Kumbe askofu kulola alikuwa mapacha?

Kumbe askofu kulola alikuwa mapacha?

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
19,349
Reaction score
36,302
Yakiwa yamebakia masaa machache kabla ya kuhifadhiwa kwa mwili wa mpendwa wetu,Muasisi wa Makanisa na Huduma za wokovu nchini Tanzania, Marehemu Askofu . Dk. Moses Kulola, imefahamika kuwa Mwanajeshi huyu wa kiroho aliyetumikia Jeshi la BWANA YESU katika kipindi chote cha maisha yake ya hapa duniani alikuwa ni mtu wa nyota ya MAPACHA ama GEMINI. Kinyota , watu waliozaliwa kati ya MEI 20 na JUNI 21 ni watu wa NYOTA YA GEMINI. Imefahamika kuwa Marehemu Askofu Kulola alizaliwa tarehe 02 JUNI 1930. SIFA KUU ya watu wa NYOTA ya GEMINI, huwa ni kufanya mambo makubwa sana na ya kipekee sana iwe ni katika michezo, sanaa, uongozi, utumishi,elimu nakadhalika. . Maisha ya watu wa mapacha huongozwa (kwa kujua ama kutokujua ) na nishati " energy " inayo patikana kwenye andiko linalopatikana kwenye kitabu cha ECCLESIASTES 9:10

" Whatever your hand finds to do, do it with all your might, for in the realm of the dead, where you are going, there is neither working nor planning nor knowledge nor wisdom. ".

Ndio maana chochote kile akifanyacho mtu wa nyota ya mapacha huwa kinafanikiwa sana iwe ni kizuri ama kibaya. Utafiti unaonyesha kuwa , karibu katika kila eneo la maisha ya mwanadamu kuanzia kwenye michezo, uongozi,sanaa, biashara, elimu nakadhalika , kuna mtu wa nyota ya mapacha ambaye anachukuliwa kuwa wa kipekee sana katika eneo hilo husika...

N.B: Ninaomba radhi kwa nitakao kuwa nime wakwaza kwa kulihusisha jina la Marehemu Askofu Kulola na mambo ya nyota, ila kwa wasio fahamu, elimu ya nyota ipo toka enzi za Pontyo wa Pilato, hata wale Mamajusi walitumia nyota kugundua kuwa Mfalme Yesu amezaliwa.

MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU ASKOFU KULOLA MAHALI PEMA PEPONI, NA AWAFARIJI WAFIWA. AMINA
 
Acha uchawi wako! mpunga nyota wewe! askofu hakuongoza kanisa kinajimu bali kwa nguvu za Roho mtakatifu. koma tabia hii. katika Jina lipitalo majina yote la Yesu kristo wa Nazereti.
 
uchawi wa shehe yahaya.. usiulete kwa mtumushi wa mungu
 
Acha uchawi wako! mpunga nyota wewe! askofu hakuongoza kanisa kinajimu bali kwa nguvu za Roho mtakatifu. koma tabia hii. katika Jina lipitalo majina yote la Yesu kristo wa Nazereti.

Uzi wangu umejaa hekima kuliko komenti yako and yet u claim to be the follower of YESHUA. Uzi huu ni mkubwa sana kuliko wewe, u better back down!
 
acha kutuletea habari za kimajini majini na kishirikina hapa,pambafu!
 
Kwa nijuavyo usomaji wa nyota hauna nafasi katika imani ya kikristo! hatuambiwi wale mamajusi walikuwa wataalamu wa kusoma nyota za 'mapacha, au gemini'. wataalamu wa nyota haina maana ya ubashiri wa jinsi hii. Hii ni kazi ya Lucifa na jeshi lake

mix with yours
 
Its proof that watu wa nyota ya MAPACHA are very strong and blessed!
You claim that they succeed in whatever venture they embark in, be it good or evil. Aren't you suggesting that some are good disciples of the father of evil the devil himself!
 
Acha uchawi wako! mpunga nyota
wewe! askofu hakuongoza kanisa kinajimu bali kwa nguvu za Roho mtakatifu. koma tabia hii. katika Jina lipitalo majina yote la Yesu kristo wa Nazereti.
 
Mbona na mie ni PACHA pia ila ni mtu wa kawaida sana tu hapa SIKONGE.
 
You claim that they succeed in whatever venture they embark in, be it good or evil. Aren't you suggesting that some are good disciples of the father of evil the devil himself!


Umenielewa vibaya kaka, nimemaanisha kuwa watu wa Gemini huwa strong sana katika kazi au mambo wanayo yafanya, mambo hayo yanaweza kuwa ni michezo, uigizaji, muziki, biashara, huduma ya kiroho nakadhalika. Hii ni mifano michache:

i. Tupac Shakur & Notorious B.I.G a.k.a BIggie Smalls : WAFALME WA HIPHOP DUNIANI.

ii. Reginald Mengi
iii. George Bush wa pili... List ni ndefu sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom