Kukosewa kwa jina kwenye chet cha Necta

Eshacky

JF-Expert Member
Apr 26, 2011
965
244
Ndugu wa Jf, wiki iliyopita nimeenda kuchukua result slip yangu ya form 6 shuleni tambaza,baada ya kutolewa ili niendelee na process za kuomba chuo. Cha ajabu nimekuta hakuna heruf ya kat mfano. Eshack "d" Msamvu. Je taratibu na kufuatiria kwa marekebisho zipoje, na vip haziwez kunichelewesha hizi process za chuo. Naomba msaada wa maelekezo yenu kaka na dada zangu wenye kujua..
Nawasilisha.
 
Nasikia kurekebisha huchukua hadi miezi sita, wewe endelea na chuo hawawez kukuzngua kwa kosa hilo.
 
Nasikia kurekebisha huchukua hadi miezi sita, wewe endelea na chuo hawawez kukuzngua kwa kosa hilo.
navy, cunajua cku hz unajiandiksha online, nikiweka zle index namba za O and A-level, majina hayamatch, so inakataa..
 
Hapo kuna option 2:
1. Unaweza ukaapply tcu kama jina lako lilivyo kwenye vyeti vyako bila kuongeza letter.
2: wakati unajaza fom za heslb ndipo unaweza kuatach hyo hrf ilyosahaulka.
my take: it is not the fnal solution.
 
Hapo kuna option 2:
1. Unaweza ukaapply tcu kama jina lako lilivyo kwenye vyeti vyako bila kuongeza letter.
2: wakati unajaza fom za heslb ndipo unaweza kuatach hyo hrf ilyosahaulka.
my take: it is not the fnal solution.
tnx kwa ushaur,lakin tcu kwa sasa unaandika index number na c jina, na juzi nilitaka kufungua account ikakataa baada kuchunguza ndo nikakuta hilo tatizo.
 
Ndugu,nijuavyo mimi ni kuwa hawatakaa wagundue tatizo kirahisi. Pia naona kidogo haukutaka kuwa mkweli kwani kama ungekuwa unapeleka physically ndo mtu angekwambia ivo lakini kwa kujua tu index number bila hata jina tayari wanajua jina likoje.

Nakushauri urejiste kwa kutumia majina yaliyo kwenye cheti cha form4, baadae ukaombe kubadili iyo karatasi.

Ikumbukwe result slip si cheti, kwa iyo mpaka cheti kinatoka iyo result slip itakuwa inaexpire na jina la cheti litakuwa lile uliloandika wakati unajiandikisha kufanya mtihani.

Usihofu maana matokeo ya f4 ndo yaliyokupeleka fom5 kwa iyo baraza wana jina lako sahihi. Cha muhimu maelezo yako yote uyaweke ktk jina la fom4 na ndo cheti kinachofanywa reference kwa mkopo, kwa miaka yote ukaayo chuoni.

Ndugu ukianza kujichanganya na kuwaeleza wanaoandikisha mfano mkopo n.k utajikwamisha. Ukisha apply,nenda baraza la mitihani upate kopi nyingine.

Kuna mchangiaji kasema vyeti hutumia miezi6, ila nadhani tatizo lako ni results slip, ambayo ndani ya siku1 au2 unaipata pale baraza.

Note:
Kama ukiangalia matokeo yako ya f6 ktk website ukakuta jina limekosewa ujue hata cheti kitakuja kwa jina ilo,ila ukiangalia moe web,au necta website ukakuta jina liko sawa, basi tulia usubiri cheti chako.

Ni ushauri wangu tu, na nakutakia mafanikio ila usipaniki kwa tatizo ilo mdogo wangu.
 
Thnx a lot gsan, kuhusu kuwaona physical kwa kuwa nimechukua result slip ijumaa, nimeona niende j3 nikafuatilie, ila mara ya kwanza nilijarbu kwny mtandao na ikaandìka hvyo, uzur n kwamba hata living certificate ya f6 ina jina sahih, kwa hyo n uthibitisho tosha.
Asante kwa msaada mzur wa mawazo, endapo nitakwama ntakuja kuwajulish wana jamvi wenzangu.
 
ni tatizo linatatulika ila linahitaji muda. cha muhimu anza kupata barua toka kwa Mkuu wa shule ulosoma high level then uende baraza la mitihani
 
Necta wanapoleta result slip shuleni,pia huleta na form ya kuhakiki kama majina yaliyotumika ni sahihi. Cha kufanya ni kuuarifu uongozi wa shule,kisha wao watajaza fomu ya kurekebisha jina,ni kweli itachukua muda hadi warekebishe,ila kwa chuo wewe omba kama jina lako lilivyo kwenye cheti cha kidato cha nne.
 
Ndugu wana Jf, lile tatizo langu hatimaye nimefikia pazur ,baada ya kuchukua barua toka shule na vielelezo nimeweza peleka necta, na wameniambia watatoa tena baada ya mwez hiyo result slip yangu, kuhusiana na mtandao wa tcu kukataa mwanzon, nimeweza kwenda ofis zao na kunirekebishia ili niweze kuapply, hvyo pind necta watakapofanya marekebisho nao watayapokea. shukrani kwa wanajamvi kwa ushaur wenu, tuendelee kusaidiana ktk namna moja ama nyengine..
Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom