Kumbe Puma Energy ni kampuni ya Serikali!

Kumbe Puma Energy ni kampuni ya Serikali!

CCM mpaka leo hujui kama serikali ina hisa na siyo mmiliki mkuu halafu unapongeza serikali ya awamu ya 5 kwa lipi ?
Shuleni mlienda kusugua madawati
 
Total wanaangalia ni faida tu kwa Nini wasafirishe mafuta ghafi uarabuni au ulaya yakasafishwe huko halafu yarudi Tanzania wakiuza wapate faida ndogo wakati yangesafishwa Tanzania jirani faida inakuwa kubwa kuliko kusafirisha mafuta gafi? Ujue huko wanakopeleka hawana kiwanda cha kusafisha mafuta ni vya kampuni zingine .sasa hapa kama kuna kiwanda shida ya nini waweza safisha mafuta yote Tanzania kiwanda cha tipper kisha wakasafirisha nje yasiyosafishwa au kuuza Ndani issue ni kuwa whatever method they use mwisho wa siku iwe kupitia Tipper Total au Puma tutavuna pesa

Ulileta jibu la kishabiki pale juu, kwa bahati mbaya umepatikana kwa kuambiwa Total iko hapa nchini siku nyingi. Imebidi akili ikurudie na kupanga jibu la kulazimisha na sio lile la mahaba niue. Halafu una uhakika gani Total watapeleka hayo mafuta yote hapo Tipper? je una taarifa sahihi za kiwango cha mafuta yatokayo Uganda kwa siku na uwezo wa Tipper kusafisha mafuta? Acha maelezo ya kishabiki hapa jukwaani maana watu wanaulewa mpana, wewe ngoja huko vijijini ambako watu hawana uelewa wa mambo mkawaeleze habari ya bomba la mafuta ya Uganda, wadhani ni bomba la pamoja la Uganda na Tanzania kitu ambacho sio kweli. Ukweli hiyo kampuni ya Puma sio wengi wanajua kwamba serekali ina hisa humo ndani. Au ndio hayo mambo ya mikataba ya siri kisha likibumburuka watu wakasema mnasema sio wazalendo?
 
Martin George PUNGUZA UVIVU WA KUJUA MAMBO MKUU

INA MAANA WEWE HUJUI HATA MAKAMPUNI GANI YANAMILIKIWA NA SERIKALI

TENA INAONEKANA HISTORIA YA UBINAFSISHAJI HUJUI HATA CHEMBE.. CHEE..
 
Mkuu usiumize kichwa chadema original wenye akili wa Ndani na nje ya nchi waliondoka na Slaa hawa waliopo wengi wanywa viroba vilivyopigwa marufuku, konyagi na gongo usipoteze muda wako

Kama wewe sio mnafiki onyesha post uliyowahi kumsifia Slaa wakati anamuita Kikwete ni fisadi, au ukimtetea wakati anaitwa padre mzinzi na mropokaji. Au ndio hayo hayo ya sifa za marehemu?
 
Mkuu usiumize kichwa chadema original wenye akili wa Ndani na nje ya nchi waliondoka na Slaa hawa waliopo wengi wanywa viroba vilivyopigwa marufuku, konyagi na gongo usipoteze muda wako
Kweli kabisa mkuu. Dr. Slaa aliondoka na Chadema wote wenye akili na wengi waliachana na maswala ya siasa.

Kama kipindi kile zile ndege za Bombardier zinakuja apa Tanzania, manyumbu wengi walitokwa na povu na kusema ndege mbovu ndio maana zinamwagiwa maji kumbe ni desturi ya ndege kumwagiwa maji. Eti ndege zimechemsha kutoka Canada mpaka Tanzania
 
Vitu vibaya vinatofautiana.Slaa na chadema yake aliyokuwa nayo pamoja Na kua ilikuwa mbaya sio sawa na hii iliypo hii ni worse kuilinganisha na Ya Slaa ni kumdhalilisha mzee wa watu

Ndio nasema weka post yoyote ya wakati huo uliyoonyesha kwamba wangalau ulikubaliana na baadhi ya siasa zake. Kinyume na hapo ww ni mnafiki na kinachokufanya ulieulie hapa ulidhani Magu ni malaika, sasa anapewa kubwa yake ndio unakimbilia kumtaja Slaa kama kinga ya huu ukweli.
 
Kama ulikuwa hujui now you do... Serikali ina hisa tu Puma energy ni kampuni binafsi ya nje ilinunua hisa za BP but serikali imeizidi puma kwa hisa so serikali wanahaki ya kuongoza management kwa ushirikiano.. BP aliuza hisa kipindi cha uchakachuaji wa mafuta biashara ikawa ngumu na Bp peke yake ndie alikuwa na mafuta bora tena meupe bila chenga ndio kimbilio kubwa na baada ya serikali kupangia bei mafuta BP wakamwaga mchezo kwani utaratibu wa waingereza ni no ubabaishaji na pay yao ni kubwa kujali mfanyakazi na mteja
 
Kiukweli hili nilikuwa sijui kama Puma Energy inamilikiwa na serikali kwa namna yeyote ile. Ahsante sana serikali ya awamu ya 5!

..serikali kuwa na hisa Puma Energy siyo habari mpya.

..Bodi ya wakurugenzi inayoondoka iliteuliwa na JK na Prof.Muhongo mwaka 2014.

..soma taarifa ya serikali kwa umma hapa chini.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA NISHATI NA MADINI


Simu: +255 22 2117156-9
Nukushi: +255 22 2111749

Barua pepe: ps@mem.go.tz

Unapojibu tafadhali taja:

nembo
754/33 MTAA WA SAMORA,

S. L. P. 2000,

DAR ES SALAAM.



TAARIFA YA UMMA

UTEUZI WA MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI YA PUMA ENERGY (T) LTD NA WAKURUGENZI WA BODI


Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amemteua Dkt. Ben E. Moshi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya PUMA Energy (zamani ilijulikana kama BP Ltd). Uteuzi huo wa Dkt. Ben Moshi ni wa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 1 Machi, 2014.

Kutokana na uteuzi huo Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter M. Muhongo (Mb.) amewateua wafuatao, kuwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya PUMA Energy (T) Ltd kwa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 1 Machi, 2014:

Mhandisi Dkt. Malima MP. Bundara, Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha GARETRACE;
Bw. Solomon R.M. Odunga; Katibu Mkuu Mstaafu;
Bw. James Andilile, Kamishna Msaidizi wa Nishati katika Wizara ya Nishati na Madini; na
Bw. Daniel N. Nsanzugwanko, Mtaalam Mshauri wa masuala ya biashara.
Imetolewa na

KATIBU MKUU
 
..serikali kuwa na hisa Puma Energy siyo habari mpya.

..Bodi ya wakurugenzi inayoondoka iliteuliwa na JK na Prof.Muhongo mwaka 2014.

..soma taarifa ya serikali kwa umma hapa chini.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA NISHATI NA MADINI


Simu: +255 22 2117156-9
Nukushi: +255 22 2111749

Barua pepe: ps@mem.go.tz

Unapojibu tafadhali taja:

nembo
754/33 MTAA WA SAMORA,

S. L. P. 2000,

DAR ES SALAAM.



TAARIFA YA UMMA

UTEUZI WA MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI YA PUMA ENERGY (T) LTD NA WAKURUGENZI WA BODI


Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amemteua Dkt. Ben E. Moshi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya PUMA Energy (zamani ilijulikana kama BP Ltd). Uteuzi huo wa Dkt. Ben Moshi ni wa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 1 Machi, 2014.

Kutokana na uteuzi huo Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter M. Muhongo (Mb.) amewateua wafuatao, kuwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya PUMA Energy (T) Ltd kwa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 1 Machi, 2014:

Mhandisi Dkt. Malima MP. Bundara, Mwenyekiti Mtendaji wa Kituo cha GARETRACE;
Bw. Solomon R.M. Odunga; Katibu Mkuu Mstaafu;
Bw. James Andilile, Kamishna Msaidizi wa Nishati katika Wizara ya Nishati na Madini; na
Bw. Daniel N. Nsanzugwanko, Mtaalam Mshauri wa masuala ya biashara.
Imetolewa na

KATIBU MKUU
Ahsante mkuu kwa rejea ya uhakika kabisa!
 
Kiukweli hili nilikuwa sijui kama Puma Energy inamilikiwa na serikali kwa namna yeyote ile. Ahsante sana serikali ya awamu ya 5!
Puma Energy imekuwa hivyo hata kabla ya serikali ya awamu ya 5 kuingia madarakani-fanya utafiti kwanza kabla ya kuandika
 
Puma Energy imekuwa hivyo hata kabla ya serikali ya awamu ya 5 kuingia madarakani-fanya utafiti kwanza kabla ya kuandika
Mkuu hata kuja kwangu hapa Jf ni sehemu ya utafiti, au wewe unaamini jf ni ya wanamipasho tu!
 
Hapa ndo unapogundua kuwa watz wengi kuhusu maswala ya uchumi na biashara ni weupe!! kichwani!!

sasa hapa makosa yanaweza yakawa pande zote mbili,

Serikali kwa maana ya mikataba wanayoingia nayo wanaweka siri au uvivu watz kusoma na kujua tz ikoje wapi tulipo na wapi tunaenda kama tunalivyo kawaida yetu kusoma hatusomi.

Lakini ukiweka mambo ya siasa kila mtu anajua.
 
Puma Energy - Wikipedia

161594445a0e677bcb26038470e1be39.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukijileta na maana yako bila ya kujua mwenzio kamaanisha nini,abadani huambiwi unaachwa ujifanye unajua kumbe unaungua jua.
Bado hujanijibu swali nililokuuliza..! kwasababu nimeuliza maana nikiwa siijui sio kwamba nimekuja na maana yangu.
 
Back
Top Bottom