Kumbe sina kabila

Kumbe sina kabila

Mleta mada jaribu kusimama sehemu moja kutetea hoja zako, kama utatumia vitabu vya Mungu ijulikane Kama unajenga hoja Kwa wewe mwenyewe ijulikane!

Nilitaka Kusema machache; maendeleo siku zote huja na athari nyingi sana! Utaanza Leo kukataa Kabila na kesho utaishia kumtambua baba na mama tu katika familia yako na Hao wazaliwa wenzako Kwa wazazi wako! Na kesho utasema wewe ni mtanzania na si mwaafrica!

Haya mambo yako Kwa wenzetu huko! Mtu anajijua yeye tu km ni mjerumani ni mjerumani tu anashika kiasili chake Hicho tu! Hawezi sema yeye ni muulaya ata siku moja!

Haya maendeleo yana athari kubwa sana, na itafikia hatua maadili watu yataporomoka sana! Upendo kupingua, heshima, mavazi ya kutokujisitiri n.k

Umuhimu Wa asili Ni kutuweka pamoja na kutunza maadili!
 
Jitambue ndugu, unaweza ukawa na asili bila kabila. BINADAMU wa kwanza Adam alikua kabila gani?
KIMSINGI kama ni kabila basi wote tungekua na kabila lililotokana na yeye Adam.

Mkuu Ukisema binadamu tayari unawakilisha Kua sisi ni uzao Wa Adamu!

Na pia Ukitizama maandiko baada ya Adamu kukajakua Na makabila ktk huo uzao Wa Adamu!
Kwahiyo ukizama ktk maandiko utakuta makabila yamo! Kwahiyo ni wewe kuamua Unataka kutetea hoja yako Kwa maandiko Au?
 
Msimamo wangu sina kabila! Kwakua sioni umuhumimu wake!
Hakuna dini hata moja inayokuhoji kabila pindi unapotaka kuungana nao.
 
Mwulize mama yako vizuuuri mkiwa faragha atakuambia baba yako wa damu ni yupi na kabila lake. kabila la huyo mjanja ataketajwa na bi mkubwa ndio kabila lako.
 
Mwulize mama yako vizuuuri mkiwa faragha atakuambia baba yako wa damu ni yupi na kabila lake. kabila la huyo mjanja ataketajwa na bi mkubwa ndio kabila lako.
Hivi unachoona ajabu nini mtu kua hana kabila? Na ni kigezo kipi kinachotumika kwamba mtoto lazima afuate au awe kabila la baba?
 
Ktk maandiko hakuna makabila kuna uzao. Mfano wa Ibrahim, uzao a Ayuob,Uzao wa Nuhu n.k
swala la makabila halikupewa umuhimu kihivyo.
Na uzao hauna uhusiano wowote na muundo wa kabila. Rejea ktk kamusi ya kiswahili sanifu tafuta maana ya.
1.FAMILIA
2.UKOO
3.UZAO
4.KABILA
Kimsingi huwezi kuepuka kua na familia,ukoo na uzao.
Lakini unaweza kuepuka kua na KABILA kwakua hakuna chain yoyote inayounganisha ktk origin ya mtu.
 
Ktk maandiko hakuna makabila kuna uzao. Mfano wa Ibrahim, uzao a Ayuob,Uzao wa Nuhu n.k
swala la makabila halikupewa umuhimu kihivyo.
Na uzao hauna uhusiano wowote na muundo wa kabila. Rejea ktk kamusi ya kiswahili sanifu tafuta maana ya.
1.FAMILIA
2.UKOO
3.UZAO
4.KABILA
Kimsingi huwezi kuepuka kua na familia,ukoo na uzao.
Lakini unaweza kuepuka kua na KABILA kwakua hakuna chain yoyote inayounganisha ktk origin ya mtu.

Una uhakika juu ya maandiko Kua Hakuna makabila?
 
Bado hoja zako hazina mashiko! Leta hoja
1.Kipi kimekufanya uwe na kabila?
2.Nini faida unayopata ya kabila uliopo?
3.Weka wazi hasara za mtu atakazozipata pindi akiwa hana kabila?
Kabila ni Muhimu katika kukuunganisha na Wazazi au Ndugu zako wa asili
  • Umuhimu wa Kabila utauona hasa pale utakapotokewa na tukio Muhimu hasa katika maisha yako (Siombei na huenda limeshakutokea) hapo watu wote huwa wanakaa pembeni ilaai kuangalia MILA zako zinatakaje
  • Faida mojawapo ni msaada tu kwani hakuna kitu mtu atakiweza yeye peke yake na Mke
    • Mfano Harusi mwanao anaolewa na Wanyakyusa au Wasukuma, Huwezi kusanya marafikizako tena wawe mashabiki wa Mpira wa Man U au Simba wakampokee Mkwe na kudaiwa MKAJA Hao iwe Mkeo ni Mluguru ujue Mashemeji, (wajomba) watakunyang'anya Bint ili ujue umuhimu wa KABILA
  • HASARA utakayoipata utakapokosa Kabila ni pale utakapotengwa na marafiki zako ambao mnashinda nao Bar/Kilabuni hawatalala kwako wala kuhudhuria watakulazimisha mwende bar kwa Moja moto moja baridi na familia kuiacha
  • HASARA ya mwisho ni kuwa HUNA MAJUKUMU YA FAMILIA ukikua utakumbuka kabila, Utaifa, na DINI kuwa ni MUHIMU kwa Binadamu yeyote kabla HAJAFA labda UANAJUA hufi
 
Ktk maandiko hakuna makabila kuna uzao. Mfano wa Ibrahim, uzao a Ayuob,Uzao wa Nuhu n.k
swala la makabila halikupewa umuhimu kihivyo.
Na uzao hauna uhusiano wowote na muundo wa kabila. Rejea ktk kamusi ya kiswahili sanifu tafuta maana ya.
1.FAMILIA
2.UKOO
3.UZAO
4.KABILA
Kimsingi huwezi kuepuka kua na familia,ukoo na uzao.
Lakini unaweza kuepuka kua na KABILA kwakua hakuna chain yoyote inayounganisha ktk origin ya mtu.

Kasome vizuri Biblia, utayakuta Makabila 12 (Mwanzo 49:28)
Kuyainua Makabila ya Yakobo Isaya 49:6
Siku ya mwisho (ambayo wewe huiamini makmee) Makabila 12 yatayahukumu Makabila ya Israel Mathayo 19:28
Samahani kwa wasioamini juu ya Makabila mm nimenukuu km tulivyoelezewa na Maandiko
 
Last edited by a moderator:
Kabila ni Muhimu katika kukuunganisha na Wazazi au Ndugu zako wa asili
  • Umuhimu wa Kabila utauona hasa pale utakapotokewa na tukio Muhimu hasa katika maisha yako (Siombei na huenda limeshakutokea) hapo watu wote huwa wanakaa pembeni ilaai kuangalia MILA zako zinatakaje
  • Faida mojawapo ni msaada tu kwani hakuna kitu mtu atakiweza yeye peke yake na Mke
    • Mfano Harusi mwanao anaolewa na Wanyakyusa au Wasukuma, Huwezi kusanya marafikizako tena wawe mashabiki wa Mpira wa Man U au Simba wakampokee Mkwe na kudaiwa MKAJA Hao iwe Mkeo ni Mluguru ujue Mashemeji, (wajomba) watakunyang'anya Bint ili ujue umuhimu wa KABILA
  • HASARA utakayoipata utakapokosa Kabila ni pale utakapotengwa na marafiki zako ambao mnashinda nao Bar/Kilabuni hawatalala kwako wala kuhudhuria watakulazimisha mwende bar kwa Moja moto moja baridi na familia kuiacha
  • HASARA ya mwisho ni kuwa HUNA MAJUKUMU YA FAMILIA ukikua utakumbuka kabila, Utaifa, na DINI kuwa ni MUHIMU kwa Binadamu yeyote kabla HAJAFA labda UANAJUA hufi

Ndugu zangu wa asili naweza kuwatambua hata kama sina kabila kwasababu kinachotuunganisha ni ukoo si kabila.
 
Na hayo matukio muhimu iwe msiba,ndoa,n.k hayataendeshwa kikabila bali kwa utaratibu wa imani ya dini niaminiyo.
Wapi kabila litapata nafasi?
 
Wanajamvi!
Baada ya kutafakari kwa muda na kwa kina kuhusu makabila yote duniani. Nimeamua niwe sina kabila.hii ni kwasababu
1.Mwanadamu wa kwanza (ADAM) Ambae wanadamu wote tumetokana nae alikua hana kabila.

2.Kutokua na kabila kutaniweka huru na kashfa zote zinazoelekezwa kwa makabila ya hapa nchini,kama majivuno,ubishi,wizi,ubahiri n.k
3.Kutokua na kabila kutaniweka huru na tamaduni zote ambazo zimepitwa na wakati kama ukeketaji,nyumbantobo,kuoa ng'ombe 70 n.k
My take- sijaona faida hata 1 ya kabila nipo huru sasa karibu ujiunge nami.
uzuri wake ujavunja katiba ya tz tu..
 
Naungana nawewe mkuu ndio maana hata mimi niliona hakuna umuhimu wa kuwa na jina kwani linanisaidia nini? kunawakati ukiwaza zaidi inafikia mahali unakua huwazi tena kwa kua ushawaza sana na vyote utakavyoviwaza ulisha viwaza kabla ...lol.(zamani niliwahi kusikia eti mtu akisoma sana anakua chizi qwiqwiqwiqwiqwiiii)
 
Naungana nawewe mkuu ndio maana hata mimi niliona hakuna umuhimu wa kuwa na jina kwani linanisaidia nini? kunawakati ukiwaza zaidi inafikia mahali unakua huwazi tena kwa kua ushawaza sana na vyote utakavyoviwaza ulisha viwaza kabla ...lol.(zamani niliwahi kusikia eti mtu akisoma sana anakua chizi qwiqwiqwiqwiqwiiii)
Haa haaa kweli kaka!
Hivi jina lina faida gani zaidi ya kuitwa na kuitika?
 
Back
Top Bottom