Kukamatwa kwa Dkt. Mashinji na Viongozi wengine wa CHADEMA: Maoni ya Dkt. Slaa

Ni Kwanini unaamini kwamba hawakuomba kibali je umeshindwa kuwapigia na kuwauliza au una kinyongo nao tangia walipokuudhi?

Kama wanakamatwa na kushinda kesi mahakamani unajifunza nini juu ya aliyewakamata? Umesema Watu waongee fact ambalo Ni jambo jema unadhani wewe umeongea fact gani? Uko Canada na unajua siasa za vyama vingi Tanzania Ni Kweli hukusikia Raisi aliposema hakuna mikutano ya hadhara?

Wakati ule unatangaza list of shame ulipata kibali? Unadhani leo unaweza kuwa na nafasi hiyo kama hiyo bila kuwekwa ndani? Unadhani wakati wote ulipowekwa ndani ulikuwa hukufuata taratibu?

Ndipo Chama kilipofika baada ya kuondolewa viongozi makini kwa bei ya kunde kisa njaa ya siku moja.Dr.Slaa kama ilivyo jadi yake ametoa somo. Kaomba pia aelimishwe kwenye maeneo tunayoona kuwa kwa hoja aliyotoa kapitwa na wakati.

Kama viongozi waliokamatwa walitimiza matakwa yote ya kisheria waweke hadharani taarifa zao.Kama polisi walikosea kawapa tahadhari na madhara ya hatua hizo.Nini kinakufanya utukane au uhoji mahali alipo? je ukiwa nje ya Tanzania unauza utanzania wako?
 
Dk.slaa nilikua nakupenda ila CCM imekupenda zaidi. Ona sasa hivi unawatetea CCM.

JPM alizuia mikutano ya siasa mpaka 2020 police wanatekeleza sheria ya rais kifungu kidogo.

Usiku mwema, msalimie mkeo

Hebu soma hapa mkuu pengine utapata hoja nzuri.

...Kauli ya Rais si sheria na haiwezi kuvunja Sheria iliyotungwa na Bunge ( Sheria na 5 ( RE 2002 ni sheria halali iliyotungwa na Bunge). Ninaamini kabisa kama kuna amri yeyote ya Rais, chama makini kingeli " challenge" amri hiyo chini ya vipengele vya sheria vya " Prerogative Orders za Certiorari, Prohibimus na Mandamus".

Wanasheria wanajua vizuri matumizi ya sheria hizo katika kudhibiti matumizi mabovu ya mamlaka ya kuiongozi yeyote. Hivyo, tusitafute majibu mepesi katika " udikteta". Ni muda mwafaka sasa kutafuta majibu sahihi penginepo.
 
Siku wewe na mkeo mlipopigwa mabomu Arusha hamkuwa na kibali???? Si ulisema umeacha siasa mkuu? Mbona unataka kuaminisha watu yale maneno kwamba ulikuala billion 4 na kujipa uhamisho kwenda prime minister trudeau?
Alisema ameacha siasa au siasa za vyama?
CHADEMA LOWASA muwe makini kumsikiliza Daktari.
 
Siyo kama hajui ila anajifanya tu.

...Kauli ya Rais si sheria na haiwezi kuvunja Sheria iliyotungwa na Bunge ( Sheria na 5 ( RE 2002 ni sheria halali iliyotungwa na Bunge). Ninaamini kabisa kama kuna amri yeyote ya Rais, chama makini kingeli " challenge" amri hiyo chini ya vipengele vya sheria vya " Prerogative Orders za Certiorari, Prohibimus na Mandamus". Wanasheria wanajua vizuri matumizi ya sheria hizo katika kudhibiti matumizi mabovu ya mamlaka ya kuiongozi yeyote. Hivyo, tusitafute majibu mepesi katika " udikteta". Ni muda mwafaka sasa kutafuta majibu sahihi penginepo.

AMehoji wanasheria wa chama wanashauri vipi uongozi wa CHADEMA? au wanasubiri kesi?

Jibuni hoja.

Hivi LOWASA kawafanyaje CHADEMA siku hizi?
 
Hee Mzee unatia aibu, nilikushangaa siku ile uliyojitokeza kumshambulia EL ukiwa mamluki wa CCM. Lkn leo nimekushangaa tena kuzungumza jambo unalolijua na unauzoefu nalo tena sana kinyume na ukwwli wake.

EL alipokelewa ukiwapo na wewe, hukupinga, mkakaa kumthibitisha hukupinga, akatangazwa mgombea ukateleza teleza baada ya mwezi ukaja na msemo huewzi kushirikiana na mashetani, majizi na mengi uliyasema. Binti anachumbiwa na jambazi unakubali inatangazwa ndoa baba unakubali siku ya ndoa unamtoa mwanao aolewe unakubali na kushangilia. Jambazi na Binti wakiwa honeymoon baba unaanza kusema sikubali yule jamaa ni jambazi.

Leo tena hujui eti tawala za hapa ati kuna vibali na utoaji taarifa kweli nafsi yako inakuthibitishia hilo kulitilia shaka mpk ulizungumze mbele ya hadhara.
 
Dr. yaani watu wana kikao cha ndani ni lazima watoe taarifa police? kwani lengo la kutoa taarifa police si ni kwa ajili ya ulinzi? je kama wahusika hawahitaji huo ulinzi je? pia tamko la rais kuzuia mikutano ya vyama vya siasa hapa nchini toka kwa rais sio siri.
 
Kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Hadi Mzee Slaa leo anayasema haya wakati alipigwa virungu na mabomu ya machozi ya kutosha.

Labda tusaidie kuuliza kwa wanaCCM wenzio kwa vile una kadi, je ni nini siri ya wao mikutano yao kupewa kibali, ya ndani na ya nje wakati vyama vingine havipati kibali?
 
Kasahau kipindi mchumba Josephine wanataka waoane zengwe lilioanzishwa na kina Sophia Simba wakishirikiana na Rose Kamili pale bungeni sembuse mambo ya vibali?

Nasikitika kuna kipindi huyo mzee nilikuwa na mu idolise namuona mtu wa maana katika siasa, nikisoma posts zake kama hizi naona ule ni muda niliopoteza kuwa na role model wa aina hii
Role model wako sasa ndo kawa LOWASA au KINGUNGE?
 
f3555d85e0b38c03ec99da9ce8d8fdfd.jpg
 
Kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Hadi Mzee Slaa leo anayasema haya wakati alipigwa virungu na mabomu ya machozi ya kutosha.

Labda tusaidie kuuliza kwa wanaCCM wenzio kwa vile una kadi, je ni nini siri ya wao mikutano yao kupewa kibali, ya ndani na ya nje wakati vyama vingine havipati kibali?
Hebu msaidie Daktari kumuonesha kwanza kama waliomba hivyo vibali. (Hiyo ndio hoja yake)
 
Dr anauma na kupuliza lakin anakua kila kitu ila Ukweli Ukawa huyu Dr slaa ndio alikua anatosha ile nafasi ya Katibu Mkuu..

Naamini yeye angekua ameweka mambo sawa sasaiv katika hii kamata kamata....mkubali hapa mlipoteza jembe
 
Dk.slaa nilikua nakupenda ila CCM imekupenda zaidi. Ona sasa hivi unawatetea CCM.

JPM alizuia mikutano ya siasa mpaka 2020 police wanatekeleza sheria ya rais kifungu kidogo.

Usiku mwema, msalimie mkeo
Matamshi ya Rais siyo sheria ninavyoona ni kweli pana umuhimu wa kuangalia upya hivyo vifungu alivyojaribu kutufafanulia tukijadili mambo haya kwa kinyongo hatufiki popote pale i hope hii post itasomwa na pande zote na kila mmoja atakuwa amejifunza kitu na vilevile tukumbuke kuwa "BANIANI MBAYA KIATU CHAKE DAWA".

DR inawezekana kuna aliyoyafanya ikaonekana hayapendezi but bado ni msomi na nguli wa sheria ambaye mawazo yake yanaweza tumika kuleta mustakali mpya wa sura ya taifa letu na matokeo chanya yatakayoimarisha demokrasia na misingi ya haki.

Na pia tukumbuke ugumu alioupitia akiwa katibu mkuu wa chama chake ambapo alipita nchi nzima akimnadi Mh. Lowasa kama fisadi alafu ghafla arudi tena kumnadi kama mgombea wa chama chake..ilikuwa ngumu Kumeza!

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Pamoja na mazingira ya kisiasa kwa upinzani yamekuwa magumu, lkn upinzani umeshindwa kubadilika kutokana na mazingira.

Kwa sasa dunia ni ya digitali, Jamii kubwa ya watanzania wanatumia internet.

Chadema na upinzani wanaweza fanyia mikutano yako kupitia mitandao na kueneza itikadi yao, kueleza mazaifu ya serikali na kujitangaza zaidi.

Kuendelea kulalamika, haitosaidia mwisho wa siku uchaguzi unakaribia.
Ni Watanzania wangapi wana access na internet? Tatizo la upinzani katika chaguzi limekuwa vijijini, je huko unafikaje kwa internet ikiwa ndoo ya maji haipataikani. Tuzungumzie mambo kwa uhalisia

Laiti ingekuwa internet ni rahisi kiasi hicho CCM wasingekuwa na haja ya kauznguka
Iweje wao wafanya mikutano ya ndani na nje halafu ushauri wengine 'digitali'

Pili, ni ukosefu wa waledi unaponyang'anywa haki ukafikiri mbadala badala ya kuipigania.

Nyerere alikuwa na kazi nzuri tu wakati wa ukoloni, aliamu kuiacha kwasababu aliamini kuna haki inakosekana. Ndivyo wazee wetu walivyopigania uhuru

Mikutano ya siasa ni takwa na haki ya kikatiba. Unaposhauri watu waiache haki hiyo unakaribisha matatizo zaidi ya ufumbuzi. Ipo siku utaamka asubuhi na kuambiwa usitamke neno siasa la sivyo utafungwa nawe utatafuta njia ya 'digitali'

Lakini pia digitali ipi unayoongelea ikiwa kuna sheria zimewekwa za mtandao kuidhibiti?
 
Ushahidi mzuri mkutano wako wa kufungua Tawi huko Iringa Nyororo mpaka ikapelekea kifo cha Mwangosi, polisi walichokifanya unakijua, ufunguzi wa tawi na mkutano wa ndani ya tawi.
Well said mkuu. Dr Slaa tungeomba ufafanue kifo cha Mwangosi ukiwepo kama katibu mkuu, je hukufuata matakwa ya sheria za mikutano ya ndani? Tusaidie hili tafadhali
 
1.Hakuna amri ya raisi (presidential decree) kuwa ni marufuku kufanya mikutano ya vyama vya siasa ndani na/au ya nje.Ni kweli hakuna kwakweli,na kama ipo basi wanasheria waichallenge mahakamani hiyo amri kukiuka katiba na sheria ya vyama vya siasa.Hapa kuna mambo ya kujifunza kabla ya kutumia jazba.Je ili kauli ya raisi ikidhi vigezo vya kuitwa 'presidential decree' ni hatua zipi inatakiwa ipitie?Bila kupitia hizo hatua inabaki kuwa kauli ya kisiasa na hivyo yapaswa kushuhulukiwa kisiasa?

2. Mikutano ya ndani haiitaji kibali.Inahitaji kutoa taarifa. Kuzuiwa kufanyika maana yake kuwe ndani ya sheria na sababu zinazoweza kusababisha kuzuiwa zimewekwa hapo juu. Na aliyezuia anawajibika kutoa sababu na kupanga siku/muda mwingine na/au mahali pengine. Nje ya hapo ni ukiukwaji wa sheria.Je hili limesimamiwa kwa kiwango gani?

3. Mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa inahitaji kibali.Kuzuiwa maana yake kuwe ndani ya sheria na sababu zinazoweza kusababisha kuzuiwa zimewekwa hapo juu.Na aliyezuia anawajibika kutoa sababu na kupanga siku/muda mwingine na/au mahali pengine. Nje ya hapo ni ukiukwaji wa sheria.Je hili limesimamiwa kwa kiwango gani?
 
Back
Top Bottom