Kuishi maisha ya movie

Kuishi maisha ya movie

julius mahinya

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
1,152
Reaction score
384
Imekuwa ni kawaida watu kutamaani kuishi maisha ya kwenye movie unakutana na msichana ili umtongoze sharti umuite mahali tulivu apate kinywaji pengine chakula ndio uanze kurusha verse ukiwa hujui atakubali au la lakini mfuko wako umetobolewa nae tiari!

Huyu huyu anayetaka kuoa/kuolewa anategemea akaishi maisha kama alivyoona kwenye movie flani hivi! anadhani maisha ni rahisi kama kwenye movie! baby nipeleke shopping anafika anakusanya rundo la nguo, vipodozi, viatu,n.k huku akitegemea mfuko wako.

Usipotoa hela anaona hujamtendea haki. utasikia mbona wenzio hawako hivyo mtake sasa akupe mfano mtu ambaye hayuko hivyo, hana ila anaona kwenye movie!

Life is performance , life is not rehearsal. Wadada kwa wakaka kila kitu si rahisi kama muonavyo kwenye movie mtu katoka labda kijijini mara tu maisha yamenyooka kafanikiwa na wewe unaiga tu! msichana wa leo namaanisha mwenye hadhi machoni pa watu kumpata ukiwa umevaa kanda mbili unakwatua chini sahau sharti uwe na gari ndio umpate na wengine hudhani mwenye gari ana hela nyingi sana kila akitaka basi lazima umpe unakuta anang'ang'aniza utadhani mchawi.

Na hivi wasanii wetu hawajui wao ndio kioo cha jamii wanacopy maisha yasiyo yetu wanaigiza, movie nyingi hata mtu anaeekiti masikini basi ana nyumba na fursa mbele yake ya kutatua umaskini kitu ambacho sio kweli kwa jamii zetu za kiafrika, kila boss ana gari kwenye karibia kila movie.

Wadada wanatafuta mtu mwenye maisha flani alioona kwenye movie basi ndio aolewe naye huku wakaka nao kuoa ni issue nyingine anataka awe na vitu sawa na watu wa kwenye movie flani ndio aoe!

Maisha ya movie ni rahisi sana ndugu zangu kuliko uhalisia wa maisha sahihi sanaa iliopo haikidhi kutoa elimu na burudani sawa na mahitaji yetu kifupi sio bora. Maana haitatui matatizo ila inayazidisha so better uwe na your own view ya maisha na si kuona flani kavaa nguo flani basi na mimi nataka, yaani mdada yuko busy na movie kisa aishi nae hivyo kwenye maisha halisi.
 
Hivi mtu akikuita tu out of nowhere na kuanza kukutongoza si utamshangaa! Unajengaje urafiki ukishaingia kwenye mahusiano? Manake waswahili sio wahindi, unaingia ndani ndo mnaanza kupendana.

halafu unaenda kumtongozea mtu sea cliff, na akiwa na high demands unaanza kununa.

#wanaumekiinichamabadiliko
#dontbefake
Nje na maisha ya maghribi watu wanatongozanaje?
 
hollywood life,spitual husbands but all in all onyesha uhalisia from 0 day ,kama vipi unachomekea disc kwenye daladala la m,bagala hilihilo wakati limejaza
 
Ifike mahali wanaume wawe real waache kujifake nao. Unakuta mtu kaazima hadi gari, kakopa fedha hii yote ni kwasababu anataka kujiweka kwenye nafasi ambayo hayupo lakini anaitanamani sasa unapokutana na dada kwenye hotel kubwa for the first time una mwachia laki kadhaa za usafiri na kila kidate unabehave the same lazima aishi maisha ya tamthilia
 
Hivi nini hapa duniani sio cha kuiga????!!!
Watu wanavuna shambani saa hizi we unapost hapa!!!!!

Maisha ni kujifunza na mafunzo hayaishi leo wala kesho ,ukishajifunza vya kutosha unaanza hiyo "performance" katika jukwaa linalokufaa sasa kama wewe mtu wa sarakasi ukajituka jukwaa lenye tiles, aga fasta!!!!!

Kama wewe ni wa maigizo lakini hakuna sehemu ya kubadilishia "attires" fikiria mara mbili!!!!!

Performance inategemea performer na audience, mabadiliko huanza na wewe!!!!!
 
Ifike mahali wanaume wawe real waache kujifake nao. Unakuta mtu kaazima hadi gari, kakopa fedha hii yote ni kwasababu anataka kujiweka kwenye nafasi ambayo hayupo lakini anaitanamani sasa unapokutana na dada kwenye hotel kubwa for the first time una mwachia laki kadhaa za usafiri na kila kidate unabehave the same lazima aishi maisha ya tamthilia

Wanapata anachokitaka????!!!
Wanaridhika na hiyo drama yao???!!!
 
Wanapata anachokitaka????!!!
Wanaridhika na hiyo drama yao???!!!

OLESAIDIMU mwanamke umesha mtreat hivyo mara kadha sasa unapoanza kujiweka kwenye hali yako ya ukweli (uhalisia) na dada anaendelea kudemand vitu vikubwa ili hali mwanaume hayupo kwenye position ya kuprovide ndio mnaanza kulalamika sasa kama hivi.Lakini ukijionesha true color yako tangu mwanzo wa mahusiano yako mwanamke akidemand vitu vikubwa ni mwehu.
 
Maisha ya director yanapokuja kwenye real life, lazima mvurugano uwepo
 
OLESAIDIMU mwanamke umesha mtreat hivyo mara kadha sasa unapoanza kujiweka kwenye hali yako ya ukweli (uhalisia) na dada anaendelea kudemand vitu vikubwa ili hali mwanaume hayupo kwenye position ya kuprovide ndio mnaanza kulalamika sasa kama hivi.Lakini ukijionesha true color yako tangu mwanzo wa mahusiano yako mwanamke akidemand vitu vikubwa ni mwehu.


Hakuna mwehu kati ya hao!!!
Wote wana akili timamu kabisa! !!!!
Na ukitaka kujua wapo timamu subiri mmoja kati yao aone hatari ya kufilisika,kuachwa,matakwa kutotimizwa au vyote kwa pamoja!!!!
 
inaboa kupita kiasi hali kama hii.

Yani hadi leo unamuita mtu mahali ili mle kisha umtongoze
masikini sijui ndo unaanzaje " dada nikinywa maji nakuona kwenye glass, silali nakuota"
acha tu ufanyiwe movie kwakweli kama ndo hivo
 
hivi siku hizi bado kuna kutongozana kwa kuitana mahali??? mnawapata wapi wanawake wa hivo?
 
Back
Top Bottom