Kujitoa kwa Mwapachu CCM, Sababu hizi hapa

Kujitoa kwa Mwapachu CCM, Sababu hizi hapa

WanaJF naombeni jibu:Ni kwanini kiongozi yeyote akitoka CCM ndipo panatangazwa mambo yake mabaya?Ina maana wachafu wote wajificha CCM?
 
Kaka, kwa nini usiwe unakaa kimya kama wenzako? unajichora sana na watu tunakusoma jinsi ulivyo kichwani.
Nakushauri utulie, acha kujibizana na watu humu!
Kwa mfano, hapo juu sasa ndo umeuliza nini? kweli?

Kama Ben Saanane ANAFIKIRI KIPOPOMA Hivyo Mkuu Wewe Unadhani Lowassa, Mbowe Na Sumaye WATAKUWAJE Kifikra? Sijutii Kuipenda CCM ( CHAMA CHA MAPINDUZI ) Kwani Mwana CCM Mwenye UPEO FINYU WA KUFIKIRI Kama Wa Huyo Ben Saanane.
 
Ndugu Wanabodi,

Suala la kujitoa kwa ndugu Mwapachu CCM na kudai Kuwa ati CCM siyo mamake, siyo suala geni. Wafukunyungu kama sisi tulilifahamu hili sikunyingi na tulisubiria litokee. Wengine bado wapo an watafuata siku si nyingi!

Kama alivyoeleza yeye binafsi, Mwapachu alikuwa ni TeamLowassa , Lowaasa akiwa bado yuko CCM. Mwapachu ni miongoni mwa makada wa CCM waliokuwa wakigawa fedha za Lowassa pale DODOMA. Mwapachu alikuwa ni miongoni mwa walioratibu msafara wa vijana waendesha bodaboda walioendesha pikipiki hadi Dodoma kumuomba EL agombee Urais. Ni Mwapachu huyu huyu aliandaa (kwa kushirikiana na Team Lowassa) CV za watakaowekwa katika nafasi mbalimbali mara EL atakapotinga Ikulu kupitia CCM.

kubwa zaidi na kilichofanya ajitoe CCM, Balozi Mwapachu ameahidiwa na aliahidiwa nafasi ya UWAZIRI WA MAMBO ya NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA. Tunalifahamu hili na list nzima ya Walioahidiwa Ukuu wa Mikoa, Wilaya, Wizara, Ubalozi, na Ukatibu Mkuu ipo.

Ninachotaka kuwaambia ni kuwa hao wanaotoka CCM siyo kwa sababu wanataka MABADILIKO YA KWELI in kwa sababu wanafuata maslahi. Wanaotaka mabadiliko ha kweli walikuwa CDM tangu hata kabla ya uchaguzi mkuu kuanza. Kuweni makini mnaposhabikia wanaojiondoa CCM muda huu wa kampeni Zambia lala salama!

nawasilisha.

Basi kama ni hivyo ulikuwa unasubiri nini kuandika tangu Lowassa akiwa CCM?
 
WanaJF naombeni jibu:Ni kwanini kiongozi yeyote akitoka CCM ndipo panatangazwa mambo yake mabaya?Ina maana wachafu wote wajificha CCM?

Kama CDM/UKAWA wanasema CCM haifai we unataka wanaotoka humo uambiwe wanafaa???!!

Ndio maana mnaambiwa ni kipindi cha tafakari na akili kuongoza tamaa ya kimawazo na misukumo ya kimakundi. . . .
 
Mbn haya umnayasema baada ya mtu kutoka cku zote ukimjua mtu mbaya wako au hakufai kwako mtoe mapema mbn hamkumfukuza mapema kweli nyie mmekwisha kabisa
 
Dah! yule mzee alisema upepo ukivuma tutaona utupu wa kuku sasa tutaona hata wa kanga...kumbe ccm ndo madudu yenu mnayoyafanya kila anayeondoka mnamtuhumu mhh nadhani hata akihama magu mtamtuhumu...viva lowasa
 
Haya mambo ya kuhama vyama ni mambo ya kawaida nchi zingine. Hapa Tanzania yanatuumiza vichwa kwa kuwa ndio yanaanza. Huu ndio mwanzo na tatayazoea. Uhuru amekua rais wa kenya bila kupitia Kanu chama alichokiasisi babae mzee Jomo.
Mkuu, sina utaratibu wa kuwapongeza wachangiaji wa fact.
Nimeanza leo. Kwako,
Haya mambo ya kuhama chama, ni kawaida sana
Hasa unapoona kinapoteza mwerekeo au kinakosa sera na mengineyo
 
Ndugu Pombe kashindwa hata kusuluhisha mgogoro na mkewe kwa kuwa anajua hatoingia Ikulu! Nyerere alishasema 'uhuni' mtu unaweza kufanyia popote barabarani!
 
Mabadiliko yepi ya kimfumo utayapata kutoka kwa wana mtandao? Nyie watu zishughulisheni akili zenu msiwe mashabiki tu. Hilo liko wazi Lowassa was here kuendeleza mtandao uliotutesa hapa kwa miaka 10 sasa.

Tuonyeshe post yoyote uliyoonyesha kwamba EL alikuwa anawatesa kupitia mtandao kabla ya kuhamia upinzani.
 
Hakuna nafasi za ukuu wa wilaya wala ukuu wa mkoa hawana kazi kwenye serikali ya Lowasa nafasi zao zinafutwa wakurugenzi watawajibika zaidi.kwa mawazo yako hayo umechelewa..

Huo ni ujinga wa Mbowe na hautekelezeki.Hata katiba pendekezwa haikufuta nafasi hzo bali utaratibu wa kuzıpata.Hatuwezi kuondoa tawala za mikoa.Au kutakuwa na mkurugenzi wa mkoa?Hatujawa machizi kııvyo wewe dogo.
 
Hana maslahi tena CCM.Kama ni UBUNGO Kashatemwa.Alimtegemea Lowassa lakini sasa ndiyo hivyo tena. 1.Mimi naomba kuuliza kuhusu Msimamo wa Kingunge katika KATIBA PENDEKEZWA 2.Swali kwa Sumaye,Kingunge na Lowassa.Watuambie Je,Uchaguzi Mkuu wa 1995,2000,2005 na 2010 ulikuwa HURU Na wa HAKI??

Jamaa wanatumia upumbavu wa Watanzania kama mtaji.Acha mijitu ikome.Jitu limeiba,likafungwa, linalalamikia.Watu wanadhanı serikali ya Lowasa maisha yatakuwa holela na kila mtu ataıshi atakavyo.Yetu macho.
 
Kama ni hvo nani msafi ndani ya ccm! Kumbe ukiwa ndani msafi ukitoka nje mchafu hhhhhh.
 
Hana maslahi tena CCM.Kama ni UBUNGO Kashatemwa.Alimtegemea Lowassa lakini sasa ndiyo hivyo tena. 1.Mimi naomba kuuliza kuhusu Msimamo wa Kingunge katika KATIBA PENDEKEZWA 2.Swali kwa Sumaye,Kingunge na Lowassa.Watuambie Je,Uchaguzi Mkuu wa 1995,2000,2005 na 2010 ulikuwa HURU Na wa HAKI??

Wamesema wao niwanamabadiliko na siku 100 za kwanza watashughulikia rasimu ya 2 ya wananchi na sio katiba pendekezwa napo hapo ulipitwa ukupasikia.
 
Hicho kitengo LB7 kinafungwa rasmi oct 24, sasa sina uhakika sana kama ulikuwa unakumbuka hata kutunza nauli ya kurudia kijijini Sitimbi.

Na kitafungwa saa saa tisa alasiri wakati huo matokeo yakiendelea kutangazwa
 
Hivi mnajua kwamba Kikwete atajitoa CCM tarehe 24 Oktoba 2015!!!???au hamjui. Na atamkana Magufuli hadharani. Na yeye mtamzushia lipi!??
 
Vile visu vya cuf zanzibar kabla ya uchaguzi wa 2005 viliingizwa na nini na mbona hadi leo hatujasikia kesi ikitajwa mahakamani? propaganda za ccm zimezoeleka.
Lowassa 2015
 
Wote hao wasaka tonge tu hakuna mwenye uchungu na nchi hii, wangekuwa wanataka mabadiliko ya kweli wangeungana mapema na akina Zitto, mnyika, lissu, silaa, lipumba wakati WA mchakato WA katiba mpya ILA wanaokuja Leo wote wanafata maslahi yao
 
Back
Top Bottom