Kumbe polisi wa usalama barabarani wanawekewa malengo ya kutoza ushuru!

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Ama kweli hii ni ya aina yake. Leo nikiwa njiani mara nikaona konda wa daladala akijibishana vilivyo na askari wa usalama barabarani nusura kushikana mashati.

Nikasogea karibu kuona kinachojiri. Hapo ndo nikamsikia yule konda wa daladala akilalamika kuwa yule askari polisi aliyemkamata na kumpa kile kirisiti cha TRA anamuonea kwani jana jumamosi alikamatwa kwa kosa hilohilo na kupewa kirisiti cha TRA! Kwa jumla amesema kuwa leo na jana ametozwa shilingi (T) 60000 yani kila siku shilingi (T) 30000

Nilipomuuliza yule konda kwani kosa hasa ni lipi hapo ndipo nikastaajabu! Kosa lenyewe ni gari kutoa moshi! Eti gari inatoa moshi kupita kiasi!

Mbaya zaidi yule askari polisi akawa anasema kuwa malengo aliyopewa na boss wake ni lazima yatimie! Hapa sisemi! Nikisema huwa naonekana mpinga Maendeleo!

Kama haya ndo mapato TRA wanayosema kuwa wamevuka lengo kila wakija kwa waandishi wa habari basi huu ni uonevu wa dhahiri!

Magari mengi hasa ya serikali ni chakavu hilo halina ubishi! Mbaya zaidi magari haya ya serikali ni chakavu kusiko kawaida! Nenda kaangalie magari ya wakurugenzi wa taasisi mbalimbali uone! Haya huwa hayatozwi ushuru kwani serikali tukufu itajipunja mapato na kushindwa kufikia malengo na kuyavuka!

Kwa barabarani serikali inakamua vilivyo na mbaya zaidi yule polisi ni vigumu sana kukukosa na kosa.

Kila lakheri!!
 
Kama huo ni ukweli basi wahujumu u humi ni wenye meno nchi hii. Kumbe ndiyo maana ni wakati sana na wanakimbilia kimashine wakikukamata tu ili kukuchomoa hata za uongo. Siku moja niko na mkweche wangu akanizuia dada mmoja askari akakagua kila kitu akaona vikao sawa. A kaja kwenye wipers akakuta ziko sawa a kasema fungulia maji ya wiper hayakuwepo basi akaniandikia haraka. ...Unaweza kuona nchi ya ajabu magari yanayoweza kusababisha ajali hayaguswi bali wanatafuta maji ya wiper ya gari ili kukusanya Malengo waliyowekewa
 
G Sam ni kweli polisi sasa hivi wamekuwa wanalazimisha makosa ili wakufaini, Tafadhali magufuli tunaomba utusaidie, jana nimepewa kosa ambalo silielewi mtu hajafunga mkanda yuko siti ya nyuma naambiwa dereva ndio alipe fine. Sasa nimeangalia Traffic Act sijaona mahali natakiwa dereva nilipe fine kwa kosa la abiria. Isitoshe nimemwambia afunge mkanda sasa tena naambiwa kosa langu.
 
Kama kuna anadhani anaonewa na police asilipe aende mahakamani ili kama anaonewa au vinginevyo ijulikane

Mahakamani kwa fine ya 30,000 halafu kesi karani aipige kalenda miezi, unategemea mtu anapata haki yake. Unapoteza pesa nyingi kwa ajili ya kuokoa 30,000. Kimsingi polisi kuna idara ya maadili ichunguze madai haya ama sivyo wananchi watakuwa wanabambikiziwa makosa pasina sababu ya msingi. Hilo pia linachochea mazingira ya rushwa.
 
Ni kweli ....kuna siku walinikamata kuwa nimeendesha zaidi ya km 80 kwa saa sehemu ambayo sipaswi kuvuka 60 kitu ambacho hakikuwa kweli lakini traffic yule hakutaka mjadala zaidi ya kunionesha gari alilopiga picha huku hata namba za gari hazionekani ....nikaamua kulipa faini sababu sikuwa na muda wa kujibizana.....haikupita wiki wakamkamata raia mmoja wa kigeni kwa staili ile ile ....yule raia akalipa then akaenda kituo cha polisi na risiti pamoja na gari lililokamatwa ....akaomba aoneshwe rekodi ile maana aliwahakikishia lile gari la kwenye picha ya kamera si lake yamefanana tu .....baada ya mabishano wakakubali kupitia hizo picha ....ikagundulika ile gari iliyofanya apigwe faini si yake ...yamefanana tu ....wakambembeleza wamrudishie cash yaishe ...jamaa akakataa akasema alitaka kuwaonesha kuwa wanachofanya kwa wananchi si sawa .....
 
Askari traffic wadogo wanapangiwa target za makusanyo na wakubwa wao ....ukiongea nao pembeni wanakiri hivyo .....wanaokosea wawajibishwe na si kulazimisha makosa ili ufikie lengo ulilopangiwa .....
 
Ni kweli ....kuna siku walinikamata kuwa nimeendesha zaidi ya km 80 kwa saa sehemu ambayo sipaswi kuvuka 60 kitu ambacho hakikuwa kweli lakini traffic yule hakutaka mjadala zaidi ya kunionesha gari alilopiga picha huku hata namba za gari hazionekani ....nikaamua kulipa faini sababu sikuwa na muda wa kujibizana.....haikupita wiki wakamkamata raia mmoja wa kigeni kwa staili ile ile ....yule raia akalipa then akaenda kituo cha polisi na risiti pamoja na gari lililokamatwa ....akaomba aoneshwe rekodi ile maana aliwahakikishia lile gari la kwenye picha ya kamera si lake yamefanana tu .....baada ya mabishano wakakubali kupitia hizo picha ....ikagundulika ile gari iliyofanya apigwe faini si yake ...yamefanana tu ....wakambembeleza wamrudishie cash yaishe ...jamaa akakataa akasema alitaka kuwaonesha kuwa wanachofanya kwa wananchi si sawa .....
Hili ni tatizo kwa kweli!
 
QUOTE="G Sam, post: 15994988, member: 137610"]Ama kweli hii ni ya aina yake. Leo nikiwa njiani mara nikaona konda wa daladala akijibishana vilivyo na askari wa usalama barabarani nusura kushikana mashati.

Nikasogea karibu kuona kinachojiri. Hapo ndo nikamsikia yule konda wa daladala akilalamika kuwa yule askari polisi aliyemkamata na kumpa kile kirisiti cha TRA anamuonea kwani jana jumamosi alikamatwa kwa kosa hilohilo na kupewa kirisiti cha TRA! Kwa jumla amesema kuwa leo na jana ametozwa shilingi (T) 60000 yani kila siku shilingi (T) 30000

Nilipomuuliza yule konda kwani kosa hasa ni lipi hapo ndipo nikastaajabu! Kosa lenyewe ni gari kutoa moshi! Eti gari inatoa moshi kupita kiasi!

Mbaya zaidi yule askari polisi akawa anasema kuwa malengo aliyopewa na boss wake ni lazima yatimie! Hapa sisemi! Nikisema huwa naonekana mpinga Maendeleo!

Kama haya ndo mapato TRA wanayosema kuwa wamevuka lengo kila wakija kwa waandishi wa habari basi huu ni uonevu wa dhahiri!

Magari mengi hasa ya serikali ni chakavu hilo halina ubishi! Mbaya zaidi magari haya ya serikali ni chakavu kusiko kawaida! Nenda kaangalie magari ya wakurugenzi wa taasisi mbalimbali uone! Haya huwa hayatozwi ushuru kwani serikali tukufu itajipunja mapato na kushindwa kufikia malengo na kuyavuka!

Kwa barabarani serikali inakamua vilivyo na mbaya zaidi yule polisi ni vigumu sana kukukosa na kosa.

Kila lakheri!![/QUOTE]
Hilo lipo angalia jinsi wanavyosumbua vi pickup vya mizigo, wakishaona Una mzigo kwenye gari, unatafutiwa kosa na kupewa faini, mtumbua majipu Hilo halioni
 
Mahakamani kwa fine ya 30,000 halafu kesi karani aipige kalenda miezi, unategemea mtu anapata haki yake. Unapoteza pesa nyingi kwa ajili ya kuokoa 30,000. Kimsingi polisi kuna idara ya maadili ichunguze madai haya ama sivyo wananchi watakuwa wanabambikiziwa makosa pasina sababu ya msingi. Hilo pia linachochea mazingira ya rushwa.
Kama kuna mtu anaamini kaonewa apeleke malalamiko yake huko basi na asiishie hapa JF tu
 
Ama kweli hii ni ya aina yake. Leo nikiwa njiani mara nikaona konda wa daladala akijibishana vilivyo na askari wa usalama barabarani nusura kushikana mashati.

Nikasogea karibu kuona kinachojiri. Hapo ndo nikamsikia yule konda wa daladala akilalamika kuwa yule askari polisi aliyemkamata na kumpa kile kirisiti cha TRA anamuonea kwani jana jumamosi alikamatwa kwa kosa hilohilo na kupewa kirisiti cha TRA! Kwa jumla amesema kuwa leo na jana ametozwa shilingi (T) 60000 yani kila siku shilingi (T) 30000

Nilipomuuliza yule konda kwani kosa hasa ni lipi hapo ndipo nikastaajabu! Kosa lenyewe ni gari kutoa moshi! Eti gari inatoa moshi kupita kiasi!

Mbaya zaidi yule askari polisi akawa anasema kuwa malengo aliyopewa na boss wake ni lazima yatimie! Hapa sisemi! Nikisema huwa naonekana mpinga Maendeleo!

Kama haya ndo mapato TRA wanayosema kuwa wamevuka lengo kila wakija kwa waandishi wa habari basi huu ni uonevu wa dhahiri!

Magari mengi hasa ya serikali ni chakavu hilo halina ubishi! Mbaya zaidi magari haya ya serikali ni chakavu kusiko kawaida! Nenda kaangalie magari ya wakurugenzi wa taasisi mbalimbali uone! Haya huwa hayatozwi ushuru kwani serikali tukufu itajipunja mapato na kushindwa kufikia malengo na kuyavuka!

Kwa barabarani serikali inakamua vilivyo na mbaya zaidi yule polisi ni vigumu sana kukukosa na kosa.

Kila lakheri!!

hadithi yako inatufundisha nini...
 
Kama huo ni ukweli basi wahujumu u humi ni wenye meno nchi hii. Kumbe ndiyo maana ni wakati sana na wanakimbilia kimashine wakikukamata tu ili kukuchomoa hata za uongo. Siku moja niko na mkweche wangu akanizuia dada mmoja askari akakagua kila kitu akaona vikao sawa. A kaja kwenye wipers akakuta ziko sawa a kasema fungulia maji ya wiper hayakuwepo basi akaniandikia haraka. ...Unaweza kuona nchi ya ajabu magari yanayoweza kusababisha ajali hayaguswi bali wanatafuta maji ya wiper ya gari ili kukusanya Malengo waliyowekewa
nchi zote ndugu yangu wanafanya hivyo. bila kuwapa malengo utapimaje ufanisi. ni kama ukiwa na taxi au daladala huwezi kumuacha dereva bila kumpa kiwango.
Na kama unataka kujua jinsi ya kuweka hiyo hesabu wala si jambo gumu, ni statistical data zitakuambia kwa KAWAIDA watu wangapi wanavunja sheria kwa siku.
 
Back
Top Bottom