wote kwenye hii bar ya jirani waliokuwa wanashinda na vilemba na mitandio yenye rangi ya cdm hata wakati wajua kali, leo ndiyo hawa wanakata mauno hapa wakiwa na nguo zenye rangi za ccm!!
Huyu mangi jirani yangu ambaye kila ukienda dukani kwake haachi kukukumbusha juu ya mabadiliko leo anasema kidogo tupotee njia!!!
Watu wa hovyo sana hawa!!