Kuku wangu hawatagi, tatizo ni jogoo?

Shark

JF-Expert Member
Jan 25, 2010
29,423
29,084
Wadau za wikiend?

Nina shida naomba msaada wenu please,

Hivi karibuni nimeamua nami kufuga kuku hapa nyumbani kwangu kwa ajili ya kujiongezea kipato pia hata kula nyumbani. Kwa kua ndio mara yangu ya kwanza kujihusisha na ufugaji wa Kuku basi niliamua kuulizia kwanza wataalam mbalimbali juu ya hii kitu na walinishauri nianze na Jogoo mmoja na Mitetea kama wanne au watano hivi. Mwanzo sikuwaelewa maana sikudhani kama Jogoo mmoja anaweza akawatimizia haja zao wale mitetea wote wanne lakini kwa vile wengi walishauri hivi basi nami nikanunua hao kuku kwa hiyo ratio ya 1:5.

Sasa shida imekuja kua toka nimewanunua hawa kuku ni kama miezi mitatu sasa na hakuna hata yai moja. Kuchunguza vizuri kumbe ni Jogoo ndio shida. Yaani huyu Jogoo hajisikii kabisa kufanya naniliu na hao mitetea. Yaani hao mitetea wanaweza wakajipitisha mbele yake na yeye akawaangalia tu. Ninmejaribu kutumia siku mbili hizi za wikiend hii kumchunguza huyu Jogoo toka asubuhi hadi jioni sijaelewa kabisa nyendo zake.

Nimewaza mengi sana juu ya huyu Jogoo, Mwanzo nilidhani labda ni mzee lakini sio Mzee ki hivyo, na wala sio mdogo pia, ni umri wa makamo tu ambao majogoo wengine wa rika lake nawaona wanapiga kazi kisawasawa. Nimefikiri pengine kama kuna binadamu ambao sio rijali au sio ridhiki basi pengine hata huyu Jogoo anaweza kua wa dizaini hiyo pia. Au pia inaweza kua ameumbwa na aibu sana au ni domo zege labda. Au anaweza akawa anatokea jamii ya kuku ambao hawapendi sana mambo ya kupandana pandana. Angekua binadamu ningesema ameokoka (mlokole) lakini kwa kuku sidhani.
Wale wazoefu msaada wenu unahitajika please, maana miezi zaidi ya mitatu sijapata hata yai la kuonja na ninawahudumia gharama kubwa tu za bure.


Ahsanteni
 
Huku kijijini kuna mtu alisema ukiwa umem'beba jogoo kisha ukakojoa, huyo jogoo hatapiga mzigo...... sasa sijui ni kweli au ni imani tu!
Mi kuna dereva wa malori ya mkoani ndio nilimuagizia, labda yeye kule alikokua alikojoa, but kama hii theory inafanya kazi Mkuu
 
Mi kuna dereva wa malori ya mkoani ndio nilimuagizia, labda yeye kule alikokua alikojoa, but kama hii theory inafanya kazi Mkuu
Mkuu

Inawezekana kweli - kutoka Dodoma hadi Dar bila kuchimba dawa njiani? Au mpaka huyo kuku awe amebebwa kwa mikono.
 
Hapana, asipopandwa anataga mayai yasiyorutubishwa!
Kwani ushaona kuku wa mayai wakipandwa?
Kweli aisee,
So hata kuku wa Kienyeji asipopandwa still anataga tu??
Msaada Mkuu, mi mgeni kwenye hii field
 
Mkuu hakuna uhusiano wowote kati ya kuku kutaga mayai na jogoo!!...... Kazi ya jogoo ni kumfanya kuku atage mayai ambayo ni fertilized kwa maana kwamba hata kama mtetea hana jogoo ataendelea kutaga mayai kama kawaida ila hayatatotolewa!..... Hao kuku wana matatizo mengine kama vile chakula bora, umri wao e.t.c ila tatizo siyo jogoo!!
 
Kweli aisee,
So hata kuku wa Kienyeji asipopandwa still anataga tu??
Msaada Mkuu, mi mgeni kwenye hii field
anataga bila tatizo sema jogoo kazi yake ni kurutubisha yai ili liweze kutotolewa mdau unaweza kuwaacha mitete mitupu ikataga bila tatizo cha msingi zingatia chakula utakachowapa hao kuku
 
anataga bila tatizo sema jogoo kazi yake ni kurutubisha yai ili liweze kutotolewa mdau unaweza kuwaacha mitete mitupu ikataga bila tatizo cha msingi zingatia chakula utakachowapa hao kuku
Ahaa,
Chakula ni mabaki tu ya chakula cha nyumbani kwangu ndio nawapa. Sasa hapa sijajua shida itakua ni nini??
Hivi kuna kuku Mtetea mgumba au tasa kwani??
 
Wadau za wikiend?

Nina shida naomba msaada wenu please,

Hivi karibuni nimeamua nami kufuga kuku hapa nyumbani kwangu kwa ajili ya kujiongezea kipato pia hata kula nyumbani. Kwa kua ndio mara yangu ya kwanza kujihusisha na ufugaji wa Kuku basi niliamua kuulizia kwanza wataalam mbalimbali juu ya hii kitu na walinishauri nianze na Jogoo mmoja na Mitetea kama wanne au watano hivi. Mwanzo sikuwaelewa maana sikudhani kama Jogoo mmoja anaweza akawatimizia haja zao wale mitetea wote wanne lakini kwa vile wengi walishauri hivi basi nami nikanunua hao kuku kwa hiyo ratio ya 1:5.

Sasa shida imekuja kua toka nimewanunua hawa kuku ni kama miezi mitatu sasa na hakuna hata yai moja. Kuchunguza vizuri kumbe ni Jogoo ndio shida. Yaani huyu Jogoo hajisikii kabisa kufanya naniliu na hao mitetea. Yaani hao mitetea wanaweza wakajipitisha mbele yake na yeye akawaangalia tu. Ninmejaribu kutumia siku mbili hizi za wikiend hii kumchunguza huyu Jogoo toka asubuhi hadi jioni sijaelewa kabisa nyendo zake.

Nimewaza mengi sana juu ya huyu Jogoo, Mwanzo nilidhani labda ni mzee lakini sio Mzee ki hivyo, na wala sio mdogo pia, ni umri wa makamo tu ambao majogoo wengine wa rika lake nawaona wanapiga kazi kisawasawa. Nimefikiri pengine kama kuna binadamu ambao sio rijali au sio ridhiki basi pengine hata huyu Jogoo anaweza kua wa dizaini hiyo pia. Au pia inaweza kua ameumbwa na aibu sana au ni domo zege labda. Au anaweza akawa anatokea jamii ya kuku ambao hawapendi sana mambo ya kupandana pandana. Angekua binadamu ningesema ameokoka (mlokole) lakini kwa kuku sidhani.
Wale wazoefu msaada wenu unahitajika please, maana miezi zaidi ya mitatu sijapata hata yai la kuonja na ninawahudumia gharama kubwa tu za bure.


Ahsanteni
nimecheka sana, hata nikajuta ni kwanini nilichelewa kuusoma huu uzi wako, sijawahi kufurahi kama siku hii ya leo inawezekana kwa muda wa mwaka mmoja sasa, lakini nashukuru mpaka sasa kuna wadau wamekujibu vizuri kitaalamu.
 
Unatakiwa kuhakikisha kuku wanapata balanced diet, unawapa dawa ya minyoo na chanjo zote muhimu.
Nina kuku 15 tu wanaotaga lakini kila siku nakusanya mayai 12 na ni hawa wa kienyeji chotara.
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom