Kweli ndugu mimi nafikiri mshahara wa Dr. ni kidogo sana ukilinganisha na kazi anayoifanya nafikiri ni bora akaongezewa. Kwani hayo manyagau yanalipwa shilingi ngapi? nani aliwahi kuwahoji kuhusu mishahara ndani ya chama chao cha magamaba? Waache kutufanya watz kama wajinga tusiejua nani mkweli na nani mwongo.Kuna kitu muhimu sana ambacho watanzania tumekisahau baada ya Dk Slaa kuhojiwa na mwandishi mmoja wa habari mwaka jana baada kupinga mishahara mikubwa ya wabunge.
Mwandishi huyo (Jina lake silikumbuki) alimmuuza Dk Slaa, 'Kama unaona mshahara wa wabunge ni mkubwa mbona bado na wewe unaupokea?'. Dk Slaa alijibu kwa ufasaha kabisa kwamba yeye anaupokea mshahara ule kwa kuwa ndio anaoutumia kuzunguka nchi nzima kuwataja mafisadi. Kazi ambayo hakika bado anaifanya hadi leo licha ya kuwa nje ya bunge.
Mi binafsi sioni nongwa kwa Slaa kulipwa huo mshahara kwa kazi kubwa anayoifanya. Lakini swali la kujiuliza, Wilson Mukama analipwa Milioni 11 kwa kukaa tu ofisini, je hii ni sawa?
Maana hata katika puyanga wanayoifanya kina Nape Nnauye huko mikoani yeye simuoni kabisa.
Mi nasisitiza Dk Slaa angozewe mshahara kwa kuwa kazi anayoifanya ni kubwa. Kutaja mafisadi tena na ushahidi juu na wahusika wakikwama kwenda mahakamani si kazi rahisi.
Slaa, Big up my President!
Kuna kitu muhimu sana ambacho watanzania tumekisahau baada ya Dk Slaa kuhojiwa na mwandishi mmoja wa habari mwaka jana baada kupinga mishahara mikubwa ya wabunge.
Mwandishi huyo (Jina lake silikumbuki) alimmuuza Dk Slaa, 'Kama unaona mshahara wa wabunge ni mkubwa mbona bado na wewe unaupokea?'. Dk Slaa alijibu kwa ufasaha kabisa kwamba yeye anaupokea mshahara ule kwa kuwa ndio anaoutumia kuzunguka nchi nzima kuwataja mafisadi. Kazi ambayo hakika bado anaifanya hadi leo licha ya kuwa nje ya bunge.
Mi binafsi sioni nongwa kwa Slaa kulipwa huo mshahara kwa kazi kubwa anayoifanya. Lakini swali la kujiuliza, Wilson Mukama analipwa Milioni 11 kwa kukaa tu ofisini, je hii ni sawa?
Maana hata katika puyanga wanayoifanya kina Nape Nnauye huko mikoani yeye simuoni kabisa.
Mi nasisitiza Dk Slaa angozewe mshahara kwa kuwa kazi anayoifanya ni kubwa. Kutaja mafisadi tena na ushahidi juu na wahusika wakikwama kwenda mahakamani si kazi rahisi.
Slaa, Big up my President!
Haijaandikwa popote, isispokuwa JK alimteua Makamba, pamoja na kwamba kila mtu halijua kuwa hakuna sifa yoyote ya kuwa mbunge. Kwa kipindi chake nakumbuka alichangia mara mara moja tu. Kwa sasa JK bado ana nafazi saba za kuteua wabunge
Wakuu tukumbuke kuwa Katibu mkuu wa CCM:
1.Hulipwa mshahara wa Ukatibu mkuu na marupurupu mengine ya kichama na hutumia usafiri wa ...Chama.
2.Katibu mkuu wa CCM huingia Bungeni kutokana na cheo chake,ina maana hapo tena hulipwa ...Mshahara kama Mbunge na Posho zote za ...kibunge na mkopo wa usafiri wa wabunge
Ukipiga hesabu hapa ina maana Katibu Mkuu huyu kwa Mwezi huingiza pesa nyingi sana.
Naye Mabere Marando alikituhumu CCM kuwa kinamlipa Katibu Mkuu wao Sh 11 milioni kwa mwezi
Alipoulizwa na Mwananchi kuhusu madai ya Marando, Mukama alikataa kutaja mshahara wake akisema kuwa ni siri yake.
Wakuu tukumbuke kuwa Katibu mkuu wa CCM:
1.Hulipwa mshahara wa Ukatibu mkuu na marupurupu mengine ya kichama na hutumia usafiri wa ...Chama.
2.Katibu mkuu wa CCM huingia Bungeni kutokana na cheo chake,ina maana hapo tena hulipwa ...Mshahara kama Mbunge na Posho zote za ...kibunge na mkopo wa usafiri wa wabunge
Ukipiga hesabu hapa ina maana Katibu Mkuu huyu kwa Mwezi huingiza pesa nyingi sana.
Heee ni wapi imeandikwa kwamba katibu mkuu huingia bungeni kwa cheo chake? Huenda una hoja kwa kuwa umetoa angalizo kwa wekundu. Tusaidie hoja hapa au Mukama naye anandaliwa kuteuliwa kuwa Mbunge? Hivi JK hajamaliza zile nafasi zake kumi za akina Nahodha, Meghji na Mbarawa?