Kujiuza

mimi kuna dada nilipewa namba yake,tukawa tunawasiliana sana lakini kabla hata ya kuonana, tayari alianza kunipiga virungu vya,mara leo vocha,mara viatu na suti inayomatch kwa ajili ya ofisini...,gharama yake sijui laki na ngapi...

Sikuwahi kumtumia fedha katika ombi lake lolote...ila nililisitiza kuonana naye kwanza.. Akaanza kuuliza," Kwani we unapenda mwanamke wa aina gani..? Je, kama utaona sina vigezo unavyovitaka je?"

Tulionana na nikamwambia nimefurahi kumuona ni mwanamke mwenye vigezo vyote ninavyovitaka.. Baada ya vinywaji tukaagana..

Tulipoachana na nakafika nyumbani,alinishangaza kwa kunitumia ujumbe kuwa hakufurahia kukutana kwa kuwa sikutoa maneno yoyote ya kumhakikishia kuwa atapata uniform hiyo ya readymade kwa ajili ya ofisini kwao...

Niishie hapo.. Je,huyu atakuwa group gani?
 

Naam, nako ni kujiuza.
 
Tunatakiwa tutofautishe hapa,kwanza mfumo wa maisha na maumbile umewafanya wadada kuwa tegemezi,hivyo kuomba msaada kwa rafiki yake,mpenzi wake au yoyote isiingizwe kwenye mjadala huu,kujiuza kuko kwa jinsia zote,wapo wanaume kazi yao kujipodoa na kujipitisha mbele ya wanawake wenye hela ili wauze sura,huku ni kujiuza,hata wale kaka poa wanapokaa barabarani kutafuta watu wawape hela in return kwa kuingiliwa,huku ni kujiuza,na wale dada poa nao ni hivyohivyo,so mwanamke anapokuwa na mpenzi wake halafu akawa anahudumiwa nae huyu hajiuzi!
 
Hahahaah. . . watu wana vurugu kweli.

Huyo inaonekana alikua anaangalia kama utafikia bei mfanye biashara.

@Wachangiaji
. . . . Thank you guys. . .
Kwa style hii naona asilimia kubwa ya wanawake watakua wanajiuza japo hao hao ndio wakwanze kuwanyooshea wenzao vidole bila kujua kwamba nao ni wale wale.


@Konnie . . . nidai zawadi.
 

Tofauti iko wapi kati ya anaesubiri barabarani na kuaga baada ya masaa na yule anaehamia kabisa kabisa kwa lengo hilo hilo?Wote si wanakubali kutumika kimwili kwaajili ya pesa?
Sema tu mmoja anakua na mteja permanent wakati mwingine anabadili wateja.
 
afu ukumbuke hii ni ya 2
nazitaka valentini dei


inamaana umefunga mjadala mapema hivi?
Naona umefanya koknlusheni.

Sijafunga bana. . sema tu nimeonyesha.kua nimesoma na nimewapata japo sijajibu mmoja mmoja.

Hhhmm we sinilikwambia unipe kijiwe cha kukuachia zawadi yenyewe hujanipa. . .
 
nna vijiwe vitatu tu
PM, MMU na Chit Chat
au unataka utume C/O desh desh?

Hhhmm we sinilikwambia unipe kijiwe cha kukuachia zawadi yenyewe hujanipa. . .
 
ni kweli kabisa mara nyingi watu husema au hutumia neno kujiuza bila sababu za msingi,,
kati ya yote uliyoeleze ni kujiuza ukito tu wanaopiga pamba za kutatanisha na watu kudai wanajiuza wakati dhamira zao hazipo hivyo

yeyote anayetafuta penzi kwa ajili kitu ( material things) huyo ni sawa na anajiuza

maana atatoa penzi ili apate anachotaka

nadhani nimejaribu kidogo
 

vp kwa anayependa kupewa pesa tu na hana hata tone la penzi moyoni?
 
Mi nafikiri si sahihi kusema mwanamke ambaye yupo kwenye uhusiano wa muda mrefu na mwanaume eti anajiuza hata hata km hampendi kwa dhati,

Asilimia kubwa ya wanawake wa kabila fulani huko kaskazini mwa TZ zamani, walipatikana kwa njia ya kutekwa halafu taarifa rasimi inapelekwa kwa wazazi , na huyo alihesabiwa kuwa ameshaolewa je, huyo naye ahesabiwe anajiuza maana hakumpenda mwanaume lkn amelazimika kuishi naye kwa kuwa mila ziliruhusu hali hiyo!?.

Wanaume walichaguliwa wenzi wao na bado mfumo huo unaendelea ktk baadhi ya makabila pasipo kujali km wanapendana au la, na mwanamke anaweza asiwe na kipato chochote hivyo mwanaume anawajibika kwa kila kitu kwa mkewe, jekuna biashara hapo?.

kuna mabinti waliopewa ujauzito wakaozeswa kwa hao waliowapa, wakati wao walikuwa wanaburudishana 2na hatimaye wanalazimika kuwa mke na mume, je kuna biashara hapo?

Hivyo, si sahihi kuwahukumu wanawake waliokwenye nyumba ndogo kwamba wanafanya biashara. Kwa imani ya dini yangu, mwanaume anatakiwa awajibike kumtunza mwenzi wake, ndo maana baadhi ya wanaume hata km wake zao wanafanya kazi bado huendelea kuwajibika kwa familia.

Tamati; anayejiuza jambo la msingi kwake ni soko(wateja) hivyo hachagui mteja ilimradi ana fedha za kulipia huduma, pia mteja anakuwa na mamlaka dhidi ya huduma inayopewa kwa maana hiyo anaweza kuitumia namna atakavyo ilimradi akidhi haja yake pasipo kumjali mtoani, jambo ambalo kwenye mahusiano hayo hapo halipo.
 

Hapo ndipo unapotakiwa uelewe tofauti kati ya mtu KUTAKA/KUPENDA/KUKUBALI mahusiano na mtu kwa ajili ya maslahi binafsi in exchange for his/her body na mtu KULAZIMIKA/LAZIMISHWA kuishi na mtu kwaajili ya mimba= mtoto, familia na mila kama hizo za mwanaume kumkamata mwanamke kwa nguvu.
 
Lizzy,Hebu naomba unisaidie kufafanua,kati ya mahusiano na kujiuza!
 
asilimia 85 ya wanawake wanajiuza au walishawai kujiuza katika maisha yao ,anaebisha aseme
Smile smile hebu nipe kwanza definition ya kujiuza ndio nijue kama nabisha au lah
 
Lizzy, People do whatever they have to in order to survive. I seriously hope you are not judging these kind of people for what they do- after all
at least they are doing something to support themselves - so much better than the people who steals which they are not really entitled and then run other people down.

Give them a break and respect them for what they do and remember your job is what you do not who you are.
 
relax,

kuzungumzia kujiuza is not a taboo, ni suala linalozungumzika si uchawi au ruya ya kupaa hewani usiku

halafu, kusema ukifanya hivi unajiuza na ukifanya hivi hujiuzi haimaanishi una mjaji mtu yeyote.

Kila binadamu ana mapungufu yake, so we are in the same boat.

Siamini kama hii ni kumdhalilisha mtu yeyote hadi tumpe breki, sababu hata tunaojadili hapa unaweza kuta ni wauzaji tu. Hatumdiskasi mtu, tunadiskasi dhana.

Take it easy man.

 

Kuna tofauti kati ya kutaka kuelewa jambo na kuhukumu . Mimi nimetaka kuelewa ndio maana ? ??? ni nyingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…