Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,209
- 42,070
Ikumbukwe kwamba Maelfu ya watu wana tumia dawa za kurefusha maisha,lakini cha kushangaza imebainika kuingizwa dawa bandia za kuferusha maisha. Hivyo mamlaka ya dawa imeagiza ziondolewe mahospitalini, zimebainika zina jenga usugu kwa virusi vya UKIMWI.
Maelfu ya watu walioathirika kwa ugonjwa wa ukimwi ambao kwa sasa wanatumia Dawa za kurefusha maisha (ARVs) nchini wapo hatarini kufupisha maisha yao baada ya kubainika kuwa toleo mojawapo la dawa hizo la machi 2011 ni bandia.
Uchunguzi unaonesha kuwa dawa hizo zilizosambaa katika mikoa ya Dares-salaam, Tanga na Mara zilianza kusambazwa tangu Mei mwaka huu na hadi sasa bado zipo sokoni,jambo lilio ilazimu Mamlaka ya Chakula na dawa Tanzania (TFDA) Kuagiza zirudishwe Bohari kuu ya Dawa (MSD).
MSD wame ahidi kutoa taarifa leo kuhusu kiasi cha dawa bandia zilizo sambazwa kwa wananchi wakati huohuo ni zaidi ya watu zaidi 400,000 wameshatumia hizi dawa.
Ni wakati umefika kwa serikali kuonesha uwajibikaji wa wazi katika mambo ya msingi na kuondokana na tabia ya kulindana huku wananchi wakizidi kuteketezwa kwa uzembe wa watu wachache.
Tunaweza kujiuliza nini kazi ya TFDA kama dawa feki zinapita kirahisi namna hii?
TFDA wamefanya uzembe wa kuruhusu dawa feki na kujidai kushituka wakati dawa zimesha samba nchini, je walikuwa wapi sikuzote na kwa nini hawakufanyia uchunguzi wa kina dawa hizi kabla ya kuruhusu kusambazwa?
Tujiulize ni nani na ni kiwanda gani kimetengeneza dawa hizi?
Ni nani aliye ruhusu dawa hizi kuwa zina faa kutumika kama siyo hawa hawa TFDA?
Ni vyema katika swala hili siasa ikawekwa pembeni na serkali kuwawa jibisha yeyote aliye husika katka uingizwaji wa dawa hizi bandia, na serikali inatakiwa ijue imeanza kuonesha kwa vitendo inavyo leta michezo ya kubahatisha kwenye maisha ya watu.
Source: Mwanachi
Maelfu ya watu walioathirika kwa ugonjwa wa ukimwi ambao kwa sasa wanatumia Dawa za kurefusha maisha (ARVs) nchini wapo hatarini kufupisha maisha yao baada ya kubainika kuwa toleo mojawapo la dawa hizo la machi 2011 ni bandia.
Uchunguzi unaonesha kuwa dawa hizo zilizosambaa katika mikoa ya Dares-salaam, Tanga na Mara zilianza kusambazwa tangu Mei mwaka huu na hadi sasa bado zipo sokoni,jambo lilio ilazimu Mamlaka ya Chakula na dawa Tanzania (TFDA) Kuagiza zirudishwe Bohari kuu ya Dawa (MSD).
MSD wame ahidi kutoa taarifa leo kuhusu kiasi cha dawa bandia zilizo sambazwa kwa wananchi wakati huohuo ni zaidi ya watu zaidi 400,000 wameshatumia hizi dawa.
Ni wakati umefika kwa serikali kuonesha uwajibikaji wa wazi katika mambo ya msingi na kuondokana na tabia ya kulindana huku wananchi wakizidi kuteketezwa kwa uzembe wa watu wachache.
Tunaweza kujiuliza nini kazi ya TFDA kama dawa feki zinapita kirahisi namna hii?
TFDA wamefanya uzembe wa kuruhusu dawa feki na kujidai kushituka wakati dawa zimesha samba nchini, je walikuwa wapi sikuzote na kwa nini hawakufanyia uchunguzi wa kina dawa hizi kabla ya kuruhusu kusambazwa?
Tujiulize ni nani na ni kiwanda gani kimetengeneza dawa hizi?
Ni nani aliye ruhusu dawa hizi kuwa zina faa kutumika kama siyo hawa hawa TFDA?
Ni vyema katika swala hili siasa ikawekwa pembeni na serkali kuwawa jibisha yeyote aliye husika katka uingizwaji wa dawa hizi bandia, na serikali inatakiwa ijue imeanza kuonesha kwa vitendo inavyo leta michezo ya kubahatisha kwenye maisha ya watu.
Source: Mwanachi