Think Tank
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 233
- 25
Hata mimi nimeshangaa uelewa wa hawa jamaa wa NCCR Mageuzi kuhusu hii order ya mahakama. Sheria imewatupa mkono hawa.
NCCR wana best lawyers kama akina Mvungi..nafikiri wana uelewa zaidi wa sheria kuliko unavyowashutumu
Mkuu Invisible, deep yenyewe ndio hiyo, haya mambo ni mazito kuliko tunayoyaona juu juu. CCM mara nyingi kama sio zote ndio mainjinia wa migogoro ya vyama vya upinzani. Mbana Hassan, Mshirika wa Kafulila ni mzee asiyekuwa na kipato cha kumwezesha kuzunguka nchi nzima, ghafla alipata uwezo huo kwa mijihela ya Mkono. Hela ndio shina la dhambi hii ndugu yangu
Unajua kipindi cha Star TV mda wake unakuwa mfupi na hatuwezi kupata majibu ya maswali yote juu ya huyu Mh. Kafulila. Kwani yeye sio Member wa hii Forum? kama vipi namuomba Mh. Zitto amlete humu jamvini ili atujibu haya maswali yote. Nawasilisha
Mh. Machali, baada ya kumfukuza Kafulila, mmejiandaaje kichama kulikomboa jimbo la kasulu kusini? Je mtaji aliokuwa nao Kafulila unadhani ni wa NCCR au wa kwake David mwenyewe?
Baadaye iligundulika kwamba Kafulila yuko financed na watu mbalimbali, inasemekana hadi Nimrod Mkono anahusika katika kutoa mijihela ya kuimaliza NCCR
SWALI KWA MH KAFULILA TRH 22.1.2012
Baada ya kuhama Chadema , Mh Zitto Kabwe alikuunga mkono katika harakati zako za kupata Ubunge kupitia NCCR Mageuzi.
pia katika Mgogoro wako na NCCR mageuzi unatuhumiwa kwamba ulikuwa unamfagilia njia mh Zitto ili aweze kugombea urais kupitai nccr endapo kipengele cha umri kupitia katiba mpya kitaondoshwa.
Swali. Ni upi uhusiano wako na Mh Zitto kisiasa hadi kufikia Mh zitto kujitoa hali na mali juu yako?
SWALI LA 2:
Inasemekana Umedanganya Bunge kuhusu Elimu yako, wapo wanaojidai wewe ni Kidato cha 6, lkn nyaraka za bunge zinaonyesha unashahada ya 1 uliopata UDSM. Swali upi Ukweli kuhusu Elimu yako?
Hamad rashid anaingia kwenye kundi la wazee au vijana??Tatizo ni kwamba viongozi wengi wa vyama ni wazee na hawako tayari kuona nafasi zao zinahatarishwa na vijana, kwahiyo hutaona mzee akifukuzwa ndani ya chama zaidi ya kushauriwa ajipime mwenyewe!
Umemsikia bila shaka Machali akisema James Mbatia ni taasisi, aking'olewa katika nafasi ya uenyekiti chama kitasambaratika! Kwahiyo utaona ni kwanini Mbatia analindwa kwa nguvu zote na kwa gharama yoyote.
SWALI KWA MH KAFULILA TRH 22.1.2012
Baada ya kuhama Chadema , Mh Zitto Kabwe alikuunga mkono katika harakati zako za kupata Ubunge kupitia NCCR Mageuzi.
pia katika Mgogoro wako na NCCR mageuzi unatuhumiwa kwamba ulikuwa unamfagilia njia mh Zitto ili aweze kugombea urais kupitai nccr endapo kipengele cha umri kupitia katiba mpya kitaondoshwa.
Swali. Ni upi uhusiano wako na Mh Zitto kisiasa hadi kufikia Mh zitto kujitoa hali na mali juu yako?
SWALI LA 2:
Inasemekana Umedanganya Bunge kuhusu Elimu yako, wapo wanaojidai wewe ni Kidato cha 6, lkn nyaraka za bunge zinaonyesha unashahada ya 1 uliopata UDSM. Swali upi Ukweli kuhusu Elimu yako?