ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,956
- 7,003
Nimeona Waziri wa Maliasili na Utalii analalamika kuwa kuna dereva amepita mikumi akiwa kasi na VX V8 amemgonga swala na hajasimama. Haya ni maoni yangu:-
1. Gari hilo lazima linamilikiwa na kada wa CCM.
2. Dereva wa gari au mmiliki anajua hawana cha kumfanya.
3. Anaamini hata akikamatwa, yataishia kuwa mazungumzo na case inaisha.
Kwa tukio hili ni ishara kuwa CCM wanajiona wana haki zilizozidi kuliko wengine ndani ya nchi hii.
Na tabia hizi wamezionesha kwa kufanya figisu kwa wagombea wa vyama vingine. Wao wanajiona nchi hii ni mali yao. Ukofika kwenye maeneo ya wazi, utaona bendera za ccm, vyama vingine vikiweka zinatolewa.
Mabango ya kampeni utayakuta ya ccm, upinzani wakijaribu yanachanwa. Mikutano ya ccm mingi inavunja kanuni lkn hutasikia wanachukuliwa hatua. Yote hii wanajiona wana hati miliki ya kufanya lolote kwenye nchi hii.
Tabia za namna hii ndio zimebadili kura yangu kutoka ccm kwenda kwa Tundu Lisu. Lengo aje anyooshe usawa wote tuwe sawa mbele ya sheria.
Inakera kuona vyombo vya serikali kutumika kulinda CCM. Inakera sana
1. Gari hilo lazima linamilikiwa na kada wa CCM.
2. Dereva wa gari au mmiliki anajua hawana cha kumfanya.
3. Anaamini hata akikamatwa, yataishia kuwa mazungumzo na case inaisha.
Kwa tukio hili ni ishara kuwa CCM wanajiona wana haki zilizozidi kuliko wengine ndani ya nchi hii.
Na tabia hizi wamezionesha kwa kufanya figisu kwa wagombea wa vyama vingine. Wao wanajiona nchi hii ni mali yao. Ukofika kwenye maeneo ya wazi, utaona bendera za ccm, vyama vingine vikiweka zinatolewa.
Mabango ya kampeni utayakuta ya ccm, upinzani wakijaribu yanachanwa. Mikutano ya ccm mingi inavunja kanuni lkn hutasikia wanachukuliwa hatua. Yote hii wanajiona wana hati miliki ya kufanya lolote kwenye nchi hii.
Tabia za namna hii ndio zimebadili kura yangu kutoka ccm kwenda kwa Tundu Lisu. Lengo aje anyooshe usawa wote tuwe sawa mbele ya sheria.
Inakera kuona vyombo vya serikali kutumika kulinda CCM. Inakera sana