..huyu Jumbe alikuwa anapinga Muungano, halafu leo hii hataki kurudi kwao Zanzibar. miaka yote ameendelea kujibanza Mjimwema, Kigamboni.
..anyway, inasemekana alitafuta Mwanasheria toka Ghana, akiitwa Kwah Swanzy, kumsaidia kuandaa kesi ya kikatiba dhidi ya serikali ya Muungano.
..inasemekana nyaraka za suala hilo zilichomolewa toka ktk ofisi ya Raisi wa Zanzibar, na kupelekwa kwa Juliasi.
..baada ya hapo sisi wananchi tulishtukizwa tu na habari toka makao makuu ya chama dodoma, kwenye kikao cha NEC, kwamba Mzee Jumbe amejiuzulu na nafasi yake imechukuliwa na Ali Hassan Mwinyi.
..inasemekana humo mwenye kikao cha NEC, vinara wa kutoka Zenj katika kumshambulia Alhaji Aboud Jumbe, alikuwa ni huyu Maalim Seif Sharrif Hamad.
..baada ya sakata hiyo, Maalim Seif Sharrif Hamad, aliteuliwa kuwa Waziri Kiongozi, akichukua nafasi ya Brig.Ramadhani Haji Faki.
..wanasiasa mbalimbali wa Zenj, mfano Col.Seif Bakari, waliingia ktk mkumbo mmoja na Aboud Jumbe, na kuwekwa kizuizini Bara.
..mambo yalitulia kidogo, lakini yakaja kuchafuka zaidi wakati Ali Hassan Mwinyi alipoteuliwa kumrithi Mwalimu Nyerere, na Sheikh Idiris Abdul Wakil kuteuliwa kugombea nafasi ya Uraisi wa Zanzibar.
NB:
..Sheikh Idiris Abdul Wakil alikuwa akiishi Ilala-Bungoni kabla ya kuteuliwa kuwa Raisi wa Zenj.
..ndiyo maana nasema hawa wa-Zenj dawa yao ni kuwatimua wote toka Bara warudi kwao wakaongee vizuri kuhusu kuvunja muungano.