Mara
nyingi nimekua nikiamini kwamba yale tunayoyafahamu kuhusu maisha ni
machache sana ukilinganisha na yale tusioyafahamu. Kiasi cha miezi
kadhaa iliyopita nilisoma utafiti fulani kuhusu hedhi. Awali nilipousoma
niliona ni hadithi tupu. Lakini nilipoona ni vyema kuujaribu kwa
kutenda miezi minne baadae nilishangaa. Hata wewe najua utashangaa
utakaposoma makala haya. Lakini ombi langu kwako ni kukutaka ujaribu
kufanya mazoezi ili uthibitishe ukweli huo.
Miaka ya hivi karibuni imegundulika kwamba hata wanaume hupata
hedhi-ingawa wanaume hawana alama za nje za kuwaonesha kwamba wako
kwenye hedhi, kama walivyo wanawake ambao hutoka damu siku zao za hedhi
zinapofika na kukamilika.
Kwa karne na karne hakuna mtu aliyekuwa akifikiria kwamba wanaume
wangeweza kuwa wanapata nao hedhi kama wanawake. Kama mwanaume akiamua
kuweka kumbukumbu zake kwenye dayari na kujiangalia kila siku hali yake
inavyobadilikana kuwa ya kusikitika, ya kawaida, furaha na
hasira akiifuatilia hali yake namna hiyo kwa siku zote 28 za mwezi,
halafu na mwezi unaofuata, akafanya hivyo hivyo, halafu mwezi wa tatu
nao akatenda hivyo, na halafu ailinganishe miezi hiyo mitatu atashangaa.
Kuna siku tatu, nne au tano ambazo zitafanana katika dayari zote tatu,
lini ana hasira ana masikitiko, ni mharibifu, na tabia nyingine kama
hizo. Hivyo ndivyo vipindi vya hedhi kwa wanaume kama ilivyo kwa
wanawake. Zoezi hili anaweza kufanya mwanaume yeyote, akishindwa kupata
matokeo anaweza kuwasiliana na mimi na kuuliza ni kwa nini nimeandika
uongo.
Ni jambo ambalo lipo na limeshafanyiwa tafiti mbalimbali, hata mimi
binafsi nimefanya zoezi hilo kwa miezi minne na limetoa majibu kama
hayo. Kwa kawaida mwanaume hana dalili za kimwili za kutoka damu kama
mwanamke ndio maana, karne na karne hakuna mtu aliyejali lakini ni
jambo la uhakika kwamba wanaume wanapata hedhi.
Dalili za mwanaume aliye kwenye hedhi ziko akilini zaidi na sababu ziko
wazi: mwanamke asili yake ni kimwili zaidi, kihisia zaidi, na mwanaume
ana asili ya ubongo zaidi. Lakini mwanaume anapata usumbufu ule ule
anaopata mwanamke anapokuwa kwenye hedhi. Tofauti ni moja tu, kwamba
mwanaume hatoki damu. Lakini kila mwezi, baada ya siku 28, hali fulani
ya kiakili na kihisia itakuwa inajirudia.
Na kama umejaribu kujichunguza kwa mwaka mzima, utashangaa kwamba,
ulikuwa na hasira mgomvi, mwenye huzuni na vingine vya aina hiyo, si
hivihivi tu bali ni kwa sababu ulikuwa kwenye hedhi. Kama ukishafanya
zoezi nililokwambia la dayari, jiulize, kama ulipokuwa kwenye hali hizo
ulikuwa umekerwa na yeyote au chochote. Utagundua kwamba hukuwa umekerwa
bali ulikuwa unasumbuliwa na hedhi yako.
Mwanaume na mwanamke wameumbwa kwa matofali yaleyale, kwa maumbile
yaleyale na baiolojia ileile. Tofauti yao ni kwamba mwanaume ni chanya
na mwanamke ni hasi kama tungekuwa tunazungumzia umeme. Huwezi kupata
umeme kwa kuwa na chanya mbili; wala ukitumia hasi mbili bali
ukichanganya chanya na hisi. Hivyo, kama mwanamke anapata hedhi kama
hatua muhimu kuelekea mwito wa kimaumbile, haiwezekani mwanaume asipitie
hatua hiyo, ingawa kwa uchanya wake.
Kupata hedhi kwa mwanamke inaeleweka kwamba, ni kutokana na wito wa
kimwili. Maana yake ni kwamba, alikuwa amefikia hatua ambapo kimaumbile
alitakiwa kujamiiana ili apate ujauzito. Je, kama hakuna mabadiliko kwa
mwanaume, itawezekana vipi mwanaume kujamiiana na mkewe ambaye yuko
kwenye hitaji hili la kimaumbile?
Ina maana basi kwamba mwanaume naye ni lazima kila mwezi awe na
mabadiliko ambayo yatamfanya aingie mahali ambapo atavutana na mwanamke
kimapenzi. Hili ni suala la maumbile ili kufanya kuzaliana kuwepo.
Utajuaje kuwa mwanaume ameingia kwenye hali hiyo? Ndiyo pale ambapo
wataalamu wamegundua hizo siku nne au tano za mabadiliko ya kiakili kwa
mwanaume!
khaaaa!!we jamaa acha kabisa hyo kitu hapana mwanamume kuwa na hedhi,labuda wewe iko na jinsia mbili.