Kumbe saidi mwema si lolote!

Arafat

JF-Expert Member
Nov 17, 2009
2,581
758
Nimesoma barua ya Saidi Mwema kwa Waandishi wa habari ya Januari 13, 2011 siamini kama ni Mbumbumbu kiasi hicho;

  • Hivi kweli Jeshi nyeti kama hilo linaweza kuongozwa na mtu hasiyejua hata ABC za Utawala wa Sheria na Ulinzi wa jamii na hata hajui kuandika barua! Ukiangalia kwa makini ile barua unashaanga, mi nimeona mapungufu nane makubwa yanayotilia shaka uwezo wa huyu Bwana saidi Mwema.
  • Barua haina sahihi wala jina la mtoa taarifa, haiwezi kuwa taarifa halali maana kila mtu anaweza kuikataa na kuikana mda wowote au imeandikwa na Makamba!! “A letter is nothing but the authorisation of its content and its context” hata barua za Elimu ya Msingi wanajua hilo.

  • Swala lipo mahakamani anatoa taarifa za kuchoche upande mmoja nje ya mahakama hivi huyu Saidi hajui kwamba swala lolote likiwa mahakamani halipaswi kutolewa katika vyombo vya habari kwa lengo la kuchochea ushahidi wa upande mmoja, na kama hajui anafanya nini kwenye ofisi ya Umma?

  • Anasema baada ya taarifa za kiintelijensia polisi iliamua kuzuia maandamano kwa mujibu wa sheria! Barua yoyote ya kitaalam ilipaswa kuainisha ni kwa mujibu wa sheria gani ya mwaka gani? na kifungu kipi? Kilimpa mamlaka ya kuzuia maandamano, siyo kuweka hewa kuwa alizuia kwa mujibu wa sheria!

  • Barua haitoi njia mbadala kwa wananchi waliotaka kwenda kwenda mkutano wangefika vipi kama hawaruhusiwi kuandamana ila mkutano unaruhusiwa, hii si karne ya Jeshi la Polisi kuendelea kuongwa na watu mbumbumbu, kama hakutaka maandamano na aliruhusu mkutano hao watu wangefika vipi kwenye maandamano na tayari wapo hapo Phillips wangepaa! Au aliwaperekea magari ya kupanda? Said tumia akili angalao kidogo!

  • Saidi anaendelea kutoa upupu, hati Kamati ya ulinzi na Usalama inaendelea na uchunguzi juu ya Viongozi wa chadema! Jamani au hiyo barua tuliyopewa JF siyo yake; hivi kamati ya ulinzi na Usalama ina mamlaka gani ya kufanya uchunguzi wa swala hilo huku mwenyekiti wake akiwa ni mkuu wa mkoa, ambaye ni Mjumbe na kada na moja wa CCM! Saidi umesoma ila hujaelimika hata kidogo, kumbe hili swala si la polisi ni huyu Mwema ndiye aliyeingiza Polisi katika swala la kamati ya ulinzi na usalama!!.

  • Kama bado kuna upelelezi tena unaofanywa kwa pamoja na kamati ya ulinzi na usalama kwanini ulikama vingozi wa CDM, au hujui kwamba Mpelelezi makini na Mwendesha Mshtaka wake umkamata mtuhumiwa mara baada ya Upelelezi kubaini ukweli na kukusanya ushahidi tathibiti juu ya tuhuma! Saidi hujui hilo na wewe ndio IGP! Kumbe wewe ni Mbumbumbu!! Nani atasaidia Polisi wa chini kujua kama nawe hujui?

  • Barua inaonyesha kibali cha maandamano kilitolewa January 03, 2011; iweje taarifa zako feki ulizo pokea Januari 04, 2011 useme ni taarifa za kiintelijensia za wiki moja? Au pia hujui kuwa 4-3=1? Hilo pia hujui! Kumbe wewe ni mbumbumbu? Kwanini husiseme taarifa ya kiintelijensia ya siku moja? Au unataka kusema mlitoa kibali mkiwa na taarifa hizo? Na kama ndivyo nani alikugeuza mawazo tena siku ya mwisho? Au ndio tuseme wewe unafanya kazi kwa maslahi ya Chama Fulani na ndio waliokutuma! Kama la nini sasa?

  • Unasema Mwanasheria mkuu wa serikali pia anashirikia nanyi kufanya Uchunguzi! Maajabu haya au unavyeti bandia? Sasa nani atakaye tetea raia katika mfumo wa sheria hapa Tanzania? Hujui kwamba hapaswi kufanya uchunguzi wa makosa ya jinai? “Checks and balance ya sheria ipo wapi hapo sasa ndini ya serikali?” Nakama hujui sheria waliyovunja mpaka uombe msaada wa Mwanasheria mkuu uoni kuwa hujui kazi yako?una subiri nini kujiuzulu!!

Jamani wana-JF Pitieni ile barua ya huyu jamaa siMWEMA haina aiba ya Kitaaluma hata kidogo, uthadhani imeandikwa na Mwanasiasa.
 
Mbona imekuchukua muda mrefu kiasi hicho kubaini umbumbumbu wa SM??? Amepewa cheo hicho kwa nguvu ya ushemeji na jk.
 
Back
Top Bottom