tobodunda
Member
- Sep 4, 2018
- 53
- 85
Wakati mwingine unajiuliza maswali
1. Wanasiasa na agenda zao za kisiasa zinaisaidiaje nchi?
2. Mambo wanayoyafanya yanawasaidia vp wananchi wanowaongoza?
Maswali hayo mawili yamepelekea kubaini uwepo wa makundi mawili ya wanasiasa
1. Wanasiasa wapenda maendeleo.
2. Wanasiasa wachumia tumbo.
KUNDI NAMBA 1.
kundi hili la kwanza ambalo linaongozwa na Rais wa nchi JOHN MAGUFULI kwa tathmini ya haraka haraka limejikita katika kuhakikisha linaandika historia mpya ya nchi. Miradi ya maendeleo inayotekelezwa na kusimamiwa na kundi hili haijapata kutokea nchini. Kundi hili limekua mstari wa mbele kukemea na kupambana kwa vitendo masuala ya rushwa na ubadhirifu wa mali za umma, kuwawajibisha wasiowajibika na kuweka maslahi ya wananchi mbele.
KUNDI NAMBA 2
Hoja yangu kwa kiasi kikubwa itajikita katika kundi hili. Kundi hili limekua mstari wa mbele kukwamisha jitihada mbalimbali zinazofanywa na kundi la kwanza. Kundi hili linaundwa na wanasiasa wengi wa Upinzani na wachache wa Chama tawala. Wajumbe wa kundi hili walio wengi ni wale ambao wameneemeka sana na tawala zilizopita kwa janja janja nyingi. Kundi hili hapo awali lilikuwa na nguvu sana kwani katika vikao vingi vya maamuzi lilikuwa na wajumbe wengi wa kupitisha agenda zao.
Kundi hili ilifikia hatua ambayo wakisema NO basi hakuna jambo lolote litalofanyika katika nchi hii. Agenda kubwa ikiwa ni kulinda maslahi yao na kutunisha vitambi vyao. Kuna nyakati amabazo tawala zilizopita zilipotaka kufanya maamuzi yanayowagusa walitishia na kuahidi kwamba nchi hii haitatawalika. Hapo awali wajumbe wengi wa kundi hili walikuwa ni wanasiasa wazee wakifuatiliwa kwa karibu na wafanyabiashara kama wawezeshaji wakuu na wanufaikaji wa agenda za kundi hili. Kwa sasa kundi hili limepata wajumbe wapya tena vijana haswaa ambao damu inawachemka, wakitamani kundesha ma-HUMMER na magari mengine ya kifahari. Wakitamani kuwa na maisha mazuri kuliko hata wazee waliowakuta katika kundi hili.
HATMA YA KUNDI LA PILI KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA TANO
Tangu utawala wa awamu ya tano umeingia madarakani, Kundi hili limeathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na kwamba maslahi yao yamebanwa, hawana tena sauti katika vikao vya maamuzi, cake waliyoitegemea haipo tena, hawawezi tena kushinikiza uongozi uliopo kubeba agenda zao na kubwa kuliko hawathaminiki tena kwa Uongozi wa juu wa Serikali.
Wajumbe wa kundi hili wamekuwa wakisononeka, wakinung'unika, wakifadhaika na kusikitikia hatua zilizochukuliwa na Kundi namba 1. Hawaamini kinachotokea, wamebaki kulalamikia maamuzi ya kwanini walimpuuza na kuruhusu Magufuli kuingia madarakani. Wamekuwa wakihaha huku na kule, kufanya hili na lile kutafuta huruma za kundi la kwanza pasipo mafanikio. Imebidi wabadilishe mbinu ya mchezo, mchezo ambao umemilikiwa na kundi la kwanza na wao wamebaki kuwa watazamaji.
Mipango mbalimbali imesukwa na kundi la pili kuhakikisha hata kwa kucheza rafu wanairudisha nafasi yao katika game.
Wameazimia hata ikibidi kuiuza nchi ili warudishe hadhi yao watafanya. Wamekuwa wakisafiri nchi za Ulaya na Marekani kushawishi nchi hizo kusitisha ushirikiano na Tanzania ili tu kuiadhibu Serikali. HAWA NDIO WANASIASA HASWAA WACHUMIA TUMBO.
Ushawahi kujiuliza kwanini hawa vijana badala ya kuisaidia Serikali wanashinda mitandaoni kuwauliza World Bank jambo hili na lile. Kuwauliza EU hili na lile. Kufanya safari katika nchi za Ulaya kila uchao kwa madai eti wanenda kuonana na marafiki zao. Chuki wanayoenda kuijenga huko haijawah tokea tangu nchi hii imeumbwa. Inafika kipindi unajiuliza hivi hawa ni kweli watanzania? Ni kweli wameaminiwa na nchi yao kufanya upuuzi huo? Ni kweli njaa zimewabana kiasi cha kuwa tayari hata kuona wananchi wakitaabika baada ya misaada kukatwa?
Wao hilo hawajali. Wanaangalia vitambi vyao vimeathirika kwa namna gani. Hawana hofu kwa kuwa mifuko yao imetunishwa kwa harakati zao. Hawamfikirii kabisa mtanzania anayetaabika kutokana na mradi wa maji kukwama. Wanafurahia kuona jamii ikitaabika huku wakisema "Ngoja tuone sasa kama nchi itatawalika, Tuone Sisi na yeye nani zaidi" Je ndo kazi tuliyowapa wakatusaidie bungeni??
Mimi ntaanza na Mbunge wangu ZITTO KABWE. Aje atueleze kwetu Kasulu ni kwa kiasi gani Mimi mwananchi wa Kasulu nafaidika kutokana na yeye kufurahia Bank ya Dunia kusitisha ufadhili wa mradi wa elimu? Ni vp mm nafaidika kutokana na Bank ya dunia kusitisha ufadhili wa mradi wa maji? Lakini ntataka aeleze tena bila kupepesa macho kwanini kafurahia suala la ushoga?
WANASIASA WACHUMIA TUMBO NI KANSA YA TAIFA...DHAMBI ZA USALITI NA DHULUMA HAZITAWAACHA SALAMA.
1. Wanasiasa na agenda zao za kisiasa zinaisaidiaje nchi?
2. Mambo wanayoyafanya yanawasaidia vp wananchi wanowaongoza?
Maswali hayo mawili yamepelekea kubaini uwepo wa makundi mawili ya wanasiasa
1. Wanasiasa wapenda maendeleo.
2. Wanasiasa wachumia tumbo.
KUNDI NAMBA 1.
kundi hili la kwanza ambalo linaongozwa na Rais wa nchi JOHN MAGUFULI kwa tathmini ya haraka haraka limejikita katika kuhakikisha linaandika historia mpya ya nchi. Miradi ya maendeleo inayotekelezwa na kusimamiwa na kundi hili haijapata kutokea nchini. Kundi hili limekua mstari wa mbele kukemea na kupambana kwa vitendo masuala ya rushwa na ubadhirifu wa mali za umma, kuwawajibisha wasiowajibika na kuweka maslahi ya wananchi mbele.
KUNDI NAMBA 2
Hoja yangu kwa kiasi kikubwa itajikita katika kundi hili. Kundi hili limekua mstari wa mbele kukwamisha jitihada mbalimbali zinazofanywa na kundi la kwanza. Kundi hili linaundwa na wanasiasa wengi wa Upinzani na wachache wa Chama tawala. Wajumbe wa kundi hili walio wengi ni wale ambao wameneemeka sana na tawala zilizopita kwa janja janja nyingi. Kundi hili hapo awali lilikuwa na nguvu sana kwani katika vikao vingi vya maamuzi lilikuwa na wajumbe wengi wa kupitisha agenda zao.
Kundi hili ilifikia hatua ambayo wakisema NO basi hakuna jambo lolote litalofanyika katika nchi hii. Agenda kubwa ikiwa ni kulinda maslahi yao na kutunisha vitambi vyao. Kuna nyakati amabazo tawala zilizopita zilipotaka kufanya maamuzi yanayowagusa walitishia na kuahidi kwamba nchi hii haitatawalika. Hapo awali wajumbe wengi wa kundi hili walikuwa ni wanasiasa wazee wakifuatiliwa kwa karibu na wafanyabiashara kama wawezeshaji wakuu na wanufaikaji wa agenda za kundi hili. Kwa sasa kundi hili limepata wajumbe wapya tena vijana haswaa ambao damu inawachemka, wakitamani kundesha ma-HUMMER na magari mengine ya kifahari. Wakitamani kuwa na maisha mazuri kuliko hata wazee waliowakuta katika kundi hili.
HATMA YA KUNDI LA PILI KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA TANO
Tangu utawala wa awamu ya tano umeingia madarakani, Kundi hili limeathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na kwamba maslahi yao yamebanwa, hawana tena sauti katika vikao vya maamuzi, cake waliyoitegemea haipo tena, hawawezi tena kushinikiza uongozi uliopo kubeba agenda zao na kubwa kuliko hawathaminiki tena kwa Uongozi wa juu wa Serikali.
Wajumbe wa kundi hili wamekuwa wakisononeka, wakinung'unika, wakifadhaika na kusikitikia hatua zilizochukuliwa na Kundi namba 1. Hawaamini kinachotokea, wamebaki kulalamikia maamuzi ya kwanini walimpuuza na kuruhusu Magufuli kuingia madarakani. Wamekuwa wakihaha huku na kule, kufanya hili na lile kutafuta huruma za kundi la kwanza pasipo mafanikio. Imebidi wabadilishe mbinu ya mchezo, mchezo ambao umemilikiwa na kundi la kwanza na wao wamebaki kuwa watazamaji.
Mipango mbalimbali imesukwa na kundi la pili kuhakikisha hata kwa kucheza rafu wanairudisha nafasi yao katika game.
Wameazimia hata ikibidi kuiuza nchi ili warudishe hadhi yao watafanya. Wamekuwa wakisafiri nchi za Ulaya na Marekani kushawishi nchi hizo kusitisha ushirikiano na Tanzania ili tu kuiadhibu Serikali. HAWA NDIO WANASIASA HASWAA WACHUMIA TUMBO.
Ushawahi kujiuliza kwanini hawa vijana badala ya kuisaidia Serikali wanashinda mitandaoni kuwauliza World Bank jambo hili na lile. Kuwauliza EU hili na lile. Kufanya safari katika nchi za Ulaya kila uchao kwa madai eti wanenda kuonana na marafiki zao. Chuki wanayoenda kuijenga huko haijawah tokea tangu nchi hii imeumbwa. Inafika kipindi unajiuliza hivi hawa ni kweli watanzania? Ni kweli wameaminiwa na nchi yao kufanya upuuzi huo? Ni kweli njaa zimewabana kiasi cha kuwa tayari hata kuona wananchi wakitaabika baada ya misaada kukatwa?
Wao hilo hawajali. Wanaangalia vitambi vyao vimeathirika kwa namna gani. Hawana hofu kwa kuwa mifuko yao imetunishwa kwa harakati zao. Hawamfikirii kabisa mtanzania anayetaabika kutokana na mradi wa maji kukwama. Wanafurahia kuona jamii ikitaabika huku wakisema "Ngoja tuone sasa kama nchi itatawalika, Tuone Sisi na yeye nani zaidi" Je ndo kazi tuliyowapa wakatusaidie bungeni??
Mimi ntaanza na Mbunge wangu ZITTO KABWE. Aje atueleze kwetu Kasulu ni kwa kiasi gani Mimi mwananchi wa Kasulu nafaidika kutokana na yeye kufurahia Bank ya Dunia kusitisha ufadhili wa mradi wa elimu? Ni vp mm nafaidika kutokana na Bank ya dunia kusitisha ufadhili wa mradi wa maji? Lakini ntataka aeleze tena bila kupepesa macho kwanini kafurahia suala la ushoga?
WANASIASA WACHUMIA TUMBO NI KANSA YA TAIFA...DHAMBI ZA USALITI NA DHULUMA HAZITAWAACHA SALAMA.