Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
Kutokea kuanza kwa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2010, mgombea urais wa CCM Mhe Jakaya Kikwete na wapiga debe wake wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kukwepa hoja zinazosababisha umaskini wa watanzania na kuifanya Tanzania kuendelea kuwa nchi maskini. Ni katika mkakati huo CCM imegoma kushiriki midahalo mbali mbali waka huu.
Hoja ambazo zinawasababishia watanzania umaskini na Tanzania kuendelea kuwa maskini pamoja na (a) Serikali ya CCM kushindwa kukusanya kodi ipasavyo kutokana na viongozi wake wengi kuwa na mashirikiano na wawekezaji na wafanyabisahara wakubwa hapa. (b) Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazopata mapato ya chini kabisa kutoka kwenye madini yake Dhahabu, Almasi, Tanzanite n.k. (c) Serikali kushindwa kukusanya mapato ya kutosha kutoka katika vivutio mbali mbali vya utalii, ikiwemo uwindaji wa kitalii, mbuga za wanyama, mahoteli, fukwe n.k.
Mapungufu hayo pampja na mengine zimeifanya Serikali ya Tanzania ambyo imekuwa ikiongozwa na CCM kwa talkribani mika 49 kuwa na uwezo mdogo sana wa kifedha kumudu kuwapatia watanzania huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya, maji safi n.k. Hali hii imeilazimu Serikali ya CCM kuwa na sera za uchangiaji huduma za elimu, afya na upatikanaji maji safi; japo huduma inayotolewa ni ya kiwango cha chini sana.
Kutokana na watanzania wengi kukosa fedha za kuchangia afya na upatikanaji maji safi, na huduma zenyewe kuwa ni za ya viwango vya chini sana maelfu ya watanzania wamekuwa wakipoteza maisha kila mwaka kwa maradhi ya aina mbali mbali kama vile malaria, kipindipindu, kuhara n.k ambayo yangeweza kuzuilika laity kama Serikali ingekuwa imejijengea uwezo wa kuboresha miundo mbinu na upatikanaji huduma za afya.
Kwa upande wa elimu CCM imeamua kuwafanya mamilioni ya watanzania kuwa watumwa ndani ya nchi yao kwa kuwakusanya watoto wa wafanyakazi na wakulima na kuwadanganya kuwa inawapatia elimu katika vyumba vya madarasa visivyo na waalimu, madawati, vitabu vya kiada, madaftari, maabara n.k.
Wakati haya yakitokea watoto wa viongozi na watendaji wa Serikali ya CCM wanasoma katika shule za binafisi za kulipia ambazo zina waalimu na mahitaji yote muhimu. Watoto wao wanakwedna shule kwa magari ya serikali, mashirika ya umma na mabasi ya shule ya kulipia. Fedha zote hizi zinatoka katika mifuko ambayop iltakiwa kuwahudumia wanyonge.
Kutokana na Serikali ya CCM kushindwa kukusanya mapato kama ilivyotajwa hapo juu imekuwa ikiweka kodi kubwa katika bidhaa mbali mbali ikiwemo mafuta kwa nia ya kupata fedha za kujenga barabara. Kodi hizi husababisha mfumuko wa bei hapa nchini na kuongeza umaskini wa watanzania.
Moja ya mbinu ambayo CCM imekuwa ikitumia kukwepa hoja zilizotajwa hapo juu staili ya kutoa ahadi hewa lukuki ambayo inaonekana kuwachanganya wananchi na wapinzani pia. Hali hii inawafanya wapinzani waache kujenga hoja zenye kuibana CCM kuhusu ilivyoshindwa kusimamia na kutumia utajiri na raslimali zilizopo Tanzania kwa manufaa ya watanzania na badala yake wapinzania wanaanza kucheza ngoma ya CCM ya kutoa ahadi lukuki.
Ili kukabiliana na Propaganda za CCM, wagombea wake na viongozi wake mbali mbali ambao wanapatiwa fursa zaidi na vyombo vingi vya habari, DR Slaa na wagombea wote wa CHADEMA wanatakiwa kuwafahamisha watanzania mara kwa mara yafuatayo:-
(i) aina ya madini na ujazo yaliyochimbwa na kuondoka hapa nchini kutoka mwaka 2005 hadi sasa.
(ii) kiasi cha fedha kilichopatikana kama mrahaba duni uliowekwa na Serikali ya CCM.
(iii) kiasi cha fedha Serikali ya CCM ilichopokea kwa niaba ya watanzania kutoka 2005 hadi sasa kutoka kwenye madini.
(iv) Kiasi cha Mrahaba ambao Serikali ya CHADEMA ingeweka kutoka katika madini husika.
(v) kiasi cha fedha ambacho kingeweza kupatikana chini ya utaratibu huo wa CHADEMA kutoka katika madini yaliyochimbwa kati ya 2005 hadi sasa.
(iv) na fedha hizo zingeweza kujenga miundo mbinu, shule, hospitali n.k ngapi.
2) Kiasi cha fedha wafanyabiashara wanachokwepa kila mwaka kutoka 2005 hadi sasa. Na fedha hizo zingeweza kufanya nini katika utoaji huduma za jamii, ujenzi wa miundo mbinu n.k?
3) Kiasi cha fedha kinachokosekana kukusanywa kupitia sekta ya utalii kutokea 2005 hadi sasa. Na fedha hizo zingeweza kufanya nini katika utoaji huduma za jamii, ujenzi wa miundo mbinu n.k?
NB: Dr Slaa na wagoimbea wote wa CHADEMA nchi nzima wajikite katika kuwafafanulia na kuonyesha watanzania kuwa inawezekana watoto wote wa Tanzania wakapata elimu bure kutoka chekechea hadi Kidatu cha Sita;
na kodi ya vifaa vya ujenzi vinavyotumiwa na wanyonge yaani saruji, bati, nondo, misumari n.k vinavyoweza kupunguzwa bila ya kuathiri uendeshaji wa Serikali baada ya CHADEMA kusimamia mukusanyaji apato ya Serikali kama ilivyoonyeshwa hapo juu.
Timu ya Kampeni ya CHADEMA ikumbuke kuwa binadamu ameumbwa kusahau mara kwa mara. Hivyo huhitaji kukumbushwa mara kwa mara. Hivyo watumie kipindi hiki cha Kampeni kurudia rudia mambo haya msingi hususan usimamizi wa madini, kodi, utalii n.k ili wananchi waweze kukumbuka na kutoa adhabu kwa CCM tarehe 31 Oktoba 2010.
Mwana JF yeyote anayeweza kutupatia hizi takwimu hapa atakuwa ametoa msaada mkubwa sana kwa wagombea mbali mbali wa CHADEMA ili kutusadia kuwaeleza watanzania wenzetu kiini cha umaskini wetu na kwanini tunalazimika kufanya mabadiliko kupitia uchaguzi wa mwaka 2010.
Hoja ambazo zinawasababishia watanzania umaskini na Tanzania kuendelea kuwa maskini pamoja na (a) Serikali ya CCM kushindwa kukusanya kodi ipasavyo kutokana na viongozi wake wengi kuwa na mashirikiano na wawekezaji na wafanyabisahara wakubwa hapa. (b) Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazopata mapato ya chini kabisa kutoka kwenye madini yake Dhahabu, Almasi, Tanzanite n.k. (c) Serikali kushindwa kukusanya mapato ya kutosha kutoka katika vivutio mbali mbali vya utalii, ikiwemo uwindaji wa kitalii, mbuga za wanyama, mahoteli, fukwe n.k.
Mapungufu hayo pampja na mengine zimeifanya Serikali ya Tanzania ambyo imekuwa ikiongozwa na CCM kwa talkribani mika 49 kuwa na uwezo mdogo sana wa kifedha kumudu kuwapatia watanzania huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya, maji safi n.k. Hali hii imeilazimu Serikali ya CCM kuwa na sera za uchangiaji huduma za elimu, afya na upatikanaji maji safi; japo huduma inayotolewa ni ya kiwango cha chini sana.
Kutokana na watanzania wengi kukosa fedha za kuchangia afya na upatikanaji maji safi, na huduma zenyewe kuwa ni za ya viwango vya chini sana maelfu ya watanzania wamekuwa wakipoteza maisha kila mwaka kwa maradhi ya aina mbali mbali kama vile malaria, kipindipindu, kuhara n.k ambayo yangeweza kuzuilika laity kama Serikali ingekuwa imejijengea uwezo wa kuboresha miundo mbinu na upatikanaji huduma za afya.
Kwa upande wa elimu CCM imeamua kuwafanya mamilioni ya watanzania kuwa watumwa ndani ya nchi yao kwa kuwakusanya watoto wa wafanyakazi na wakulima na kuwadanganya kuwa inawapatia elimu katika vyumba vya madarasa visivyo na waalimu, madawati, vitabu vya kiada, madaftari, maabara n.k.
Wakati haya yakitokea watoto wa viongozi na watendaji wa Serikali ya CCM wanasoma katika shule za binafisi za kulipia ambazo zina waalimu na mahitaji yote muhimu. Watoto wao wanakwedna shule kwa magari ya serikali, mashirika ya umma na mabasi ya shule ya kulipia. Fedha zote hizi zinatoka katika mifuko ambayop iltakiwa kuwahudumia wanyonge.
Kutokana na Serikali ya CCM kushindwa kukusanya mapato kama ilivyotajwa hapo juu imekuwa ikiweka kodi kubwa katika bidhaa mbali mbali ikiwemo mafuta kwa nia ya kupata fedha za kujenga barabara. Kodi hizi husababisha mfumuko wa bei hapa nchini na kuongeza umaskini wa watanzania.
Moja ya mbinu ambayo CCM imekuwa ikitumia kukwepa hoja zilizotajwa hapo juu staili ya kutoa ahadi hewa lukuki ambayo inaonekana kuwachanganya wananchi na wapinzani pia. Hali hii inawafanya wapinzani waache kujenga hoja zenye kuibana CCM kuhusu ilivyoshindwa kusimamia na kutumia utajiri na raslimali zilizopo Tanzania kwa manufaa ya watanzania na badala yake wapinzania wanaanza kucheza ngoma ya CCM ya kutoa ahadi lukuki.
Ili kukabiliana na Propaganda za CCM, wagombea wake na viongozi wake mbali mbali ambao wanapatiwa fursa zaidi na vyombo vingi vya habari, DR Slaa na wagombea wote wa CHADEMA wanatakiwa kuwafahamisha watanzania mara kwa mara yafuatayo:-
(i) aina ya madini na ujazo yaliyochimbwa na kuondoka hapa nchini kutoka mwaka 2005 hadi sasa.
(ii) kiasi cha fedha kilichopatikana kama mrahaba duni uliowekwa na Serikali ya CCM.
(iii) kiasi cha fedha Serikali ya CCM ilichopokea kwa niaba ya watanzania kutoka 2005 hadi sasa kutoka kwenye madini.
(iv) Kiasi cha Mrahaba ambao Serikali ya CHADEMA ingeweka kutoka katika madini husika.
(v) kiasi cha fedha ambacho kingeweza kupatikana chini ya utaratibu huo wa CHADEMA kutoka katika madini yaliyochimbwa kati ya 2005 hadi sasa.
(iv) na fedha hizo zingeweza kujenga miundo mbinu, shule, hospitali n.k ngapi.
2) Kiasi cha fedha wafanyabiashara wanachokwepa kila mwaka kutoka 2005 hadi sasa. Na fedha hizo zingeweza kufanya nini katika utoaji huduma za jamii, ujenzi wa miundo mbinu n.k?
3) Kiasi cha fedha kinachokosekana kukusanywa kupitia sekta ya utalii kutokea 2005 hadi sasa. Na fedha hizo zingeweza kufanya nini katika utoaji huduma za jamii, ujenzi wa miundo mbinu n.k?
NB: Dr Slaa na wagoimbea wote wa CHADEMA nchi nzima wajikite katika kuwafafanulia na kuonyesha watanzania kuwa inawezekana watoto wote wa Tanzania wakapata elimu bure kutoka chekechea hadi Kidatu cha Sita;
na kodi ya vifaa vya ujenzi vinavyotumiwa na wanyonge yaani saruji, bati, nondo, misumari n.k vinavyoweza kupunguzwa bila ya kuathiri uendeshaji wa Serikali baada ya CHADEMA kusimamia mukusanyaji apato ya Serikali kama ilivyoonyeshwa hapo juu.
Timu ya Kampeni ya CHADEMA ikumbuke kuwa binadamu ameumbwa kusahau mara kwa mara. Hivyo huhitaji kukumbushwa mara kwa mara. Hivyo watumie kipindi hiki cha Kampeni kurudia rudia mambo haya msingi hususan usimamizi wa madini, kodi, utalii n.k ili wananchi waweze kukumbuka na kutoa adhabu kwa CCM tarehe 31 Oktoba 2010.
Mwana JF yeyote anayeweza kutupatia hizi takwimu hapa atakuwa ametoa msaada mkubwa sana kwa wagombea mbali mbali wa CHADEMA ili kutusadia kuwaeleza watanzania wenzetu kiini cha umaskini wetu na kwanini tunalazimika kufanya mabadiliko kupitia uchaguzi wa mwaka 2010.