Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Kumbe purukushani zote za kujitawala lengo lilikuwa tuliusaka uhuru ili kuwa vibaraka wa wachina.
Hawana Facebook, Whatsup na Google basi hiyo ni sababu tosha ya kuwaiga
Hawana mfumo wa vyama vingi basi nasi ni kuigaiga tu huku tukidai kuhamia Dodoma ni kumuenzi "baba wa taifa" aliyeshauri kurejeshwa mfumo wa vyama vingi!
Wanapiga risasi watuhumiwa wa ufisadi basi nasi risasi kona kwa kona maana hata wachina wanapiga risasi.
Wanaikopesha serikali ya marekani basi nasi tuanze kuikopesha
Wachafuzi wakuu wa mazingira basi nasi kiguu kwa njia
Wamefuta ukomo wa Urais basi nasi ni copycats hatuna historia na urithi wowote hivyo ni kufuta ukomo wa Urais ili mmoja wetu na ndugu zake na wapambe zake waendelee kula na kusaza sis tuokote makombo yao tu kwani Mchina ndiye Mungu wetu na anapaswa kuabudiwa.
Wana chama chao tawala basi tufute vyama vyote vya siasa na kuwapigia magoti chama chao cha kikomunisti jina tu kishike "utamu" wa uongozi! Sijui ccm sijui cuf sijui wanamagwanda ni kuvifuta kwa kubadili katiba na sheria na kukitangaza chama tawala cha uchina ndicho pekee tawala hapa nchini!
Tusikomee hapo:-
Wanatawaliwa na wachina wenzao basi watumishi wote wa umma wajiuzulu kuanzia siku internet itazimwa na kuwakabidhi serikali wachina. Rais na baraza la mawaziri wachina, wakuu wa mikoa na wilaya wawe wachina, wabunge na madiwani wawe wachina. Tusiishie hapo tuendelee kutimua raia wote kwenye utumishi wa umma na kuwakabidhi wachina inji hii ya wagagagigikoko!
Kweli Akutukanaye hakuchagulii tusi.
Nionavyo
Ukiona kiongozi wa umma anachukia uwazi na hataki kuwajibika kwa umma JIULIZE haya ayafanyayo ni KWA MANUFAA YA NANI?
Hawana Facebook, Whatsup na Google basi hiyo ni sababu tosha ya kuwaiga
Hawana mfumo wa vyama vingi basi nasi ni kuigaiga tu huku tukidai kuhamia Dodoma ni kumuenzi "baba wa taifa" aliyeshauri kurejeshwa mfumo wa vyama vingi!
Wanapiga risasi watuhumiwa wa ufisadi basi nasi risasi kona kwa kona maana hata wachina wanapiga risasi.
Wanaikopesha serikali ya marekani basi nasi tuanze kuikopesha
Wachafuzi wakuu wa mazingira basi nasi kiguu kwa njia
Wamefuta ukomo wa Urais basi nasi ni copycats hatuna historia na urithi wowote hivyo ni kufuta ukomo wa Urais ili mmoja wetu na ndugu zake na wapambe zake waendelee kula na kusaza sis tuokote makombo yao tu kwani Mchina ndiye Mungu wetu na anapaswa kuabudiwa.
Wana chama chao tawala basi tufute vyama vyote vya siasa na kuwapigia magoti chama chao cha kikomunisti jina tu kishike "utamu" wa uongozi! Sijui ccm sijui cuf sijui wanamagwanda ni kuvifuta kwa kubadili katiba na sheria na kukitangaza chama tawala cha uchina ndicho pekee tawala hapa nchini!
Tusikomee hapo:-
Wanatawaliwa na wachina wenzao basi watumishi wote wa umma wajiuzulu kuanzia siku internet itazimwa na kuwakabidhi serikali wachina. Rais na baraza la mawaziri wachina, wakuu wa mikoa na wilaya wawe wachina, wabunge na madiwani wawe wachina. Tusiishie hapo tuendelee kutimua raia wote kwenye utumishi wa umma na kuwakabidhi wachina inji hii ya wagagagigikoko!
Kweli Akutukanaye hakuchagulii tusi.
Nionavyo
Ukiona kiongozi wa umma anachukia uwazi na hataki kuwajibika kwa umma JIULIZE haya ayafanyayo ni KWA MANUFAA YA NANI?