Njowepo
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 9,710
- 2,226
Mkataba mwingine kama wa Dowans huu hapa!
Na Gerald Kitabu
31st July 2011
Ni ule mwekezaji aliyepewa ardhi kwa miaka 99
Kodi ya ardhi sh. 200, Halmashauri kupata sh.500
Diwani wa kata ya Litapunga, Godfrey Lusambo (kulia) akiwa na viongozi wa serikali ya mtaa na wanakijiji cha Kambuzi Halt, Katumba, wilaya ya Mpanda, wakilalamika kwa watafiti wa Shirika la Haki Ardhi na waandishi wa habari.
Wananchi, watendaji wa vijiji na Madiwani wa kata za Litapunga na Mishamo Wilayani Mpanda, Mkoa mpya wa Katavi, wamepinga yaliyokuwa makazi ya wakimbizi ya Mishamo na Katumba, kukodishwa kwa mwekezaji ambaye ni kampuni ya Agriosol ya Marekani, kwa maelezo kwamba uwekezaji huo, hautakuwa na tija kwa taifa.
Makubaliano ya awali (ambayo NIPASHE inayo nakala yake), kati ya mwekezaji huyo na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, yanaonyesha kwamba kampuni ya Agrisol itakodisha kwa miaka 99, eneo la Katumba hekta 80,317 na Mishamo hekta 219,800.
Mwekezaji pia atalipa Sh. 200 kama kodi ya ardhi kwa ekari na Halmashauri itapata Sh. 500 kwa ekari, hata hivyo haijulikani malipo hayo yatalipwa kwa muda gani yaani kwa mwezi au kwa mwaka.
Makubaliano hayo yanaonyesha pia kwamba iwapo kutatokea mgogoro, serikali itatumia busara kuutatua lakini ikishindikana, shauri hilo litasikilizwa jijini London, Uingereza na msuluhishi ambaye atakuwa Chemba ya Biashara ya Kimataifa (International Chamber of Commerce).
Kadhalika, inaelezwa kwamba mwekezaji huyo ataajiri mameneja wa mashamba kutoka nje hususan Afrika Kusini na ataendesha kilimo cha mbegu za kimaabara.
Hata hivyo, baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo Mawaziri na wale wa Halmashauri ya Mpanda, wamekuwa 'wakipigia debe' uwekezaji huo, kwa madai kwamba utaongeza uzalishaji wa chakula na kuongeza ajira kwa Watanzania.
WANANCHI
Watendaji wa vijiji na Kata zinazozunguka maeneo hayo, wamepinga uwekezaji huo kwa maelezo kwamba hawajashirikishwa kikamilifu na hati hiyo haina maslahi kwa taifa.
Wakizungumza na waandishi wa habari walioongozana na timu ya watafiti kutoka shirika la HakiArdhi kuhusiana na uwekezaji huo, viongozi hao na wananchi wameitaka serikali ijifunze kwa yaliyotokea kwa kampuni tata ya Dowans kwa kujifunga na mikataba mibovu, ya muda mrefu kwa bei chee.
Mwekezaji pia anaitaka serikali ibadili sheria ili kuruhusu kilimo cha vinasaba (Genetically Modified Crops), ambacho kimsingi kinaua mbegu za asili na kudhoofisha ardhi.
Diwani wa kata ya Litapunga, Godfrey Lusambo, alisema madiwani wa kata zinazozunguka eneo hilo, hawakuwahi hakualikwa kwenye mikutano iliyopitisha makubaliano hayo tata wala kwenda kwenye ziara nchini Marekani.
Viongozi wa wilaya wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Wenyeviti wa kamati na Madiwani wa kutoka mbali na hapa kama vile Mpimbwe na Ulwila ndio waliokwenda Iowa- Marekani na waliporudi tu sisi tukawa tunaletewa maagizo bila kujua undani wake, alisema.
Msafara wa wajumbe kumi waliokwenda Iowa-Marekani uliongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Salum Chima, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Rajabu Rutenge, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpanda, Philip Kalyalya, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpanda Silvester Nswima, Mkurugenzi wa Wilaya Eng. Emmanuel Kalobelo, Mjumbe wa kamati ya fedha Rose Mayaya, na Mjumbe wa Kamati ya maadili Teddy Nyambo.
Wengine ni Mwanasheria wa Halmashauri Patrick Mwakyusa, Afisa Kilimo na Mifugo Fabian Kashindye, na Haruna Mwakitanile (cheo hakikuweza kupatikana mara moja).
Alisema wajumbe hao waliporudi kutoka Marekani, wananchi walishangazwa na kitendo cha Serikali kutenga mipaka kwa ajili ya mwekezaji wakati vijiji hivyo havijawahi kupimwa.
Ofisa Mtendaji wa kata ya Mishamo, Agustino wanga, alisema hawajawahi kuiona kampuni ya AgriSol wala wawakilishi wao ambao ni Agrisol Tanzania Limited, na kwamba wamekuwa wakiwasikia viongozi wakieleza kuwa makazi hayo ya wakimbizi yatakodishwa kwa Wamarekani kwa miaka 99.
Mimi binafsi nina mpango wa kuhama kabisa maana wakiondoka wakimbizi tu, huduma muhimu nazo zitakoma, hatuwezi kuwezana na mwekezaji ambaye hatumjui, alisema.
Kwa upande wake, Katibu wa jumuiya ya wafugaji mkoani Rukwa, Masanja Katambi, alisema inashangaza kuona serikali inaingia mkataba usio na maslahi kwa taifa badala ya kuwapatia wafugaji maeneo hayo ambao wamekuwa wakigombea malisho na wakulima.
Kila siku wafugaji wanagombana na wakulima na mara nyingine kuuana, kwa sababu ardhi haitoshi katika mkoa wetu. Wafugaji hudiriki hata kuwahonga askari wa wanyamapori katika mbuga ya Katavi ili kuingiza mifugo yao kwa malipo maalumu, hili Serikali hailioni? alisema.
Mkuu wa Makazi ya Katumba na Mishamo, Athuman Igwe, alisema anachosubiri ni kutekeleza amri ya serikali pindi taratibu za uwekezaji zitakapokamilika.
Hata hivyo, alisema wakimbizi walipaswa kuwa wameondoka kupisha uwekezaji lakini anashangaa kuona kuwa bado zoezi hilo halijakamilika mpaka hivi sasa.
Hili Zoezi la kuwahamisha wakimbizi linaratibiwa na Tamisemi, sisi tunasubiri utekelezaji tu, alisema mkuu huyo ambae pia ni mratibu wa makazi ya Ulyahulu yaliyopo Kigoma.
Alifafanua kwamba kikwazo ni wakimbizi ambao wanataka walipwe Sh. 19 milioni kila mmoja kama fedha za uhamisho badala ya Sh. 300,000 walizopangiwa.
Mmoja wa wakimbizi, Andrea Helmashi, alisema Sh. 300,000 ni ndogo kwa kuwa wengine wanafamilia ya watu zaidi ya 10 na kupendekeza kwamba wangelipwa Sh. 13 milioni.
SERIKALI INASEMAJE
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Rajab Rutenge, alitetea uwekezaji huo akieleza kwamba ni wa faida kubwa kwa taifa na wakazi wa maeneo yanayozunguka makazi hayo kwani utaboresha upatikanaji wa chakula nchini.
Mimi ni mtalaamu wa masuala ya chakula na nchi yetu inakabiliwa na janga la njaa, ni lazima tushirikiane na kampuni ya Agrisol kumaliza tatizo hilo, alisema.
Kwa upande wake, Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ambaye ni mmoja wa waliotia saini makubaliano hayo, Patrick Mwakuysa, alisema kampuni hiyo ina lengo la kuongeza uzalishaji wa chakula, masoko na kutengeneza ajira kwa Watanzania.
Na Gerald Kitabu
31st July 2011
Ni ule mwekezaji aliyepewa ardhi kwa miaka 99
Kodi ya ardhi sh. 200, Halmashauri kupata sh.500
Diwani wa kata ya Litapunga, Godfrey Lusambo (kulia) akiwa na viongozi wa serikali ya mtaa na wanakijiji cha Kambuzi Halt, Katumba, wilaya ya Mpanda, wakilalamika kwa watafiti wa Shirika la Haki Ardhi na waandishi wa habari.
Wananchi, watendaji wa vijiji na Madiwani wa kata za Litapunga na Mishamo Wilayani Mpanda, Mkoa mpya wa Katavi, wamepinga yaliyokuwa makazi ya wakimbizi ya Mishamo na Katumba, kukodishwa kwa mwekezaji ambaye ni kampuni ya Agriosol ya Marekani, kwa maelezo kwamba uwekezaji huo, hautakuwa na tija kwa taifa.
Makubaliano ya awali (ambayo NIPASHE inayo nakala yake), kati ya mwekezaji huyo na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, yanaonyesha kwamba kampuni ya Agrisol itakodisha kwa miaka 99, eneo la Katumba hekta 80,317 na Mishamo hekta 219,800.
Mwekezaji pia atalipa Sh. 200 kama kodi ya ardhi kwa ekari na Halmashauri itapata Sh. 500 kwa ekari, hata hivyo haijulikani malipo hayo yatalipwa kwa muda gani yaani kwa mwezi au kwa mwaka.
Makubaliano hayo yanaonyesha pia kwamba iwapo kutatokea mgogoro, serikali itatumia busara kuutatua lakini ikishindikana, shauri hilo litasikilizwa jijini London, Uingereza na msuluhishi ambaye atakuwa Chemba ya Biashara ya Kimataifa (International Chamber of Commerce).
Kadhalika, inaelezwa kwamba mwekezaji huyo ataajiri mameneja wa mashamba kutoka nje hususan Afrika Kusini na ataendesha kilimo cha mbegu za kimaabara.
Hata hivyo, baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo Mawaziri na wale wa Halmashauri ya Mpanda, wamekuwa 'wakipigia debe' uwekezaji huo, kwa madai kwamba utaongeza uzalishaji wa chakula na kuongeza ajira kwa Watanzania.
WANANCHI
Watendaji wa vijiji na Kata zinazozunguka maeneo hayo, wamepinga uwekezaji huo kwa maelezo kwamba hawajashirikishwa kikamilifu na hati hiyo haina maslahi kwa taifa.
Wakizungumza na waandishi wa habari walioongozana na timu ya watafiti kutoka shirika la HakiArdhi kuhusiana na uwekezaji huo, viongozi hao na wananchi wameitaka serikali ijifunze kwa yaliyotokea kwa kampuni tata ya Dowans kwa kujifunga na mikataba mibovu, ya muda mrefu kwa bei chee.
Mwekezaji pia anaitaka serikali ibadili sheria ili kuruhusu kilimo cha vinasaba (Genetically Modified Crops), ambacho kimsingi kinaua mbegu za asili na kudhoofisha ardhi.
Diwani wa kata ya Litapunga, Godfrey Lusambo, alisema madiwani wa kata zinazozunguka eneo hilo, hawakuwahi hakualikwa kwenye mikutano iliyopitisha makubaliano hayo tata wala kwenda kwenye ziara nchini Marekani.
Viongozi wa wilaya wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Wenyeviti wa kamati na Madiwani wa kutoka mbali na hapa kama vile Mpimbwe na Ulwila ndio waliokwenda Iowa- Marekani na waliporudi tu sisi tukawa tunaletewa maagizo bila kujua undani wake, alisema.
Msafara wa wajumbe kumi waliokwenda Iowa-Marekani uliongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Salum Chima, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Rajabu Rutenge, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpanda, Philip Kalyalya, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpanda Silvester Nswima, Mkurugenzi wa Wilaya Eng. Emmanuel Kalobelo, Mjumbe wa kamati ya fedha Rose Mayaya, na Mjumbe wa Kamati ya maadili Teddy Nyambo.
Wengine ni Mwanasheria wa Halmashauri Patrick Mwakyusa, Afisa Kilimo na Mifugo Fabian Kashindye, na Haruna Mwakitanile (cheo hakikuweza kupatikana mara moja).
Alisema wajumbe hao waliporudi kutoka Marekani, wananchi walishangazwa na kitendo cha Serikali kutenga mipaka kwa ajili ya mwekezaji wakati vijiji hivyo havijawahi kupimwa.
Ofisa Mtendaji wa kata ya Mishamo, Agustino wanga, alisema hawajawahi kuiona kampuni ya AgriSol wala wawakilishi wao ambao ni Agrisol Tanzania Limited, na kwamba wamekuwa wakiwasikia viongozi wakieleza kuwa makazi hayo ya wakimbizi yatakodishwa kwa Wamarekani kwa miaka 99.
Mimi binafsi nina mpango wa kuhama kabisa maana wakiondoka wakimbizi tu, huduma muhimu nazo zitakoma, hatuwezi kuwezana na mwekezaji ambaye hatumjui, alisema.
Kwa upande wake, Katibu wa jumuiya ya wafugaji mkoani Rukwa, Masanja Katambi, alisema inashangaza kuona serikali inaingia mkataba usio na maslahi kwa taifa badala ya kuwapatia wafugaji maeneo hayo ambao wamekuwa wakigombea malisho na wakulima.
Kila siku wafugaji wanagombana na wakulima na mara nyingine kuuana, kwa sababu ardhi haitoshi katika mkoa wetu. Wafugaji hudiriki hata kuwahonga askari wa wanyamapori katika mbuga ya Katavi ili kuingiza mifugo yao kwa malipo maalumu, hili Serikali hailioni? alisema.
Mkuu wa Makazi ya Katumba na Mishamo, Athuman Igwe, alisema anachosubiri ni kutekeleza amri ya serikali pindi taratibu za uwekezaji zitakapokamilika.
Hata hivyo, alisema wakimbizi walipaswa kuwa wameondoka kupisha uwekezaji lakini anashangaa kuona kuwa bado zoezi hilo halijakamilika mpaka hivi sasa.
Hili Zoezi la kuwahamisha wakimbizi linaratibiwa na Tamisemi, sisi tunasubiri utekelezaji tu, alisema mkuu huyo ambae pia ni mratibu wa makazi ya Ulyahulu yaliyopo Kigoma.
Alifafanua kwamba kikwazo ni wakimbizi ambao wanataka walipwe Sh. 19 milioni kila mmoja kama fedha za uhamisho badala ya Sh. 300,000 walizopangiwa.
Mmoja wa wakimbizi, Andrea Helmashi, alisema Sh. 300,000 ni ndogo kwa kuwa wengine wanafamilia ya watu zaidi ya 10 na kupendekeza kwamba wangelipwa Sh. 13 milioni.
SERIKALI INASEMAJE
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Rajab Rutenge, alitetea uwekezaji huo akieleza kwamba ni wa faida kubwa kwa taifa na wakazi wa maeneo yanayozunguka makazi hayo kwani utaboresha upatikanaji wa chakula nchini.
Mimi ni mtalaamu wa masuala ya chakula na nchi yetu inakabiliwa na janga la njaa, ni lazima tushirikiane na kampuni ya Agrisol kumaliza tatizo hilo, alisema.
Kwa upande wake, Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ambaye ni mmoja wa waliotia saini makubaliano hayo, Patrick Mwakuysa, alisema kampuni hiyo ina lengo la kuongeza uzalishaji wa chakula, masoko na kutengeneza ajira kwa Watanzania.