Kuhusu Mama...Hii imekaaje?

Kuhusu Mama...Hii imekaaje?

Wewe unataka kusafirishiwa bure kwa kuwa tu ni mama yako?!!! Hata kama ni mama yako mzazi kama una shughuli zako za kukuingizia kipato, mrudishie mkwanja wake. Watu wengine bwana, umeambiwa akiwa mama yako ndio uwe kupe??!!!
 
Yaani mamako alikulea na kukulisha ukiwa mdogo. Na bado unataka aendeleze malezi? Una tabia mbaya, kwanza kabla hata hajakuambia umrudiishie hela ungetuma na ya ziada kabisa asiingie mfukoni kutuma vitu vyako! Ukiambiwa gharama ya kutuma ni laki 2 unatuma tatu kabisa just in case. Na usisahau kumtumia mamako hela hata kama hajaomba wala kuwa na kazi ya kukufanyia.
Halafu eti anajiita Father. Hizi ni tabia za kifather kweli??!!!! Mimi amenishangaza sana kwa kweli. Huyu ndio wale ambao anaenda kukaa kwa mtu bila mpango eti kwa kuwa tu ni ndugu yake.
 
..Halafu unajiita " a father" yaani we unadhani mama ana jukumu la kukufanyia we kila kitu bure bure tuu.. We mwanaume wa aina gani? Unatutia aibu! Mwanaume majukumu kaka sio unakuja kulia hapa jf eti mama anakudai hela ya kukutumia vitu vyako. Khaa!
Huyu jamaa kaniudhi sana. Labda tumuulize umri wake, ukute ni kavulana ka miaka 14.
 
Mambo mrembo!
Yaani mamako alikulea na kukulisha ukiwa mdogo. Na bado unataka aendeleze malezi? Una tabia mbaya, kwanza kabla hata hajakuambia umrudiishie hela ungetuma na ya ziada kabisa asiingie mfukoni kutuma vitu vyako! Ukiambiwa gharama ya kutuma ni laki 2 unatuma tatu kabisa just in case. Na usisahau kumtumia mamako hela hata kama hajaomba wala kuwa na kazi ya kukufanyia.
 
Vipi mkuu, una umri wa miaka mingapi?
Habari zenu watumiaji wa JF wenzangu?
Tupeane uzoefu kama ishawahi kukutokea, kwa wale tuliojaliwa kuishi na Mama.
Mama anaomba kurudishiwa gharama zake anazotumia juu yangu, mf: kanitumia kitu niko mbali na home, anadai nimlipe, amenisafirishia vifaa vyangu nilivyoviacha nilikokuwa nikiishi before, anadai nimrudishie alichotumia.
==========================
NOTE: si kuwa hana kazi wala cha kumuingizia kipato.
==========================
Hii imekaaje??? Imewahi kukutokea???
Au kwa kuwa si Mama mzazi???
Je, Mama mzazi anaweza kufanya hivyo???
 
Yaani mamako alikulea na kukulisha ukiwa mdogo. Na bado unataka aendeleze malezi? Una tabia mbaya, kwanza kabla hata hajakuambia umrudiishie hela ungetuma na ya ziada kabisa asiingie mfukoni kutuma vitu vyako! Ukiambiwa gharama ya kutuma ni laki 2 unatuma tatu kabisa just in case. Na usisahau kumtumia mamako hela hata kama hajaomba wala kuwa na kazi ya kukufanyia.

Kama hela ya kusafiriaha miZigo yake tu analalamika, hela ya matumizi mama yake ndo aisahau hakuna dalili za mtoa mada kumtumia


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kijana unapenda kulelewa wewe lo!!!,mara ya mwusho kumtumia hela mamako lini, inaonesha mama amekuchoka kwa ubahili wako!!badilika
 
Tuma hela ndugu, hata kama anakazi na sio mama mzazi mbona kakuhudumia mpaka hapo ulipo.
Ye pia anaweza kuwa na mahitaji zaidi yako
 
Mama yangu mzazi ukimuomba akutumie kitu pesa yake unalipa,ila akiamua mwenyewe hiyo ni kama zawadi...pesa haina cha mama mzazi wala baba mzazi atii
 
Mama hakutakiwa kabisa kukuomba gharama ila wewe ulitakiwa umtumie hadi ya usumbufu
 
Tatizo unapenda vya bure,,,, siku nyingine tumia kampuni ikusafirishie hivo vitu kusumbua tu mama yako na kutoa hela bahili.
 
Mama wa kambo tuna kazi...! Hata umpe roho yako haitatosha! Mwe....!
 
Back
Top Bottom