Kulikoni Wamachinga walipie vitambulisho mara mbili?

Kinoamiguu

JF-Expert Member
Nov 29, 2018
10,764
13,370
Habari za majukumu wakuu.

Nilikuwa nangalia Azam TV asubuhi hii. Mtangazaji alikwenda stand ya Segerea kuwahoji watumishi wa stand ile.

Miongoni Mwao ni mfanyabiashara mdogo. Kwa mujibu wa mfanyabiashara yule ni kwamba wao walishalipia VITAMBULISHO VYA WAMACHINGA tsh 20000 kwa mwaka.

Hata hivyo cha kushangaza ni kwamba manispaa unaendelea kuwatoza KODI / USHURU kila uchao. Wakiuliza kulikoni wanaambiwa vitambulisho vya Wamachinga pesa yake ilienda serikali kuu na kwamba haihusiani na manispaa.

Unajiuliza maswali.

Je, mbona raisi wa wanyonge alisema hakuna kuwabughudhi Wamachinga baada ya kulipa ile 20000/ na tena akasema vitambulisho vitatumika hata kwa matibabu?

Tofauti kati ya kodi za manispaa na serikali kuu ni nini na kwanini mtu mmoja tena nyongeza kama anavyoitwa alipe kodi mara mbili?

Uko wapi ule msimamo kwamba Wamachinga akilipa kodi na kupata vitambulisho mpaka mwakani?

Tulidanganywa kwenye kampeni? Kwanini?

Chanzo: Azam TV morning trumpet
 
Kwa kuangalia ukweli na jinsi manispaa zinavyojiendesha hivi vitambulisho vimewaumiza sana manispaa zote nchini.

kwa siku mfano hapo Segerea ushuru wa soko,mama ntilie nk ulikuwa ni kama laki 3 hivi.so kwa mwezi ni 300000x30 ni milion 9.hapo ni stand tu.b Bdo sehem zingine.

vitambulisho vya machinga kwa siku 360 ni tzs 20000. na hii hela inaenda ofisi ya rais. je manispaa inafaidika na nini kwa uwepo wa wa fanya biashara wadogo kwenye maeneo yake ambapo kila baada ya saa 24 manispaa zinatakiwa kuondoa uchafu uliozalishwa na hava wafanya biashara? Kuhakikisha ulinzi(mgambo) wapo wa kutosha nk.

Serikali kwa hili inatakiwa ijitafakari na kuja na suluhisho la kudumu. Pale Kariakooo zaidi ya million tano zinapotea kila siku kuingia kwenye mapato ya wilaya ya ilala,lakini itokee siku Kariakoo apajasafishwa, taka zake zitajaza malori zaidi ya 50 nani analipia huu usafi na kwa hela toka mfuko upi?

Kwa sasa viongozi wengi wana fanya kazi na kutimiza majukumu yao katika mazingira magumu na yenye bajeti kiduchu au zero kabisa.
 
Kwa kuangalia ukweli na jinsi manispaa zinavyojiendesha hivi vitambulisho vimewaumiza sana manispaa zote nchini.

kwa siku mfano hapo Segerea ushuru wa soko,mama ntilie nk ulikuwa ni kama laki 3 hivi.so kwa mwezi ni 300000x30 ni milion 9.hapo ni stand tu.b Bdo sehem zingine.

vitambulisho vya machinga kwa siku 360 ni tzs 20000. na hii hela inaenda ofisi ya rais. je manispaa inafaidika na nini kwa uwepo wa wa fanya biashara wadogo kwenye maeneo yake ambapo kila baada ya saa 24 manispaa zinatakiwa kuondoa uchafu uliozalishwa na hava wafanya biashara? Kuhakikisha ulinzi(mgambo) wapo wa kutosha nk.

Serikali kwa hili inatakiwa ijitafakari na kuja na suluhisho la kudumu. Pale Kariakooo zaidi ya million tano zinapotea kila siku kuingia kwenye mapato ya wilaya ya ilala,lakini itokee siku Kariakoo apajasafishwa, taka zake zitajaza malori zaidi ya 50 nani analipia huu usafi na kwa hela toka mfuko upi?

Kwa sasa viongozi wengi wana fanya kazi na kutimiza majukumu yao katika mazingira magumu na yenye bajeti kiduchu au zero kabisa.
Mkuu kuwa na kitambulisho Cha ujasiria Mali sio kwamba tozo za uchafu hatuchangii. Kila mwezi tunalipa hela za taka na risiti tunapewa.
 
Mkuu kuwa na kitambulisho Cha ujasiria Mali sio kwamba tozo za uchafu hatuchangii....kila mwezi tunalipa hela za taka na risiti tunapewa.
Mkuu hapa sijajua ikoje kutokana na sehem husika, sehem ninanyofanyia baishara zangu wenye mafrem ndio tunalipa ushuru wa taka , machinga wenyewe hawalipi, wenyewe wana tozo hizo za kila siku za shilingi mia tatu, lakini pia huwa ni wabishi kuitoa hiyo mia tatu, kwa kisingizio cha kitambulisho cha machinga, kiuhalisia kuhusu suala la usafi serekali kuu hua haihusiki kabisa ni manispaa ndio zinahusika , kwa hiyo kuendelea kuichangia ni muhimu pia.
 
Kwa kuangalia ukweli na jinsi manispaa zinavyojiendesha hivi vitambulisho vimewaumiza sana manispaa zote nchini.

kwa siku mfano hapo Segerea ushuru wa soko,mama ntilie nk ulikuwa ni kama laki 3 hivi.so kwa mwezi ni 300000x30 ni milion 9.hapo ni stand tu.b Bdo sehem zingine.

vitambulisho vya machinga kwa siku 360 ni tzs 20000. na hii hela inaenda ofisi ya rais. je manispaa inafaidika na nini kwa uwepo wa wa fanya biashara wadogo kwenye maeneo yake ambapo kila baada ya saa 24 manispaa zinatakiwa kuondoa uchafu uliozalishwa na hava wafanya biashara? Kuhakikisha ulinzi(mgambo) wapo wa kutosha nk.

Serikali kwa hili inatakiwa ijitafakari na kuja na suluhisho la kudumu. Pale Kariakooo zaidi ya million tano zinapotea kila siku kuingia kwenye mapato ya wilaya ya ilala,lakini itokee siku Kariakoo apajasafishwa, taka zake zitajaza malori zaidi ya 50 nani analipia huu usafi na kwa hela toka mfuko upi?

Kwa sasa viongozi wengi wana fanya kazi na kutimiza majukumu yao katika mazingira magumu na yenye bajeti kiduchu au zero kabisa.
Na ukikohoa tu, kutumbuliwa kunakuhusu.

5-tena🙄
 
Habari za majukumu wakuu.

Nilikuwa nangalia Azam TV asubuhi hii. Mtangazaji alikwenda stand ya Segerea kuwahoji watumishi wa stand ile.

Miongoni Mwao ni mfanyabiashara mdogo. Kwa mujibu wa mfanyabiashara yule ni kwamba wao walishalipia VITAMBULISHO VYA WAMACHINGA tsh 20000 kwa mwaka.

Hata hivyo cha kushangaza ni kwamba manispaa unaendelea kuwatoza KODI / USHURU kila uchao. Wakiuliza kulikoni wanaambiwa vitambulisho vya Wamachinga pesa yake ilienda serikali kuu na kwamba haihusiani na manispaa.

Unajiuliza maswali.

Je, mbona raisi wa wanyonge alisema hakuna kuwabughudhi Wamachinga baada ya kulipa ile 20000/ na tena akasema vitambulisho vitatumika hata kwa matibabu?

Tofauti kati ya kodi za manispaa na serikali kuu ni nini na kwanini mtu mmoja tena nyongeza kama anavyoitwa alipe kodi mara mbili?

Uko wapi ule msimamo kwamba Wamachinga akilipa kodi na kupata vitambulisho mpaka mwakani?

Tulidanganywa kwenye kampeni? Kwanini?

Chanzo: Azam TV morning trumpet
Si uneambiwa peleka hiko kitambulisho Benki upate mkopo?, wasubiri nini?
 
Back
Top Bottom