Kwanza TV
Member
- May 2, 2017
- 33
- 69
Ilikuwa ni simanzi na vilio kwa wakazi wa Kimara Suka wiki iliyopita baada ya baadhi ya nyumba kubomolewa na watu wanaodaiwa kutoka TANROADS.
Wakazi tuliowahoji walionyesha kusononeka na pia kukata tamaa huku wengi wakikiri hawana pa kwenda na wamelazimika kulala nje na familia zao. Kwa mujibu wa wakazi hawa, wao walienda mahakamani na kesi bado iko mahakamani hivyo kitendo cha kuwabomolea kimewakuta hawajajiandaa kwani wanasubiri hukumu.
Kwanza TV imewasiliana na TANROADS ili kupata majibu kwa upande wa serikali kuhusu ubomoaji uliofanyika na tutaendelea kuwapa taarifa zaidi
Wakazi tuliowahoji walionyesha kusononeka na pia kukata tamaa huku wengi wakikiri hawana pa kwenda na wamelazimika kulala nje na familia zao. Kwa mujibu wa wakazi hawa, wao walienda mahakamani na kesi bado iko mahakamani hivyo kitendo cha kuwabomolea kimewakuta hawajajiandaa kwani wanasubiri hukumu.
Kwanza TV imewasiliana na TANROADS ili kupata majibu kwa upande wa serikali kuhusu ubomoaji uliofanyika na tutaendelea kuwapa taarifa zaidi
