Kumbe CDM hamna Wasomi

Rais mbowe mawaziri sugu,lema former mp,lucy kiwelu,watamalizia wao mimi naona kichefuchefu tu hapa hawa watu bado hawajajipanga kuchukua nchi labda ubunge tu
 
Rais mbowe mawaziri sugu,lema former mp,lucy kiwelu,watamalizia wao mimi naona kichefuchefu tu hapa hawa watu bado hawajajipanga kuchukua nchi labda ubunge tu
Kama unaona kichefuchefu nakushauri ukatapike katika choo cha magamba.
 
Wasomi wa CCM wameifikisha wapi CCM na nchi kwa ujumla? Mwenyekiti wenu mchumi wa chuo kikuu hajui kwa nini nchi anayoiongoza ni maskini!

Wasomi CDM wako wengi sana, tofauti ni kuwa wengi wao ni vijana wadogo na professionals wenye shughuli zao. Unataka wote tuvae magwanda kwenda maofisini ndio mjue kuna wasomi kiasi gani! 2015 ndio utaona ninachozungumzia leo.
 
Huwezi kuwaona kwa sababu unaangalia ndani ya box. Sisi tunaangalia nje ya box. Siasa za personalities ndizo zimewafikisha CCM hapo walipo. Hawana ideas, hawana sera, hawana vision. Sisi tunajenga vision ya kuwasaidia Watanzania kujikwamua na ufisadi, kuwasaidia Watanzania wawe wawekezaji na wajasiriamali wenyewe, kuwasaidia Watanzania kusimamia maendeleo yao bila kutegemea wale waliotunyonya na kutufikisha hapa kwamba ndio wakombozi wetu. Sasa wewe ukianza kuangalia personalities, huwezi kuwaona, lakini ukijikita katika sera na vision wapo Watanzania ndani na nje ya nchi ambao wako tayari kulisukuma gurudumu hili la mageuzi.

WaTz ndani na nje ya nchi ,kweli wapo tena wengi sana,ila hawa hawawezi kukubalika kushika nafasi za uongozi kama za Uraisi na mawaziri wake ,haiingii akilini ,mimi hapa napigana na chama tawala kufa kupona nadhalilika mitaani nanyanyasika bungeni halafu tunaibuka kidedea unamtoa mtu ulaya aje kuwa waziri ,naona kitanuka.

Karume hakusoma baada ya Mapinduzi ,wengi walimfuata kudai wadhifa akawambia haiwezekani kumtoa mtu kijijini akaendeshe meli akimaanisha kwamba si kila mtu anaweza kuwa kiongozi kuongoza serikali.

Jambo moja nitalikubali ikiwa Raisi anaweza kumchagua mtu yeyote yule ambae pengine si wa chama chake,sio mbunge kuwa waziri wake ,hapo mnaweza kuwategemea hao WaTz watakaoweza kusaidia kulisukuma gurudumu la maendeleo.

Ila kwa ninavyoiona CDM ndani ya nchi yetu na jinsi walivyo viongozi walio mstari wa mbele katika chama hiki ambao tegemeo lao na waongozwa ni kwa wao kutoa Raisi na mawaziri,sioni kama kitatosheleza ngazi nilizohitaji kupangiwa safu(proposed)
 
Mbona silaha zinajulikana ,ninavyofahamu silaha za Chama ni sera ,? Na nilichowapa ni ushindi hivyo katika ushindi nilihitaji ni nani hao ambao(proposed) wataongoza nchi hii ? baada ya kushinda uchaguzi ,mbona mnakuwa wagumu ni kitu rahisi tu ,inaonyesha hamujiamini mnaogopa ,si ndio !

Ndoto za mchana, aren't you anyhow better than that!??
 
Naona mnafufuka mmoja mmoja ,yaani mnakuwa kama mazombi ,unaulizwa wewe unarukia kwengine ,mkuu hapa nazungumzia CDM tu .

Inawezekana wewe humjui hata kiongozi mmoja wa CDM zaidi ya Slaa,Zito,Mnyika,Lisu na mbowe ni hatari kubwa sana kuwa na wafuasi wa dizaini zako.
kwenye red patamu..........
 
Nawashangaa sana CDM ,wanataka kuongoza Nchi hii ,ukiangalia pale ndani utaona hamna kitu ,hivi wanafikiria wanataka kuongoza kijiji ? Ndio maana unawasikia wataunda serikali ndogo iliyo na mawaziri wachache sana,nikakumbuka pale walipoweka mgombea mwenza jamaa aliehitimi darasa la saba ,na kwa Zanzibar hakuna darasa saba ,inamaana alikimbia shule. eti watategemea washauri ,unategemea washauri wakati nao wanahitaji elimu ya juu.

Hebu tupangieni hapa safu yenu ,tuiite proposed safu ya uongozi ,ukianza na Raisi labda tuseme wizara kumi mpaka kumina tano ,tuone ! na kuwajadili au kuijadili hio safu !

Wewe umesoma mpaka darasa la ngapi? Je ktk ukoo wenu kuna msomi?
 
Rais mbowe mawaziri sugu,lema former mp,lucy kiwelu,watamalizia wao mimi naona kichefuchefu tu hapa hawa watu bado hawajajipanga kuchukua nchi labda ubunge tu

Hata ubunge hatukujipanga tukachukua majimbo kibao,uraisi pia hatukujipanga hadi tume ya uchaguzi,TISS,na CCM wakawa timu moja, wewe shabiki hujui kilichoko ndani ila waulize akina Bomani na TISS watakwambia!
 
Wasomi wa CCM wameifikisha wapi CCM na nchi kwa ujumla? Mwenyekiti wenu mchumi wa chuo kikuu hajui kwa nini nchi anayoiongoza ni maskini!

Wasomi CDM wako wengi sana, tofauti ni kuwa wengi wao ni vijana wadogo na professionals wenye shughuli zao. Unataka wote tuvae magwanda kwenda maofisini ndio mjue kuna wasomi kiasi gani! 2015 ndio utaona ninachozungumzia leo.

Tunasoma kutokana na makosa yaliopita kama hayo ya CCM ,kosa la CCM katika tawala baada ya Nyerere ni kutowajibika na kutofuatwa sheria kila mmoja anakula upande wake na kila mmoja anamuogopa mwenzake ,tumeona baada ya zoezi la kubadilishwa Mawaziri kidogo kuna muelekeo ,weka kando hilo.

Mimi nipo na washika dola watarajiwa Chadema au hilo ni kosa kujadili ? Nionavyo CDM ikijaaliwa kukamata dola ,ni lazima kuhakikisha sheria zinafiatwa kuanzia juu hadi chini bila ya kuogopana ,hakuna atakae kuwa juu ya sheria,kwa msemo mwengine sheria itatakiwa itawale na sio itawaliwe kama tuonavyo ndani ya utawala wa CCM.

Hivyo kutahitajika wenye elimu na hizo professionals ,ambazo unasema mnazo ila mpo nje ya pazia sikubaliani na wewe kuwa itakuwa rahisi kukuvuta ndani ya uwaziri au Uraisi ,wakati waliotia viraka kuhangaika na chama wapo na tunawaona kwenye majukwaa na kama nyinyi mpo vaeni magwanda kwenye mikutano tuwaone ,weka mbali ofisi ,hivi unasubiri watu wapiganie huko halafu wewe uwe waziri ? Labda uwe ni ndugu au jamaa wa mkuu.

naamini safu itatokana na hawa tuliowazoea kuwaona wakiwa mstari wa mbele ndio nikasema tupangieni hao proposed.
 
ccm inawasomi wengi sana na wametumia usomi wao kuliangamiza taifa.pumbaf

Ndo faida ya wasomi wa CCM....
Wasomi wanaoingia mikataba mibovu.....unafanya mchezo na
10%
Wasomi wanaokwwiba pesa na kuzihifadhi swis
Wasomi wenye trilion 3.....za kukwibaaaa
Wasomi wauza ardhi kwa kigezocha uwekezaji....hawa wasomi ukiwa mzungu na 10% yako wanakukatia ardhi, then unaenda kukopa benki ya ndani......loh.....
Wasomi wanaopima viwanjaa na kuchukuliwa na wasomi wao wabunge na mawaziri....
Wasomi wanaouza wanyama nje ya nchi......
Wasomi wa EPA, Richmond....
Wasomi walioshindwa kuifanya tanzania kuwa na umeme wa kutosha....
Wasomi walioshindwa kusupply maji safi na salama nchi nzima...
Wasomi wanaoshindwa kutoa huduma bora za afya...
Wasomi wanaoshindwa kutoa mikopo ya elimu ya juu...
Wasomi wanaohakikisha elimu inaboreshwa kwa wanafunzi kusomea kwenye nyasi....
Wasomi wanaofikiri uchumi wa tanzania upo juu kwa kuangalia idadi ya magari...
Wasomi walioongoza umati wa watanzania kunywa kikombe kwa babu wa loliondo....
Wasomi ambao hawachelewi kuku-ulimboka....
Wasomi ambao hawajui kwanini tanzania ni masikini
wasomi walioshindwa kutengeneza ajira kwa vijana.....

CCM oyeeee
kigumu chama cha mapinduzi....
Zidumu fikra za mwenyekiti......
 
Nawashangaa sana CDM ,wanataka kuongoza Nchi hii ,ukiangalia pale ndani utaona hamna kitu ,hivi wanafikiria wanataka kuongoza kijiji ? Ndio maana unawasikia wataunda serikali ndogo iliyo na mawaziri wachache sana,nikakumbuka pale walipoweka mgombea mwenza jamaa aliehitimi darasa la saba ,na kwa Zanzibar hakuna darasa saba ,inamaana alikimbia shule. eti watategemea washauri ,unategemea washauri wakati nao wanahitaji elimu ya juu.

Hebu tupangieni hapa safu yenu ,tuiite proposed safu ya uongozi ,ukianza na Raisi labda tuseme wizara kumi mpaka kumina tano ,tuone ! na kuwajadili au kuijadili hio safu !

Unataka wasomi mkuu, kama akina Mkulo,Karamagi,Ngeleja,Lowasa,Nundu,Ekelege,Blandina Nyoni,Mponda,Maige,na wenzao!? i wapi tija yao?
 
Ccm kuna wasomi wazuri..RAIS Lusinde,PM Atakuwa Prof Steven ngonyani,MAKAMU WA RAIS Komba,WAZIRI WA FEDHA Lameck Airo.
 
Rais mbowe mawaziri sugu,lema former mp,lucy kiwelu,watamalizia wao mimi naona kichefuchefu tu hapa hawa watu bado hawajajipanga kuchukua nchi labda ubunge tu

basi kutokana na mawazo kushoto uliyonayo,uraisi tutampa PRO.MAJIMAREFU maana naona magamba mnataka na mnaamini Nguvu za Giza.
 
Aloo mimi nimesoma kiasi tu,nikianzia kisosora tanga(RC) nikapitia Jumuia pale mkabala na standya mabasi nikaelekea duga shule ya tapa palikuwa na mbuyu barabarani(umeanguka) kutoka hapo nikasoma Murutunguru kule Nansio Ukerewe ,nikamalizia chuo cha ufundi civil eng somewhere undislosed location.Sina taarifa za ukoo nimezaliwa peke yangu wazazi wangu wawili walifariki katika ajali ya basi sekenke.
 
mimi naitaj kiongozi na siitaj msomi kwani ni wasomi wangapi wapo kwenye serikali hii ya ******? nini wanachofanya zaidi ya kubuni mbinu za kutuibia kila cku?kwa kuwapa maprofesa uongoz ni kuzalilisha elimu zao wa 7bu wanafanya madudu mpaka naona hakuna haja ya kusoma. kwa mfano huyu mchemba ana elimu ya darasani lakn hajaelimika hata kidogo kwa maisha ya kawaida hamnazo huyu.

Okay ,na mimi naona kama uonavyo ,hatuhitaji msomi ,mimi sijasema katika hiyo safu lazima mupange wasomi,huko ni kujikanyaga ,ila katika hizo nafasi ni lazima kujipanga ili gurudumu alilodai Mkuu Jasusi liweze kusukumwa kwa maarifa na ustadi mkubwa lisije likalalia upande mmoja ,ni akina nani hao waliomo CDM kuanzia Uraisi na baraza la mawaziri 15 ambao mnaweza kuwapropose.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom